beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
David Beckham amepigwa marufuku kuendesha gari kwa miezi sita baada ya kupatikana akitumia simu wakati akiendesha gari.
Kapteni huyo wa zamani wa England amekiri makosa.
Mahakama imearifiwa amepigwa picha na raia akiwa ameshikilia simu wakati akiendesha gari lake aina ya Bentley 'taratibu' katika foleni.
Beckham, mwenye umri 44, ametozwa faini ya £750, ameagizwa alipe £100 gharama ya kesi na malipo ya ziada ya £75 katika siku saba zijazo.
Jaji katika mahakama hiyo amemuambia hata kama kasi ya gari ilikuwa taratibu kwenye foleni 'hakuna kisingizio' chini ya sheria.
Mwendesha mashtaka amesema: "Badala ya kutazama mbele na kuangalia barabara alionekana akitazama mapajani mwake.'
Wakili wa Beckham Gerrard Tyrrell amesema mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United " haikumbuki siku hiyo au tukio hilo".
Aliongeza: "Hakuna utetezi wa kilichotokea, lakini mtazammo wake ni kwamba hakumbuki."
Tyrrell ameiambia mahakama kwamba Beckham hufurahia kuendesha gari.
"Huwapeleka watoto shuleni kila siku na mara nyingine hurudi kuwachukua anapoweza, na kuwanyima hilo ni jambo ambalo hana budi kulikubali," amesema
Ni kinyume cha sheria nchini Uingereza kushika simu wakai unaendesha gari. Mtu anaweza kuadhibiwa kwa kupunguziwa pointi kwenye leseni na kutozwa faini ya £200 - lakini kutokana na uzito wa makosa unaweza kufikishwa mahakamani na ukahukumiwa adhabu kali zaidi.
Kapteni huyo wa zamani wa England amekiri makosa.
Mahakama imearifiwa amepigwa picha na raia akiwa ameshikilia simu wakati akiendesha gari lake aina ya Bentley 'taratibu' katika foleni.
Beckham, mwenye umri 44, ametozwa faini ya £750, ameagizwa alipe £100 gharama ya kesi na malipo ya ziada ya £75 katika siku saba zijazo.
Jaji katika mahakama hiyo amemuambia hata kama kasi ya gari ilikuwa taratibu kwenye foleni 'hakuna kisingizio' chini ya sheria.
Mwendesha mashtaka amesema: "Badala ya kutazama mbele na kuangalia barabara alionekana akitazama mapajani mwake.'
Wakili wa Beckham Gerrard Tyrrell amesema mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United " haikumbuki siku hiyo au tukio hilo".
Aliongeza: "Hakuna utetezi wa kilichotokea, lakini mtazammo wake ni kwamba hakumbuki."
Tyrrell ameiambia mahakama kwamba Beckham hufurahia kuendesha gari.
"Huwapeleka watoto shuleni kila siku na mara nyingine hurudi kuwachukua anapoweza, na kuwanyima hilo ni jambo ambalo hana budi kulikubali," amesema
Ni kinyume cha sheria nchini Uingereza kushika simu wakai unaendesha gari. Mtu anaweza kuadhibiwa kwa kupunguziwa pointi kwenye leseni na kutozwa faini ya £200 - lakini kutokana na uzito wa makosa unaweza kufikishwa mahakamani na ukahukumiwa adhabu kali zaidi.