Raynavero
JF-Expert Member
- Apr 29, 2014
- 38,380
- 56,078
Habarini za weekend.
Leo naongelea wale wanaopenda kukopa kurudisha kwao mtihani!
Yaani mtu anakuja anapokua na shida, kwa unyenyekevu kama yuko ibadani anaomba umsaidie kiasi cha pesa na wewe tena ubinadamu kama mother Theresa unampa
kiroho safi ili asiumbuke mjini!
Siku zinaenda,mwezi,Mara miezi miwili hakumbushii wala kusema chochote,unaamua kujitoa mhanga unamuulizia vipi ile ishu sasa!
mambo magumu Ila njoo tarehe Fulani nikupe chako,ukienda humkuti,simu hapokei meseji hajibu!
Anakutumia meseji za kashfa ukimuulizia kuhusu pesa zako doohh!
Ulivyokua na shida ulikua mpole kama maji baridi!
Loohh!pesa yenyewe nyingii jamani!
Binadamu tujifunze uungwana tukumbuke shida sio siku moja kuna Leo na kesho unaazima cha Mtu kumbuka kurudisha kwa wakati au hata ukichelewesha basi uwe na lugha nzuri ili kesho ukopesheke!
Uungwana ni vitendo!!
Leo naongelea wale wanaopenda kukopa kurudisha kwao mtihani!
Yaani mtu anakuja anapokua na shida, kwa unyenyekevu kama yuko ibadani anaomba umsaidie kiasi cha pesa na wewe tena ubinadamu kama mother Theresa unampa
kiroho safi ili asiumbuke mjini!
Siku zinaenda,mwezi,Mara miezi miwili hakumbushii wala kusema chochote,unaamua kujitoa mhanga unamuulizia vipi ile ishu sasa!
mambo magumu Ila njoo tarehe Fulani nikupe chako,ukienda humkuti,simu hapokei meseji hajibu!
Anakutumia meseji za kashfa ukimuulizia kuhusu pesa zako doohh!
Ulivyokua na shida ulikua mpole kama maji baridi!
Loohh!pesa yenyewe nyingii jamani!
Binadamu tujifunze uungwana tukumbuke shida sio siku moja kuna Leo na kesho unaazima cha Mtu kumbuka kurudisha kwa wakati au hata ukichelewesha basi uwe na lugha nzuri ili kesho ukopesheke!
Uungwana ni vitendo!!