Dawa ipi ya Meno(Mswaki) ni bora?

Dawa ipi ya Meno(Mswaki) ni bora?

GAZETI

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
5,292
Reaction score
6,772
Wakuu, naomba kujua ni dawa ipi nzuri na ina kinga za kutosha kwa meno? Nilikuwa sina tabia ya kuangalia lebo lakini sasa inanibidi kwani kuna dawa nilitumia meno yakawa na ganzi.
 
Sensodyne ni bora zaidi, itakusaidia hata kama meno yako huwezi kula vitu vichachu/barafu/sukari nyingi hii itakusaidia utaweza bila shida. For me hii ni bora zaidi kuliko aina nyingine zote
 
FOREVER BRIGHT TOOTH GEL

Bidhaa ya kusafisha meno iliyotengenezwa kutokana na stabilized Aloe Vera Gel pamoja na bee propolis hivyo huua bacteria na vijidudu vyote. Inang’arisha meno bila kuchuna tabaka la juu la meno-ENAMEL. Huzuia meno yasitoe damu, kuponya vidonda vya mdomoni na endapo kuna maumivu mdomoni unaweza kupaka kwenye meno moja kwa moja bila kupiga mswaki.
Husaidia kusafisha fizi na kuzifanya tishu zake ziwe na afya imara.

FAIDA: Huzuia kutokwa damu, harufu mbaya, kuimarisha fizi, matundu kwenye meno,huponya vidonda vya mdomoni.
 

Attachments

Wakuu, naomba kujua ni dawa ipi nzuri na ina kinga za
kutosha kwa meno? Nilikuwa sina tabia ya kuangalia lebo
lakini sasa inanibidi kwani kuna dawa nilitumia meno yakawa na
ganzi.
Pole ndugu -kusema kweli hakuna cha colgate wala sensodyne na ndugu zake.Ngoja tuelimishane kidogo- kufa ganzi kwa meno ni dalili za

1.matatizo ya fizi

2.Hatua za awali za kutoboka kwa meno

3.Kurika kwa Meno(Attrition)

MATATIZO YA FIZI
Yawezekana kati ya meno na fizi kuna mgando mweusi au njano bila shaka umefanya jitihada za kuutoa bila mafanikio au kinywa kina harufu mbaya au kila usafishapo meno kwa mswaki damu zinatoka katika fizi-dalili hizi na hali hii inasababishwa na bacteria ambao hawatolewi vema mara zote usafishapo menoi.Hali hii inapoachwa bila matibabu kwa muda mrefu sumu za bacteria huaribu umahiri wa fizi na kuacha sehemu ya meno inayofunikwa na fizi wazi hivyo kusababisha meno kufa ganzi au kusisimuka mara baridi iingiapo kinywani.

2.Hatua za awali za kutoboka kwa Meno
Jino kuuma lina hatua zake-hatua za mwanzo kabisa ni ganzi pindi unapokunywa/kula vitu baridi chachu au moto.hatua ya pili ni mchanganyiko maumivu/ganzi ulapo/unywapo vitu baridi,chachu au moto.Hali hii inasababishwa na tindikali itolewayo na bacteria wanapotumia mabaki ya sukari(carbohydrates).

3.Meno kurika(attrition)
Meno yana sehemu ya nje kama kioo inaitwa Enamel Inayofuata inatwa Dentin kisha Pulp ambapo kuna mishipa ya fahamu na damu-mabadiliko ya unene wa sehemu ya nje (enamel)husababisha sehemu ya pili Dentin kuwa wazi hali isiyotakiwa kwan kuna mawasiliano kati ya Pulp na Dentin.Hali yaweza sababishwa na;

1.Kutafuna meno wakati tume sinzia-Hali hii husababishwa na Msongo wa mawazo,Kung'oa meno au ajari iliyosababisha kubadilika kwa milinganyo ya taya.

2.Kuugua au ujauzito unaosababisha kutapika kupita kiasi(tumboni kuna tindikali).

