wankuru nyankuru
JF-Expert Member
- Feb 11, 2019
- 477
- 750
Kwa kweli kwa siku ya leo nimefurahi sana kwa kitendo kilichofanywa na Rais Magufuli kwa kumteua Daktari Mahera kuwa mkurugenzi mpya wa tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Kama mtakavyokumbuka miaka ya hivi karibuni Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro alimfokea hadharani Dk. Mahera kisa kachelewa kwenye msafara wa Muro,cha kushangaza alifokewa mbele ya Mkuu wa Mkoa, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na wilaya.
Licha ya Dk. Mahera kujitetea kuwa usafiri ulipata itilafu DC Muro aliendelea kumwambia kuwa Mkurugenzi usicheke acha dharau bila kujua kimaumbile ndivyo alivyouumbwa.
Kwa tukio la leo lililofanywa na Rais ni fundisho tosha kwetu wanasiasa na hata tusio wanasiasa .
Hivyo, DC Muro unapaswa uende ukamuombe msamaha Dr. Mahera kwani ni boss mkubwa sasa.
Kama mtakavyokumbuka miaka ya hivi karibuni Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro alimfokea hadharani Dk. Mahera kisa kachelewa kwenye msafara wa Muro,cha kushangaza alifokewa mbele ya Mkuu wa Mkoa, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na wilaya.
Licha ya Dk. Mahera kujitetea kuwa usafiri ulipata itilafu DC Muro aliendelea kumwambia kuwa Mkurugenzi usicheke acha dharau bila kujua kimaumbile ndivyo alivyouumbwa.
Kwa tukio la leo lililofanywa na Rais ni fundisho tosha kwetu wanasiasa na hata tusio wanasiasa .
Hivyo, DC Muro unapaswa uende ukamuombe msamaha Dr. Mahera kwani ni boss mkubwa sasa.