Darasa Huru: Ufundi Laptop (Beginners To Advanced)

Darasa Huru: Ufundi Laptop (Beginners To Advanced)

safi mkuu tupo pamoja pm namba yako kuna mtu anasumbua muda wa kumfundisha sina na talanta ya kufundisha km wewe sijajaliwa
hvyo nipe namba yako nitampasia na imani mkielewana atakulipa kwa namna mtakavyokubaliana
Hakuna Haja Ya Malipo Bro.
Nikipata Muda Nitamuelekeza Na Kumsaidia Baadhi Ya Mambo
Maisha Sio Pesa Tu.
 
Karibu Mkuu
Asante sana mkuu naamini utatusaidia but once nkifanikiwa mambo yangu we jamaa lazima nije kukupa zawadi maana umefumbua macho kwenye kompyuta i like to know software engineering hata bila kukaa darasan. Please help us
 
Asante sana mkuu naamini utatusaidia but once nkifanikiwa mambo yangu we jamaa lazima nije kukupa zawadi maana umefumbua macho kwenye kompyuta i like to know software engineering hata bila kukaa darasan. Please help us
Usijali Mkuu, Zawadi Yangu Wafundishe Wengine Wasio Na Ajira!
Naamin Tutafika
 
Asante sana mkuu naamini utatusaidia but once nkifanikiwa mambo yangu we jamaa lazima nije kukupa zawadi maana umefumbua macho kwenye kompyuta i like to know software engineering hata bila kukaa darasan. Please help us
Software Repair Ni Part Tu Ya Software Engineering, Unahitaji Kufahamu Vingi Mpaka Uitwe Software Engineer, Unatakiwa Kujua Coding Sana.
Utafika Weka Juhudi
 
TUIFAHAMU BIOS MENU NA UMUHIMU WAKE KWA SOFTWARE REPAIR

(PART 1 EP01)


View attachment 1244323

Habari Wanandugu.

Ni Ijumaa ya kwanza leo ya somo letu la laptop repair, na katika part 2 hii tutaangalia SOFTWARE Issues Tu.
Tujue Kidogo Nini Maana Ya Software Kwenye Laptop Au Computer Yoyote

Software Kwa Lugha Rahisi Ni Part Ya Computer Ambayo Huwezi Kuishika Na Mkono, Virtual Unakiona Lakini Huwezi Kukishika, Kama Vile Application, Themes, Cursor Etc
Software Ndio Inakupa Wewe Hali ya kuzungumza na computer, Kwa lugha nyingine ni USER INTERFACE.
Kwenye laptop repair practically, Software Inajumlisha, ALL Computer Apps, Operating System, BIOS, Etc.

Kwa Leo Tuangalie BIOS MENU Ambao Ni Msingi Mkubwa Wa Software Repair Na Kwa IT Professional Yoyote Hapa ndipo pa kuanzia kwenye software repair.

BIOS ni nini?
BIOS ni program iliyo na mahusiano mojamoja na laptop au computer yoyote kwa sababu ina chip iliyopo ndani ya motherboard, chip hiyo ndiyo inafanya kazi ya kuunganisha vifaa vyote vilivyopo ndani ya computer kufanya kazi kwa usahihi, kwa lugha sahihi huu ndiyo moyo wa software kwenye computer, hii ndio mwalimu mkuu wa software zote ikiwemo Operating System, Ukibonyeza Button ya kuwasha laptop anayeguswa na kutoa ruhusa ni bios na yeye ndio anaielekeza computer, Utachukua Software Wapi Either Kwenye HDD, USB Drive Au CD ROM,Etc.

BIOS Menu Ni Nini?
Ni Mpangilio Wa BIOS Katika Laptop Unaompa Ruhusa Mtumiaji Kufanya Chaguzi Mbali Mbali Kabla Ya Kufikia Katika Operating System.

