Dawa ya kuua mchwa wanaojenga ndani ukutani

Dawa ya kuua mchwa wanaojenga ndani ukutani

Extrovert

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2016
Posts
72,173
Reaction score
190,754
Wadau niko mkoa kwa likizo fupi ya mafuriko ya mjini Daslam mpaka hali itapotengemaa. Huku mkoa niliko mjengoni kuna tabia ya ajabu ya mchwa wanaojenga na udongo ukutani kama ramani flani hivi ya udongo.

Nimejaribu kuwavunjia mara kadhaa ila nao wameonesha jinsi walivyo na kiburi na kujenga upya kila napobomoa tu nikilala nikiamka nakuta kama nilivyopaacha. Cha ajabu milango na madirisha yamefungwa usiku kucha sijui hata udongo wanautolea wapi.

Mwenye dawa ya kuwafukuza hawa jamaa au utundu wa kuondosha hii hali maana imekuwa kama kero kwangu. Naombeni mjitokeze.

DSC_0002.JPG
 
Mwaga mafuta taa eneo lote hilo hadi kwenye tundu wanapotokea hawatarudi tena
 
Wadau niko mkoa kwa likizo fupi ya mafuriko ya mjini Daslam mpaka hali itapotengemaa. Huku mkoa niliko mjengoni kuna tabia ya ajabu ya mchwa wanaojenga na udongo ukutani kama ramani flani hivi ya udongo.

Nimejaribu kuwavunjia mara kadhaa ila nao wameonesha jinsi walivyo na kiburi na kujenga upya kila napobomoa tu nikilala nikiamka nakuta kama nilivyopaacha. Cha ajabu milango na madirisha yamefungwa usiku kucha sijui hata udongo wanautolea wapi.

Mwenye dawa ya kuwafukuza hawa jamaa au utundu wa kuondosha hii hali maana imekuwa kama kero kwangu. Naombeni mjitokeze.
View attachment 1102007
Same here hawa nyoko, kuna sehemu wamejenga mpaka kwenye pazia.
20200613_152008.jpg
 
Kuna aina tofauti za kuua mchwa.
1. Kabla ya kujenga unatakiwa kumwaga dawa ktk eneo la ujenzi inakaa kwa mda halafu ndo unajenga.kwa kufanya hivyo hakuna mdudu atakanyaga hilo eneo na kuleta uharibifu.
2. Tafuta wataalamu . wanaenda kutafuta makazi/kichuguu chao na kumtoa malkia wa mchwa . wanachimba ,wanaweka dawa/kidonge halafu wanafukia ili dawa isambae ndani ya shimo lao.hapo mchwa wote wanakufa. Tofauti na hapo mchwa watakusumbua sana.
 
Tatizo ni umasikini , Ndio maana mambo mengine ya nakuwa hivyo , watu atufuati utaratibu wakujenga nyumba , nyumba lazima chini imalishwe na zege kali , sio unapaka paka tu sementi ,
Usiseme hivyo mi nimeweka zege ya hatari lkn mchwa kibao, mpk na dawa nilikorogea zege lkn hakuna kitu.
 
Same here hawa nyoko, kuna sehemu wamejenga mpaka kwenye pazia.View attachment 1477299
Ukiona hivyo elewa ujenzi wa nyumba hiyo ni wa kimagumashi!

Unaitwa ujenzi wa kuonja, bonge la bangaloo, lakini material iliyotumika kujenga ni tofari za kuchoma na mota ya tope!

Ukichezea madongo kwenye ujenzi lazima mchwa wakutembelee hata kama ripu ni ya saruji na umeweka dawa!

Kuhusu mantiki ya mtoa mada, nadhani imejibiwa hapo juu.
 
Pia unaweza tumia CONFIDOL ipo kwenye maduka ya mifugo.
 
hiyo nyumba ilijengwa chini ya kiwango
 
Back
Top Bottom