Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu zangu wanaJF,
Nimehabarishwa na rafiki yangu mmoja anayeishi Mbezi ya Kimara kwamba wananchi wanahaha kutafuta maji baada ya DAWASCO kuamua kukata huduma ya maji kwa wafanyabiashara wanaouza maji kwenye magari (water bowsers). Maeneo yote yaliyokuwa yanatumika kujaza maji kwenye bowsers sasa yamefungwa. Wananchi wengi wanaotegemea huduma hiyo ya magari, sasa wanateseka sana kwani chanzo chao cha maji kimesitishwa. Inawezekana DAWASCO wana malengo yao likiwemo la kuwakomoa wafanyabiashara wa maji lakini wafahamu kuwa wanaoteseka siyo wafanyabiashara bali ni wananchi wanaotegemea huduma hiyo. Hivi sasa wananchi wengi wa maeneo ya Mbezi Mwisho wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji. Lita 1,000 kwa sasa inauzwa Sh. 20,000 mpaka 25,000. Ni mwananchi gani wa hali ya kawaida anayeweza kumudu bei hiyo!! Ndiyo maana wananchi wengi wanateseka sana.
Najua Mhe. Mnyika ni mwanachama wa JF. Tafadhali sana wasaidie wapiga kura wako kuondokana na adha hiyo kubwa inayowapata wapiga kura wako. Kama kuna wakati mwanachi wa kawaida anamhitaji kiongozi wake, basi huu ndiyo wakati wenyewe. Tafadhali Mhe. Mnyika jaribu kufuatilia kwa ukaribu sana suala hili.
Nimehabarishwa na rafiki yangu mmoja anayeishi Mbezi ya Kimara kwamba wananchi wanahaha kutafuta maji baada ya DAWASCO kuamua kukata huduma ya maji kwa wafanyabiashara wanaouza maji kwenye magari (water bowsers). Maeneo yote yaliyokuwa yanatumika kujaza maji kwenye bowsers sasa yamefungwa. Wananchi wengi wanaotegemea huduma hiyo ya magari, sasa wanateseka sana kwani chanzo chao cha maji kimesitishwa. Inawezekana DAWASCO wana malengo yao likiwemo la kuwakomoa wafanyabiashara wa maji lakini wafahamu kuwa wanaoteseka siyo wafanyabiashara bali ni wananchi wanaotegemea huduma hiyo. Hivi sasa wananchi wengi wa maeneo ya Mbezi Mwisho wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji. Lita 1,000 kwa sasa inauzwa Sh. 20,000 mpaka 25,000. Ni mwananchi gani wa hali ya kawaida anayeweza kumudu bei hiyo!! Ndiyo maana wananchi wengi wanateseka sana.
Najua Mhe. Mnyika ni mwanachama wa JF. Tafadhali sana wasaidie wapiga kura wako kuondokana na adha hiyo kubwa inayowapata wapiga kura wako. Kama kuna wakati mwanachi wa kawaida anamhitaji kiongozi wake, basi huu ndiyo wakati wenyewe. Tafadhali Mhe. Mnyika jaribu kufuatilia kwa ukaribu sana suala hili.