Kajole
JF-Expert Member
- Apr 12, 2011
- 1,667
- 1,642
Habari?,rejea thread yangu yenye kichwa: JAMANI MAPENZI YATANIMALIZA NISAIDIENI PLS (nimeshndwa kuicopy hapa kwa kuwa natumia simu hvyo yeyote anaweza kunisaidia). Jaman nimembembeleza,nimeomba na kujishusha sana asiniache kwa kuwa nampenda sana lakini imeshindikana na jana kanitumia msg NISAMEHE KWA YOTE WANGU ILA BORA KILA MMOJA AWE UPANDE WAKE nilipomuuliza kwanin?,akajibu,SINA FURAHA KTK RELATION YETU NA NINAOGOPA FURAHA ISIPORUDI NTAKUWA NIMEPOTEZA MUDA WAKO. Kiukweli nimeumia sana,nmeshndwa kula toka jana asbh na sijalala usiku kucha,kiufupi nateseka sana mpaka nimefikiria kujidhuru..nikaona hapana bora nijaribu kwa hawa WAGANGA wa kienyeji pengine watanisaidia kurudisha penzi langu. Jamani hivi kweli dawa hizi zinafaa?,nisaidieni nifanye nini nateketea mwenzenu.