ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Umejuaje mimi Muislam?
Nimesema, ukimvua Mwanamke hijab umedhalilisha alama ya Uislam na umemnyanyasa mwanamke, hata kama itakuja kugundulika kwamba aliyevaa vazi hilo si Muislam.
Kama ambavyo, kwa mfano, ukimkuta mtu amebeba Biblia, ukampokonya ukaikanyaga, umedhalilisha nguzo na alama ya Ukristo na Wakristo, hata kama itaja gundulika baadae kwamba aliyekuwa amebeba biblia ile si Mkristo.
Una upeo wewe wa kujibu hiyo hoja rahisi bila kukimbilia kusema mimi ni Muislam?
kwenye red bolded
Ukristo uko tofauti. Ukifanya hivyo, umejidhalilisha wewe na si Kristo wala mkristo.
Mkristo atakaye geuka na kukupiga au kuonesha gadhabu juu yako, huyo ni wa jina tu. Wakristo wamefundishwa kusamehe na zaidi kumwombea akukoseaye REHEMA.
Kama ni kudhalilishwa, kutukanwa, kuvuliwa nguo, kutemewa mate, kuchomwa mikuki na kupigiliwa misumari yote aliyabeba Kristo msalabani, mwisho wa siku AKAWAOMBEA REHEMA..."BABA WASAMEHE KWA KUWA HAWAJUI WALITENDALO..."
Mifano ipo mingi. Mwanza makanisa mawili ya Lumala na Pasiansi yote ya Tanzania Assemblies of God (TAG), yamechomwa moto. zaidi ya kutoa taarifa kwenye vyombo vya usalam NO FATHER ACTION.
HAKUNA MATAMKO, WALA HAKUNA KUTANGAZA UHASAMA NA WAISLAMU, bali kuwaombea rehema.
".....mtu yeyote akitaka kunifuata, ajikane mwenyewe, anifuate...."