DC Muro matatani kwa deni la miaka mitatu

DC Muro matatani kwa deni la miaka mitatu

You must be very stupid, milioni moja ni pesa kidogo? Hivi unajua kwenye biashara hiyo TV na hiyo home theater pengine faida yake zote mbili ni sh laki tano??? Sasa kama hajalupa hilo deni it means siyo tu kwamba faida imeliwa but na mtaji wa hizo bidhaa imekata kwa laki 5? Halafu miaka 2 na bado unataka amdai kwa siri eti tuu kwa kuwa ni kada mwenzako!! Hebu acha kuwa mpumbavu pale mtu anapidai chake.
Nimejibu kitu ambacho nina uzoofu nacho; mahakama ya wilaya (Resident Magistrate) haiwezi kupokea hiyo kesi; labda mahakama ya Mwanzo
 
Angemwachia tu,mkuu wa wilaya ni mtu mzito sana,anaweza kumfanya chochote,wakati wowote...
 
Yaani huyu alikua Hana tiivii flat skrin Hadi alipokopa. Ukiwaona kwenye STK utadhani Ni watu wa maana. Kumbe... Si ajabu na kule TARA na BRANCH anadaiwa.
 
Angemwachia tu,mkuu wa wilaya ni mtu mzito sana,anaweza kumfanya chochote,wakati wowote...
Hana ubavu huo na akileta za kuleta mkulu akisikia hata huo ukuu wa wilaya atausikia kwenye redio. Makonda ametemwa itakua Muro?
Acha aendelee kujiharibia na ajue DSO Ana hizo taarifa
 
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro ameingia matatani na wamiliki wa duka la samani za majumbani la Future correct la jijini Arusha na wanatarajia kumshitaki kwa boss wake ama mahakamani Baada ya kugoma kulipa deni la sh, milioni 1,050,000 kwa muda wa miaka mitatu baada ya kukopa samani za ndani zenye thamani ya sh,milioni 4.4.

Kwa mujibu wa wamiliki wa duka hilo lililopo barabara ya Uhuru (Uhuru Road) jijini Arusha ,Muro ambaye ni mwakilishi wa Rais wilayani humo alikopa TV yenye ukubwa wa inchi 65 yenye thamani ya sh. Mil. 3.2.mnamo Tarehe 10/12/2018.

Pia anadaiwa kukopa radio aina ya (Home thieta) yenye thamani ya Tsh. milioni 1.2 vyote vikiwa na thamani ya Tsh. 4,400,000.

Inadaiwa kuwa siku hiyo baada ya kukabidhiwa mzigo huo Muro alilipa advance ya Tsh. 1,500,000 na deni kubaki Tsh. 2,900,000/.

Mnamo February 2,2020 Muro alilipa sh. Milioni 1 na kubaki sh. Million 1.9, pia tarehe 22/5/2020 alilipa sh. 350,000/ na tarehe 17/6/2020 alilipa sh. 500,000 na hivyo deni kubaki sh. 1,050,000/

Baada ya malipo hayo Muro aliendelea kusumbua deni hilo kwa miaka miwili mfururizo hadi Septemba 5 mwaka huu ambapo alidai lean a hawezi kulipa tena kiasi hicho cha fedha na kuwataka wakalalamike popote.

Lakini baadaye alibadilisha kauli na kudai kwamba atalipa januari mwakani jambo ambalo limesababisha usumbufu kwa mwenye Mali na ukizingatia kwamba wanapaswa kulipa kodi ya Serikali .

Wamiliki wa duka hilo wamempa Siku saba awe amelipa deni hilo kwani kwa kutofanya hivyo watamfikisha mahakàmani .

View attachment 1564018
Hiyo pesa ni kidogo sana kwa muro kushindwa kulipa. Hao wafanyabiashara Wameamua tu kumchafua
 
Na akifikishwa mahakamani itakuwa ni kesi ya uhujumu uchumi maana amesababisha mfanyabiashara kuchelewa kulipa kodi hivyo kuliingizia hasara taifa
 
Nimejibu kitu ambacho nina uzoofu nacho; mahakama ya wilaya (Resident Magistrate) haiwezi kupokea hiyo kesi; labda mahakama ya Mwanzo
Unafahamu Manji alikuwa anamdai Mengi shilling moja mahakamani!
 
Mwakilishi wa Mhe. Rais anatakiwa kuwa mwadilifu na weledi usiobishaniwa. Taarifa zitakuwa zimemfikia Mhe. Rais na huyo jamaa haki yake ni kutopewa nafasi tena ya uDC awamu ijayo.
 
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro ameingia matatani na wamiliki wa duka la samani za majumbani la Future correct la jijini Arusha na wanatarajia kumshitaki kwa boss wake ama mahakamani Baada ya kugoma kulipa deni la sh, milioni 1,050,000 kwa muda wa miaka mitatu baada ya kukopa samani za ndani zenye thamani ya sh,milioni 4.4.

Kwa mujibu wa wamiliki wa duka hilo lililopo barabara ya Uhuru (Uhuru Road) jijini Arusha ,Muro ambaye ni mwakilishi wa Rais wilayani humo alikopa TV yenye ukubwa wa inchi 65 yenye thamani ya sh. Mil. 3.2.mnamo Tarehe 10/12/2018.

Pia anadaiwa kukopa radio aina ya (Home thieta) yenye thamani ya Tsh. milioni 1.2 vyote vikiwa na thamani ya Tsh. 4,400,000.

Inadaiwa kuwa siku hiyo baada ya kukabidhiwa mzigo huo Muro alilipa advance ya Tsh. 1,500,000 na deni kubaki Tsh. 2,900,000/.

Mnamo February 2,2020 Muro alilipa sh. Milioni 1 na kubaki sh. Million 1.9, pia tarehe 22/5/2020 alilipa sh. 350,000/ na tarehe 17/6/2020 alilipa sh. 500,000 na hivyo deni kubaki sh. 1,050,000/

Baada ya malipo hayo Muro aliendelea kusumbua deni hilo kwa miaka miwili mfururizo hadi Septemba 5 mwaka huu ambapo alidai lean a hawezi kulipa tena kiasi hicho cha fedha na kuwataka wakalalamike popote.

Lakini baadaye alibadilisha kauli na kudai kwamba atalipa januari mwakani jambo ambalo limesababisha usumbufu kwa mwenye Mali na ukizingatia kwamba wanapaswa kulipa kodi ya Serikali .

Wamiliki wa duka hilo wamempa Siku saba awe amelipa deni hilo kwani kwa kutofanya hivyo watamfikisha mahakàmani .

View attachment 1564018
Aende kukopa kwa Haji Manara alipe hilo deni!
 
Bora Mo alichomoa mkopo wa boda boda kwa Hamisa!
Pengine angeishia kulipwa mia tano tu!
 
Jamaa naye anaisoma namba kimya kimya.Ukimkuta kwenye ndinga ya serikali alivyo na mbwembwe huwezi kujua nyumbani anatizama Tv ya mkopo aliyoshindwa kulipia.Awamu ya 5 na viongozi wake.
 
Unafahamu Manji alikuwa anamdai Mengi shilling moja mahakamani!
Shilling moja haikuwa DENI bali ni FIDIA. Hapa linazungumziwa deni la TZS 1,050,000 la TV. Mahakama haiwezi kuandikisha kesi ya kiasi hicho
 
Anataka vitu vizuri na pesa hana anataka nani amlipie?
Aseme kama anataka kulipiwa nimlipie.?!((
 
Back
Top Bottom