Na wewe umemalizia kabisa, Duhhh.Nimefurahishwa mno na hotuba ya Kafulila. Kama ningekuwa naandika kichwa cha habari cha gazeti saa hizi, kichwa cha habari hiyo kingekuwa "KAFULILA AMFUNIKA JK". Kaongea maneno ya kujenga kuliko maneno ya JK ya kutishia watu kuwa eti serikali tatu zitapinduliwa na jeshi!
Yaani, Yaani, Yaani Nondo tupu. Kijana mtanganyika huyu. Mungu ambariki.hakika amejenga hoja, labda tu kwa wale ambao hawakupata nafasi ya kufuatilia niwape baadhi ya hoja alizojenga
1: kama kuna watu (ccm) ambao wanadai maoni ya watu 17000 juu ya kuwa na serikali 3 ni idadi ndogo sana ambayoyo haiakisi matakwa ya watanzania 46ml, je hawa wabunge 600 wanapata wapi nguvu ya kuwa na uwakilishi wa wananchi ili hali wao ni wachache zaidi kuliko hata hao waliotoa maoni juu ya kuwa na serikali 3?
2: Amehoji kama ishu ni kumtii mwl nyere ambae hakuta kuvunjika kwa muungano,wamesahau kuwa mwl alikuwa anabadilika kulingana na wakati. Mf mwaka 1965 mwl alifuta vyama vingivlakini kulingana na mabadiliko yaliyohitaji mageuzi mwaka 1992 ni mwl uyohuyo aliweze kuwa na vyama vingi ambavyo alivifuta hapo mwanzo. Akauliza je mwl angekufa kabla ya kuanzishwa vyama vingi inamaana mpaka sasa kungekuwa na chama kimoja tu?
3: Viongozi waliopo madarakani leo wafanikishe kuwa na muungano mzuri zaidi wa serikali 3 kwakuwa hii nafasi walionayo hawatakuwa nayo tena miaka ijayo kwani ni dhahir wingi wao (ccm) utapungua hivyo watalazimika kukubali mabadiliko kwa shinikizo kubwa kitu ambacho kitazalisha muundo mbovu zaidi . Hili alitoa kama ushauri kwa viongozi waliopo madarakani kutumia hii nafasi kufanya mabadiliko mazuri tena kwa busara kuliko kusubiri presha hapo baadae.
Nimevutiwa na jinsi Mbuge Huyu alivyo weza kujieleza na kutetea Serikali Tatu kwenye Bunge Maaluma La Katiba,ameeleza kwa ufasaha na nguvu za hoja kiasi kwa waliosikiliza/kuangalia live.
Ametetea Serikali Tatu na Kumpongeza Jaji Mstaafu Joseph Warioba kwa kazi aliyoifanya na Tume yake,na kuwabeza wanaoipinga Tume ya Warioba.
Amewaumbua wanafiki kweli kweli na hoja zao nyepesi
The guy is very concistence and smart.nimempenda sana.
The guy is very concistence and smart.nimempenda sana.
Ndio walichobakiza tena wapinzani hawana lengine, kelele za serikali tatu tu kwa sasa.Nimevutiwa na jinsi Mbuge Huyu alivyo weza kujieleza na kutetea Serikali Tatu kwenye Bunge Maaluma La Katiba,ameeleza kwa ufasaha na nguvu za hoja kiasi kwa waliosikiliza/kuangalia live.
Ametetea Serikali Tatu na Kumpongeza Jaji Mstaafu Joseph Warioba kwa kazi aliyoifanya na Tume yake,na kuwabeza wanaoipinga Tume ya Warioba.
Tunaomba pls aliyerekodi hata kama ni audio atuwekee hapa ili nasi tuliokuwa mashambani na migodini nyakati hizo tuweze kusikia alichokisema mpendwa wetu David Kafulila!