3.kupiga mswaki kwa nguvu as if unaondoa Super glue ktk meno!

Dawa gani utumie.
1.NI VIZURI KUMWONA DAKTARI WA KINYWA NA MENO.

2.FUNDISHO -Unaposikia ganzi/maumivu katika meno maana yake uwiano wa Kutoka kwa madini katika jino(Demineralization)Kurudi kwa madin katika jino(Remineralization) haupo.Dawa pekee ya kurekebisha hali hiyo ni FLOURDE.Utaihisi kama pipi kifua vile ila FLOURIDE ni sumu kiwango salama ni 500-1500 parts per million(ppM).

UNUNUAPO DAWA YA MENO SOMA INGRIDIENTS ktk box mara nyingi maandishi madogo sijui kwa nini-Pamoja na ingredients nyingi utaona katika mabano 500ppM au 1000ppM au 1450ppM-Dawa kwa watoto isizidi 500ppM.

Dawa pia zina sub-brand Hasa utaona zimeandkwa WHITENING au SENSITIVE kuwa makini na BLAHBLAH WHITENING ni kama zina dawa ya kuondoa madoa au zina msasa ndani yake Sasa fikiria meno yakisagana yenyewe ni inshu Je ukisugua kwa msasa.SINSITIVE zipo vizuri maana zina FLOURDE yakutosha.

Ndugu yangu usiangalie Trade name angalia ingridients.
 
Wakuu, naomba kujua ni dawa ipi nzuri na ina kinga za
kutosha kwa meno? Nilikuwa sina tabia ya kuangalia lebo
lakini sasa inanibidi kwani kuna dawa nilitumia meno yakawa na
ganzi.

Tumia Arovela vichwa 2 ipo poa sana, mimi natumia tangu 2010 haisumbui na meno yanakuwa imara tofauti na hizo nyingine kama whitedent na colgate.
 
Si wanasema colgate ndo chaguo na pendekezo namba moja la madaktari ulimwenguni? Au?
 
tumia Aloe vera ni nzuri sana japo inauzwa ghali kidogo ambapo huuzwa kati ya TSHS.13,000/= - 15,000/=
 
Kwanza nenda kwa daktari wa ukweli wa meno kwa uchunguzi wa kina, pia muulize ni dawa gani the best.

Mimi tangu nianze kutumia sensodyne sijaweza kutumia tena dawa nyingine tofauti, nikitumia naona kama nimeweka mlenda mdomoni nasikia utelezi kinoma.
Nadhani sensodyne ina addiction, bado naendelea kuchunguza.
 
Ili dawa ya meno yenye Flouride ikusaidie fanya hivi kwanza ni vizuri kusafisha meno angalau mara mbili kwa siku asubuhi na usiku kabla ya kulala-safisha meno kwa dawa kisha chukutua na tema yote rudia mara ya pili lakin mara hii kuwa kama unapakaa dawa katika meno-usisukutue tema dawa iliyozidi -baada ya muda hutoisikia dawa mdomoni.
 
SENSODYNE ndo kila kitu,ata mie nilipatwa na ganzi nikatumia alovera toothgel,colgate hazikusaidia
now niko bomba usiseme sina tatizo la ganzi wala fizi
 
Kuna dentist mmoja aliulizwa hilo swali jana na Star TV akasema yeye anashauri watu watumie dawa zilizozoeleka kwa miaka mingi kwani zimethibitishwa kimataifa na kitaifa waachane na za kichina na sijuhi nini.

Point alosema ni kuwa kuna baadhi ya dawa hazina chloride; afu watu wanazitangaza na sie tunaingia king. Bila chloride meno lazima yaoze.

Mimi nawashangaa sana wabongo wenzangu kupenda kutumiwa kama taster...ukisikia sijuhi brand gani iko sokoni...basi huyoooo unawahi kununua...mnaweka afya zenu rehani.
 
Back
Top Bottom