DC Muro unatakiwa sasa ukamuombe msamaha Mkurugenzi mpya wa tume ya taifa ya uchaguzi Dr. Mahera

wankuru nyankuru

JF-Expert Member
Feb 11, 2019
491
763
Kwa kweli kwa siku ya leo nimefurahi sana kwa kitendo kilichofanywa na Rais Magufuli kwa kumteua Daktari Mahera kuwa mkurugenzi mpya wa tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Kama mtakavyokumbuka miaka ya hivi karibuni Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro alimfokea hadharani Dk. Mahera kisa kachelewa kwenye msafara wa Muro,cha kushangaza alifokewa mbele ya Mkuu wa Mkoa, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na wilaya.

Licha ya Dk. Mahera kujitetea kuwa usafiri ulipata itilafu DC Muro aliendelea kumwambia kuwa Mkurugenzi usicheke acha dharau bila kujua kimaumbile ndivyo alivyouumbwa.

Kwa tukio la leo lililofanywa na Rais ni fundisho tosha kwetu wanasiasa na hata tusio wanasiasa .

Hivyo, DC Muro unapaswa uende ukamuombe msamaha Dr. Mahera kwani ni boss mkubwa sasa.
 
Mbwa kala mbwa....no issues
 
Alimnyooshea kidole huku akimwambia "Ni upuuzi huo"
 
Kwahiyo unataka kutusadikisha kuwa kuwafokea watu walioko chini yako kwenye mamlaka ni kosa kwakuwa tu ipo siku wanaweza kukuzidi madaraka...!
 
Kwa taarifa yako,Mahera hajapanda Cheo. Amebadilishwa majukumu tu. Tena kimkakati....
 
Hakujua kama Dk ni Tiss,s mbobezi!


Mahera ni kichwa na hutegemewa sana na wanakitengo kwa mambo mengi sasa huyo dogo japo mimi ni mwenzangu lakini wakati ule alifanya ujinga!
Kwa hiyo ni kama "chizi" mpya?
 
Hao vijana wa magufuli hakuna mwenye busara wao kila kitu ni kutumia nguvu bila hata ya kuangalia umri wa mtu sasa hayo ndiyo matokeo yake
 
Punguza emotions, magufuli ndo ana matatizo, si angemfukuza Huyo muro kwa ukosefu wa maadili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…