Elections 2010 DC Igunga ni mkristo mkatoliki; Kwanini hajasema kitu?

Inawezekana, maana Kubenea ana jina la kiislamu lakini si muislamu kwa sababu anatumikia maadui wa Uislamu. Munafiq ni mbaya kuliko twanghut!
 
Me nadhani its hi time kwa BAKWATA kuomba radhi umma wa wadanganyika kwa kudandia treni kwa mbele...!! Next time wawe wanafanya tathmini yakinifu kabla ya kuja na kauli zisizo na mashiko badala yake wanaumbuka buuree...!!
 
Duh hatari kubwa BAKWATA watakuja na lipi tena kutumiwa kijinga kubaya.
 
Wala sio Kubenea na mwanahalisi, ilishatolewa JF mapema tu kuwa huyu mama si mwislam, labda mwanahalisi waliiona humu wakaifatilia kwa undani zaidi. Kwahiyo hapo afichui chochote, zaidi ya kuhabalisha wasiojua kama wewe.

Sio busara kubeza maoni ya watu hapa JF, hata kama hiyo issue ilitolewa hapa JF kuna ubaya gani kwa mtu huyu aliyeifahamu habari hii kupitia Mwanahalisi kutoa maoni yake?, be fair please hatugombani hapa.
 
Duh hatari kubwa BAKWATA watakuja na lipi tena kutumiwa kijinga kubaya.

Siyo Bakwata tu hata habari leo, Uhuru, Radio imani, wanazuoni wa kiislama nao walishupalia na kusema amedhalilishwa Mwislam mwenzao. Sasa mbona hawatoi matamko mengine. Udini bwana na ubaguzi wowote haufai. Mwisho wake dhambi hiyo ya ubaguzi wa kidini itawatafuna hadi kwenye moto usiozimika.
 
Habari tulizo zipata kutoka kwa familia ya mzee joseph kimario(mume wa bi kimario) ambaye ni dc wa igunga mkoani tabora zimeeleza kwamba mkuu wa wilaya amebatizwa ktk kanisa katoriki mbezi beach.

Na mume wake mr joseph kimario ni mwenyekiti wa uongozi wa parokia mbezi beach. Hivyo tunawaomba bakwata wasitumie vibaya vyombo vya habari kueneza udini tanzania.

4 more information vist PAROKIA YA BIKIRA MARIA MBEZI BEACH.


Naona DC atakuwa hautaki ukristo ndio maana hajasema..automatically anakuwa muislamu
 
Bakwata wanasema kuwa ni "mwanamke Muislam " kwa sababu mamlaka yao ipo kwenye Muislam. Tamwa na ndugu zake wao walipaswa kutetea mwanamke na CCM walipaswa kumtetea kama Mwana CCM.

Hapa kinachoonekana ni nani hodari wa propaganda tu.
Historia iliyowekwa kwanza licha ya kukosa ushahidi, haimaanishi kuwa kuvuliwa mtandio uliokwenda na nguo za kujistiri zisizobana sio vazi lililoamriwa kwa Waislam na pale Bi. Fatuma ameliwakilisha kuliko Waislam wengine au wenyewe.

Nafsi yangu ninawajua wanawake wengi walioolewa na Wakristo wakaendelea na dini zao na walipofika utuuzimani wakashika dini zaidi na kuvaa kama dini zao zinavyotaka ambapo hatua kubwa wanayofanya pia ni kujitenga makazi kimakazi na waume zao.

Kwa la huyu mama sijui, ila shamba la mumewe kufuga nguruwe au kuwa aliolewa na mkiristo hakumuondolei dini yake kama anayo. Naamini hakuna binaadamu aso dhambi kwa mujibu wa maamrisho ya dini afuatayo na angeamua kukaa chini angepata mengi ya kutafakari na kujutua

Pili hatujui Kama aliwathibitishia Bakwata kuwa yeye ni Muislam au la. Kwa vile Bakwata ni culprit wazoefu basi tunataka sana tuone na kwa hili pia waliokosea.Tunataka sasa atoe tamko rasmi kusema yeye ni Muislam. Kwangu huo nauona ni udhalilishaji wa aina nyengine kuwa sasa mtu alazimike kusimama mbele ya umma kulinda Imani yake!

Nadhani kimsingi hoja yako ingesimama vyema iwapo Bi Fatuma si Muislam na angesimama kupinga na kusema "yeye si Muislam" ili Bakwata iache kumtetea. Na ikiwa yeye ni Muislam hakuna lazima yoyote ya kusema hivyo kwa vile haki Yake tayari anaipata.

Sishabikii Bakwata kufikia kutoa matamko makali kiasi hiki, lkn haki ya kufanya hivyo wanayo kwa vile wanaemtetea anawakilisha Uislam.

Chadema did wrong kumvua mtu stara yake ambayo bila ya hiyo mwanamke Yule haamini kuwa kastirika. Purukushani ingetokea na wakamchanua blouse yake jee? Wangemtoa hivyo hivyo au wangemstiri? Ukosefu wa tact wameshindwa kuelewa kuwa mtandio na blouse una hadhi sawa kwa baadhi ya watumiaji. Na ikiwa jibu ni kuwa hata Kama angevuka blouse wangemtoa hivyo hivyo, I got nothing but to shake my head

(now hizi propaganda za JF aside mpaka zitakapoandikwa walau kwenye gazeti manake hapa mtu can say anything wala haombwi ushahidi na tunaamini kwa vile tu ni yenye kutupendeza)
Mbona kuna vibaka chungu nzima baadhi wakiwa waislam wanavuliwa nguo na kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali lakini BAKWATA haijawahi kulaani udhalilishaji huo wa wazi?
 
Inawezekana, maana Kubenea ana jina la kiislamu lakini anatumikia maadui wa Uislamu. Munafiq ni mbaya kuliko twanghut!
Ndo tatizo kubwa mlilonalo kila mmoja anajiona msafi kuliko mwenzake. Sasa wee unajiona muislam zaidi kuliko kubenea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom