DC Chuachua: Marufuku magari yanayofanya matangazo ya misiba jijini Mbeya

mshale21

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
2,049
4,904
Mbeya. Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk Rashid Chuachua amepiga marufuku magari yanayofanya matangazo ya misiba jijini hapa baada ya kuchukua miili ya watu waliofariki dunia hospitalini, akisema yamekuwa yakileta hataruki kwa wananchi na kujenga hofu.

Chuachua amesema hayo leo Jumanne Agosti 10, 2021 huku akiiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama kufanya doria na kuwachukulia hatua wamiliki wa magari hayo watakaobainika.

"Kumekuwa na tabia ya familia za watu wanaopoteza maisha kukodi magari ya matangazo na kuanza kutangaza maeneo mbalimbali ya jiji na kutaja majina ya wapendwa wao, sasa kwa niaba ya mkuu wa mkoa nimepiga marufuku rasmi leo Agosti 10 2021,"amesema Dk Chuachua.

"Ikumbukwe agizo hilo la kupiga marufuku hata aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila alikataza lakini sasa suala hilo limeibuka kwa kasi ya ajabu na kila baada ya dakika kadhaa unasikia tangazo la msiba, hivyo kusababisha shughuli za kiuchumi kusimama kwa muda."

Dk Chuachua amesema agizo hilo lianze mara moja na ndugu wanaofikwa na msiba, wawasiliane kifamilia kufanya taratibu za mazishi na kuhusu suala la matangazo kutoka hospitali mpaka kwenye maziko marufuku.

Amesema hata mikusanyiko ya watu haitaruhusiwa kwa kipindi hiki cha Covid -19 awamu ya tatu.

Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya ,Dourmohamed Issa amesema uamuzi wa mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ni sahihi kwa kuwa kumekuwa na taharuki kubwa kwa jamiii pindi magari ya matangazo na inayobeba miili ya waliopoteza maisha ikipita barabara kuu.

"Hata mimi nimewahi kupata mshtuko nikiwa naendesha gari nilikutana na magari manne yakitangaza na manne yakiwa yamebeba miili ya watu waliopoteaa maisha kimsingi ni hali inayotisha sana kwa Watanzania na hata wagonjwa wanaokuwa wamelazwa kwenye hospitali zetu,” amesema Issa.

Mkazi wa Mbeya, Rehema Mwanjonde amesema uamuzi huo wa Serikali ni sahihi kwa kuwa hata matangazo hayo yamekuwa yakiwarejeshea kumbumbuki watu waliowahi kupoteza ndugu zao.

Source: Mwananchi
 
Mbeya ni nchi Rais wao ni Sugu.

Muache wawaage wapendwa wao kwa style wanayotaka.

Kule Ghana watu huwaaga wapendwa wao kwa kucheza na jeneza hadi kaburini.
 
Siku ya kwanza nilidhani ni msiba wa kiongoz wa nchi. Kumbe ni utaratibu wao watu wa Mbeya. Mtu hata kama aliumwa na alikosa hela ya dawa siku ya msiba lazima kuwe na bajet ya gari la mziki pamoja na MC. Mbeya ni jiji ila lina mambo ya kienyeji sana
 
Kwani hapa Tanzania amna tamaduni ya makabila na miji mbalimbali? kwani lazima miji yetu zifanane tamaduni kote?

Sasa wanataka watu wanaotoka mikoa mengine wasangae nini wakifika mbeya?

Mwisho wa siku watawakataza watu kulia misibani.
 
mbeya ndio mfumo

kunakua na msafara wa maiti na magari kibao kutoka mochwari hadi mahali pa maziko

zinapigwa nyimbo kwa sauti ya juu za maomblezo huku gari zikipita kwa madaha,wafiwa wamevaa sare na wamepanda kwenye magari yao kwa raha zao

anakodiwa mc dany fm kutangaza njiani humo wasifu wa marehemu na ni kiasi gani dunia imepata pigo kwa kuondokewa na mtu muhimu

hapo mkizika mziki unahamia nyumbani na unapigwa hapo si chini ya siku tatu tukila ubwabwa,kande na maharagwe kwa kadri tulivyojaaliwa kukusanya na baada ya hapo tunaachia wanandugu kuendelea na msiba wao

sisi tunahamia kwenye msiba mwingine and the cycle goes on...

mixer sahivi mavuno ya bwana ni mengi so inasave budget pia..ni kuandaa tu 400 zako za daladala,we unahama tu misiba..shaa shaaa shaaaaaaa

waleeee twarukaa...priiiiiiiii
 
Mbeya. Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk Rashid Chuachua amepiga marufuku magari yanayofanya matangazo ya misiba jijini hapa baada ya kuchukua miili ya watu waliofariki dunia hospitalini, akisema yamekuwa yakileta hataruki kwa wananchi na kujenga hofu.

Chuachua amesema hayo leo Jumanne Agosti 10, 2021 huku akiiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama kufanya doria na kuwachukulia hatua wamiliki wa magari hayo watakaobainika.

"Kumekuwa na tabia ya familia za watu wanaopoteza maisha kukodi magari ya matangazo na kuanza kutangaza maeneo mbalimbali ya jiji na kutaja majina ya wapendwa wao, sasa kwa niaba ya mkuu wa mkoa nimepiga marufuku rasmi leo Agosti 10 2021,"amesema Dk Chuachua.

"Ikumbukwe agizo hilo la kupiga marufuku hata aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila alikataza lakini sasa suala hilo limeibuka kwa kasi ya ajabu na kila baada ya dakika kadhaa unasikia tangazo la msiba, hivyo kusababisha shughuli za kiuchumi kusimama kwa muda."

Dk Chuachua amesema agizo hilo lianze mara moja na ndugu wanaofikwa na msiba, wawasiliane kifamilia kufanya taratibu za mazishi na kuhusu suala la matangazo kutoka hospitali mpaka kwenye maziko marufuku.

Amesema hata mikusanyiko ya watu haitaruhusiwa kwa kipindi hiki cha Covid -19 awamu ya tatu.

Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya ,Dourmohamed Issa amesema uamuzi wa mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ni sahihi kwa kuwa kumekuwa na taharuki kubwa kwa jamiii pindi magari ya matangazo na inayobeba miili ya waliopoteza maisha ikipita barabara kuu.

"Hata mimi nimewahi kupata mshtuko nikiwa naendesha gari nilikutana na magari manne yakitangaza na manne yakiwa yamebeba miili ya watu waliopoteaa maisha kimsingi ni hali inayotisha sana kwa Watanzania na hata wagonjwa wanaokuwa wamelazwa kwenye hospitali zetu,” amesema Issa.

Mkazi wa Mbeya, Rehema Mwanjonde amesema uamuzi huo wa Serikali ni sahihi kwa kuwa hata matangazo hayo yamekuwa yakiwarejeshea kumbumbuki watu waliowahi kupoteza ndugu zao.

Source: Mwananchi

Kushughulika kupunguza vifo visivyo vya lazima inawezekana:

IMG_20210718_063455_991.jpg


Shughuli za kiuchumi?!

Shughulikieni tatizo la watu kufa.
 
Back
Top Bottom