Kipi Naweza Kukifanya Kwenye BIOS Menu?
  • Unaweza Kuiwekea Password Laptop Yako (Hii ni safe Zaidi kuliko ya windows)
  • Unaweza Kuangalia Taarifa Za Laptop Yako (System Info)
  • Unaweza kuiamrisha laptop yako ifuate windows kutoka kwenye Nini Mfano: HDD, USB Drive Au CD ROM
  • Unaweza Kufunga Matumizi ya Kifaa Kimoja Au Vingi Kwenye Laptop Yako, mfano: Port za USB, Speaker, Touchpad, WLAN Etc
  • Unaweza Kupunguza Nguvu za matumizi ya Laptop yako kwa kutumia menu ya Multiprocessing na Virtual Technology
  • Unaweza Kuangalia Life time na Status ya battery lako
  • Kubadili saa na kujua OS Ya Kwanza Kuwekwa Kwenye Laptop Yako.
  • Etc

NITAIPATAJE BIOS MENU?
Laptop zote zina bios menu tofauti, zinafanana baadhi kwa brand name mfano: DELL Nyingi Bios Ni F2 Na HP nyingi Bios Ni F9.
List Ya Bios Ipo Hapa Chini:

View attachment 1244326

  • Zima laptop yako
  • Bonyeza Key Kama Zinavyoonekana Hapo Juu (Hutegemea na BRAND YAKO)
  • Bonyeza kwa kuachia achia kama unaipiga ipiga mara nyingi maana mara nyingin hapa tunaotea
  • Unabonyeza pale laptop inapowaka na kuonyesha brand name (kuwa makini sio zote zinaonyesha brand name nyingine zinakuwa kwenye FAST BOOT)
  • Kama itagoma jaribu kwa kubonyeza huku ukiwa umeishikilia Function Key (Fn).

VILIVYOPO KWENYE BIOS MENU NA MATUMIZI YAKE

Hapa hutegemea na Bios Yenyewe Hapo Chini Nimetumia mfano wa Phoenix But Inaweza kuwa WARD Etc So Usikariri ila vingi vinafanana.

Tutumie mfano hapo chini.

View attachment 1244331

MAIN = Hapo utaakuta sifa za laptop yako au STEM INFORMATION
Utajua Size ya RAM, HDD, Processor Na Serial Number Ya Laptop
Sio muhimu sana kwa repair technician

ADVANCED = Hapa ni muhimu kwa technician kwa maana hapa utapata Option ya Kuzima Ports, Au WLAN au Fn Key Au Speaker, Na Touchpad Hapa Utapata Menu ya Kupunguza Nguvu Ya Pc Na Processor, Na Kwa Gamers Amba Ndio Kuna Virtual Technology, Pia Hpa ndio kuna SATA MODE Ya HDD Ukibadili Hii Windows Hauwez Run Kwa Mode Tofauti na uliyoweka wakat unafanya installation.

SECURITY = Hapa utapata menu ya kufunga Password Za Laptop Yako (BIOS PASSWORD, HDD PASSWORD, ADMIN PASSWORD).

BOOT: Hapa utapata menu ya kuiamrisha laptop wapi ikachukue windows wakat inawaka, hapa ni muhimu sana wakati unataka kufanya installation ya windows kwa kutumia external device kama USB FLASH, UEFI MODE NA LEGACY MODE Zinapatikana hapa.

MATATIZO YA BIOS NA UTATUZI WAKE
Kuna matatizo mengi ya laptop lakini yafuatayo ni common na nimekumbana nayo sana.

1. BIOS PASSWORD
Hili ni tatizo sana na huwa nacharge pesa nzuri kulitatua, hii ni ile password tuliyoiona pale juu ambayo inatokea kabla booting haijafanyika.
Ukiwasha PC Utaona Hivi
View attachment 1244332

JINSI YA KUTATUA TATIZO HILI
Kuna njia nyingi za kutatua BIOS Hutegemea Brand na Model Ya Laptop na Skills Alizo nazo Technician
  • Kutumia Backdoor Password: hii ni common password ambazo zipo tayari kwenye bios kutoka kwa manufacture lengo la hizi ni kutumika wakat wa Emergency Ku Reset, Ili Kupata Hizi Password, Washa PC Nenda Kwenye BIOS Password Ingiza Randomly Psssword Zozote Mara 3, Then laptop itakuandikia SYSTEM DISABLE, Na itakupa namba Tano Copy Hizo Namba,Then Tafuta laptop nyingine nzima Nenda Kwenye Hii Site BIOS Master Password Generator for Laptops. Andika Disable code zako then Utapewa List ya Password Za Kujaribu Kufanya Reset.

