Hivi punde
JF-Expert Member
- Apr 1, 2017
- 2,554
- 8,552
Naamu wale members wenzangu wa stuli ndefu, maji ya mende na kauli mbiu yetu ya 'Drink beer to save water'..
Moja kwa moja kwenye mada.
Mojawapo na kitu kinachokera zaidi baada ya kunywa pombe (kupita kiasi) ni kuamka na hang-over, hali ya kuumwa-umwa, hali ambayo unajisikia kichefuchefu, kukosa hamu ya kula, kunywa wala kukosa hali nzuri ya kufanya kazi na pengine kujiskia kama unataka kutapika 'nyongo'.
Kipindi hiki mtu unakuwa mchovu-mchovu licha ya kwamba jana yake umeenjoy pombe na marafiki, ndugu nk kwenye vijiwe au sherehe.
KWANINI HANG-OVER?
Ukishakuwa unakunywa pombe, ukavusha/kutoboa muda wa saa sita usiku, uwezekanao wa kupata hangover ni mkubwa sana!Lewa-ulewavyo lakini make sure unamaliza mambo yako kabla ya saa sita usiku, nikimaanisha ukalale muda huo. Na ukiona unakunywa pombe halafu ghafla unaanza kujisikia 'kucheua, kutapika'kushiba sana' ujue tayari level yako ya kunywa imefikia kikomo, kinachofuata baada ya hapo ni kuamka na 'hang-over' kesho yake.
Kisababishi kingine cha hangover ni kunywa pombe kwa pupa (haraka haraka) na kuchanganya vilevi, mfano mtu anakunywa bia baadae anahamia kwenye konyagi. Au mtu anachanganya vilevi tofauti kwenye glass moja. Hapo unachanganya madawa ndugu yangu, lazima yalete shida
JINSI YA KUTATUA/KUEPUKA HANG-OVER
1. Kunywa pombe kiasi. Maana ake epuka hali ya kuanza kujisikia kucheua,kutapika, kushiba sana, kizunguzungu. Muda huo acha kabisa kunywa. Nenda kalale
2. Kunywa maji mengi wastani wa lita 2 mpaka 3 ya baridi baada ya kunywa pombe unapotaka kulala
3. Kula vizuri wakati unakunywa pombe au baada ya kunywa pombe. Namaanisha kitu kama Kitimoto rost safi nusu au kilo 1 na ugali wa kushiba, nyama choma na ugali au ndizi, mchemsho wa kuku, mbuzi, ng'ombe, mkia au kongoro safi sana yenye pilipili za kutosha na makachumbari, mchemsho wa kuku
4. Ukiamka asubuhi unajisikia hang-over kichwani, PLEASE USIJILAZIMISHE KUAMKA hata kama huna usingizi, endelea kupumzika kitandani hata kama huna macho, hata una simu yako unaweza ukawa unachatichati tu wakati wife au mdada wa kazi anakutengenezea mchemsho wa kuku. Endelea kulala kwa muda labda wa saa 1 au 2 baada ya kuamka. Yaani nyongo haitakusumbua
ANGALIZO:
Ukishaona umekunywa pombe(kupita kiasi) usiendeshe chombo cha moto, ni kwa usalama wa maisha yako.
" Beer comes from Water, Drink beer to save Water"
Moja kwa moja kwenye mada.
Mojawapo na kitu kinachokera zaidi baada ya kunywa pombe (kupita kiasi) ni kuamka na hang-over, hali ya kuumwa-umwa, hali ambayo unajisikia kichefuchefu, kukosa hamu ya kula, kunywa wala kukosa hali nzuri ya kufanya kazi na pengine kujiskia kama unataka kutapika 'nyongo'.
Kipindi hiki mtu unakuwa mchovu-mchovu licha ya kwamba jana yake umeenjoy pombe na marafiki, ndugu nk kwenye vijiwe au sherehe.
KWANINI HANG-OVER?
Ukishakuwa unakunywa pombe, ukavusha/kutoboa muda wa saa sita usiku, uwezekanao wa kupata hangover ni mkubwa sana!Lewa-ulewavyo lakini make sure unamaliza mambo yako kabla ya saa sita usiku, nikimaanisha ukalale muda huo. Na ukiona unakunywa pombe halafu ghafla unaanza kujisikia 'kucheua, kutapika'kushiba sana' ujue tayari level yako ya kunywa imefikia kikomo, kinachofuata baada ya hapo ni kuamka na 'hang-over' kesho yake.
Kisababishi kingine cha hangover ni kunywa pombe kwa pupa (haraka haraka) na kuchanganya vilevi, mfano mtu anakunywa bia baadae anahamia kwenye konyagi. Au mtu anachanganya vilevi tofauti kwenye glass moja. Hapo unachanganya madawa ndugu yangu, lazima yalete shida
JINSI YA KUTATUA/KUEPUKA HANG-OVER
1. Kunywa pombe kiasi. Maana ake epuka hali ya kuanza kujisikia kucheua,kutapika, kushiba sana, kizunguzungu. Muda huo acha kabisa kunywa. Nenda kalale
2. Kunywa maji mengi wastani wa lita 2 mpaka 3 ya baridi baada ya kunywa pombe unapotaka kulala
3. Kula vizuri wakati unakunywa pombe au baada ya kunywa pombe. Namaanisha kitu kama Kitimoto rost safi nusu au kilo 1 na ugali wa kushiba, nyama choma na ugali au ndizi, mchemsho wa kuku, mbuzi, ng'ombe, mkia au kongoro safi sana yenye pilipili za kutosha na makachumbari, mchemsho wa kuku
4. Ukiamka asubuhi unajisikia hang-over kichwani, PLEASE USIJILAZIMISHE KUAMKA hata kama huna usingizi, endelea kupumzika kitandani hata kama huna macho, hata una simu yako unaweza ukawa unachatichati tu wakati wife au mdada wa kazi anakutengenezea mchemsho wa kuku. Endelea kulala kwa muda labda wa saa 1 au 2 baada ya kuamka. Yaani nyongo haitakusumbua
ANGALIZO:
Ukishaona umekunywa pombe(kupita kiasi) usiendeshe chombo cha moto, ni kwa usalama wa maisha yako.
" Beer comes from Water, Drink beer to save Water"