Wakuu imezoeleka kwamba mtu unapoamka asubuhi na hang_over au mning`inio kwa kibantu basi watu wengi hukimbilia supu ya nyama makongoro au miguu ya wanyama walao nyasi.
Kiuhalisia supu ya nyama peke yake haitoi mning`io. Unachotakiwa ni KUTAFUNA NDIZI na kumeza mchuzi wake kwa takribani dakika 30 hadi 40 na hapo hang~over lazima ikuache.
NB. Usisahau ni ndizi moja au mbili tu zinatosha. Kutegemea na upatikanaji wa ndizi eneo ulilopo.
Kwanza hang over hutofautiana kati ya kichwa na kichwa na pia umekunywa kiasi gani. Nimenusurika mara kadhaa kwa kupiga vyombo kupitiliza. Nilipata mning'inio kwa siku2, nilijaribu supu, ndizi lakini wapi. Nilikunywa bitelemon tu na mtindi.