  • Toa CMOS Battery.
  • Kama unaweza kufungua na kutoa CMOS Battery basi unaweza kufanya hivyo, Then ukawasha pc Unaweza Ukaitoa.
View attachment 1244337

  • CMOS Discharge.
  • Hii ni advanced kwa tech yoyote anatakiwa kuifanya lakini ni lazima kuwa makini kwa maana ukishindwa kujua PIN Out za CMOS unaweza kuiharibu motherboard, Hii Inafanywa kwa kutoa CMOS Battery na kutafuta CMOS Pin Out Kweny Board na kupigisha Short. Means Unawasha laptop then unagusanisha hizo pin kwa kutumia Tweezer, The PC Itajizima, Ukiwasha Itakuwa haina Tena Password, Mchezo Huu Tunaufanya Sana Kwa Toshiba Na ACER, Kumbuka Kila motherboard ina PIN OUT Zake, So Kuangalia Schematica Au Ku Google Hakuepukiki.
  • Mfano wa PIN OUT Huo hapo Chini:
View attachment 1244338

c) Kufanya Short Kwenye SCL na SDA Chip.

SCL na SDA chip inabid uzifanyie location kwa kutumia Schematic, Pia Utafanya Kama kwenye CMOS Discharge Hapa Utaangalia PIN out,

Mfano Hapo Chini.
View attachment 1244341

2. TOUCHPAD HAIFANYI KAZI, USB PORT HAZISOMI AU WLAN HAIFANYI KAZI.

Hili na nalo ni tatizo haswaa kwa laptop za TOSHIBA, Ukifanya Kutoa Tu CMOS Batterry Automatic CMOS Inafanya Reset, Mwisho wa siku inazima ToucHpad kwenye BIOS Menu.
USB Mode Pia Huwa Unazimwa 3.0, Mwisho wa siku Port Inakuwaga Umeme (5V) Lakini USB Device Haisomi Kabisa, Au WLAN.

SULUHISHO
Nenda Kwa BIOS Menu Upande Wa Advanced Then Angalia Kama Imezimwa Washa Na Epuka Kuchomoa CMOS Battery Mara Kwa Mara.

3. USB DEVICE HAIONEKANI WAKATI WA KUINSTALL WINDOWS KWA USB

Hii pia hutokea sana, haswaa kwa hizi laptop mpya, haijawahi kufanyiwa installation ya windows .
SULUHISHO
Nenda kwa Boot Menu Angalia Kama USB Boot Device Ipo Selected Au La, Then Iweke Iwe Your First Priority, Ukiwa unayafanya haya USB Flash Drive Yenye Windows Lazima Iwepo.

NB: Notice Za Session Hii Zipo Chini Hapo Kwa PDF.


MATATIZO YAPO MENGI, KAMA KUNA YOYOTE MWENYE NAYO AFANYE NYONGEZA HAPO NA KARIBUNI KWA DISCUSSION.

KUMBUKA KILA WAKATI, UKIWA UNAJIFUNZA LAPTOP REPAIR MWALIMU WAKO MKUU NI INTERNET


Tukutane Next Week Kwa Part 2 E02 Kama Mungu Akipenda.

Wasalaam.

Mtwara Smart.
Pamoja mkuu
 
Mkuu hivi pc ambayo ipo connected kwenye local area network na iko restricted ku install program yeyote yaani unapo install program inadai administrator password.
Hicho kikwazo nakirukaje?
 
Mkuu Hapo Nadhani Unachanganya Vitu, Admin Password Ya Laptop Haihusiani Na Windows Na Inatokea Pale Tu PC Inapowaka Pre Booting.
Admin Password Ya Windows Ni Rahis Sana Kutoka Kuliko Ya Bios.

Labda Nikuulize Hiyo Admin Password Inatokea Muda Gani Ukiwasha PC Kabla Ya Windows Au Kwenye Windows?
Hii PC nilikuwa naitumia ofisini, kuna kipindi nilitoka kikazi, nikamuachia aliyekuwa anafanya kazi na mimi.

PC watu wa IT waliweka Administration password, na hii mimi niliongea na mtu wa IT baada ya kuambiwa jamaa anaitumia Laptop vibaya.

Huko nilikoenda nimeshindwa kurejea pale ofisini na Laptop yangu nimeenda kuichukua. Shida ipo hapa, siwezi kuinstall chochote pasipo hii password kuwepo, siwezi kumake baadh changes pasipo hiyo password na naogopa kupiga windows sababu sifanya partition na nna vitu vingi mno vya msingi.
 
Back
Top Bottom