Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,576
- 2,500
Wakuu wenye uzoefu hivi ukifuga fisi unakuwa unamfanyia nini? Yani anakuwa kama mbwa au?
===
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Simon Simalenga, ametangaza msako mkali wa fisi baada ya tukio la kushambuliwa na kuuawa kwa kondoo 21 katika Mtaa wa Mahina. Amesema uchunguzi unaendelea kubaini kama kweli fisi ndio wahusika wa tukio hilo.
Simalenga ameagiza kufanyika kwa operesheni katika maeneo yote yenye vichaka ndani ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi kutokana na taarifa za kuonekana kwa wanyama hao.
"Tutafanya msako kwenye maeneo yote, maana tumeanza kusikia na kuona uwepo wa hawa wanyama," alisema Simalenga.
Aidha, amewatahadharisha wananchi wanaodaiwa kufuga fisi kuacha mara moja, kwani msako huo utawahusisha pia wale wote wanaomiliki wanyama hao kinyume cha sheria.
===
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Simon Simalenga, ametangaza msako mkali wa fisi baada ya tukio la kushambuliwa na kuuawa kwa kondoo 21 katika Mtaa wa Mahina. Amesema uchunguzi unaendelea kubaini kama kweli fisi ndio wahusika wa tukio hilo.
Simalenga ameagiza kufanyika kwa operesheni katika maeneo yote yenye vichaka ndani ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi kutokana na taarifa za kuonekana kwa wanyama hao.
"Tutafanya msako kwenye maeneo yote, maana tumeanza kusikia na kuona uwepo wa hawa wanyama," alisema Simalenga.
Aidha, amewatahadharisha wananchi wanaodaiwa kufuga fisi kuacha mara moja, kwani msako huo utawahusisha pia wale wote wanaomiliki wanyama hao kinyume cha sheria.