kibaravumba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 6,635
- 7,005
Bila shaka wengi watakuwa wanajiuliza maswali mengi bila majibu kuwa ni kwa nini pamoja na utajiri mkubwa wa rasilimali katika nchi yetu, bado kuna idadi kubwa ya watu wanaishi maisha ya umaskini mkubwa.
Tatizo ni Elimu duni.
Mfumo huu wa elimu inayotolewa nchini, imeshindwa kuamsha ari ya ubunifu kutoka kwa wasomi wetu ili kuweza kujibu maswali ya changamoto zilizopo.
Nini kifanyike?
Kukaa na kufanya tathmini upya kuhusu mfumo huu wa sasa iwapo una tija au la!
Ni nani aliyefanya utafiti kuwa mtoto umuweke shule ya msingi kwa muda wa miaka saba huku ukimfundisha mambo ambayo hata akimaliza, ni chini ya asilimia kumi tu atakuwa anayakumbuka. Wakati mtoto huyo huyo, ukimfundisha ufundi wowote, kwa muda huo,atakuwa na uwezo mkubwa sana na kuwa mwenye ubunifu wa hali ya juu.
Au ni nani alisema mtu asome O level miaka minne halafu aende A level miaka miwili?
Nani alifanya utafiti juu ya elimu zinazotolewa katika vyuo vyetu kama kweli zina toa wahitimu wenye tija?
Leo hata ukiongea na wasomi wengi hasa wanaosoma masomo ya sayansi, watakwambia wanasoma mambo mengi sana magumu yasiyo na tija kwenye taaluma zao. Masomo hayo yapo kuleta ugumu wa kupata tu vyeti ili isije kuonekana kuwa elimu ni rahisi.Lakini kiukweli, hayawasaidii kabisa katika utendaji wao wa kazi.
Kama tusipoamua kufanya maamuzi magumu na makini,tukaendelea kuthamini vyeti badala ya matokeo ya elimu, tukaachana na mifumo ya kizamani ya elimu, itakuwa ni ndoto kwa nchi yetu kuagana na umaskini.
Tatizo ni Elimu duni.
Mfumo huu wa elimu inayotolewa nchini, imeshindwa kuamsha ari ya ubunifu kutoka kwa wasomi wetu ili kuweza kujibu maswali ya changamoto zilizopo.
Nini kifanyike?
Kukaa na kufanya tathmini upya kuhusu mfumo huu wa sasa iwapo una tija au la!
Ni nani aliyefanya utafiti kuwa mtoto umuweke shule ya msingi kwa muda wa miaka saba huku ukimfundisha mambo ambayo hata akimaliza, ni chini ya asilimia kumi tu atakuwa anayakumbuka. Wakati mtoto huyo huyo, ukimfundisha ufundi wowote, kwa muda huo,atakuwa na uwezo mkubwa sana na kuwa mwenye ubunifu wa hali ya juu.
Au ni nani alisema mtu asome O level miaka minne halafu aende A level miaka miwili?
Nani alifanya utafiti juu ya elimu zinazotolewa katika vyuo vyetu kama kweli zina toa wahitimu wenye tija?
Leo hata ukiongea na wasomi wengi hasa wanaosoma masomo ya sayansi, watakwambia wanasoma mambo mengi sana magumu yasiyo na tija kwenye taaluma zao. Masomo hayo yapo kuleta ugumu wa kupata tu vyeti ili isije kuonekana kuwa elimu ni rahisi.Lakini kiukweli, hayawasaidii kabisa katika utendaji wao wa kazi.
Kama tusipoamua kufanya maamuzi magumu na makini,tukaendelea kuthamini vyeti badala ya matokeo ya elimu, tukaachana na mifumo ya kizamani ya elimu, itakuwa ni ndoto kwa nchi yetu kuagana na umaskini.