Dar: Sakata la Polisi kuuana wenyewe nje ya benki laacha sintofahamu

Dah nchi hii POLISI hata wakienda kikosi kizima kupambana askari wa JWTZ tena PRIVATE asiye na silaha wanaweza kufa WOTE.
Na wanabahati mwenzetu hajafa maana tungewafuata palepale FFU-Ukonga tukitumia askari wa AIRWING 603KJ Au Gongo la mboto 511KJ

Na niwaambie ukweli mchungu wanaJF msioelewa haya mambo ya kijeshi kuwa mjeshi anatibiwa na akipona anarudi kuendelea na kazi kama kawaida na pongezi atapewa za kutosha na muda sio mrefu atapanda na cheo.

Huu ni kweli mchungu,msiamini mtakacho tangaziwa kuwa kapewa adhabu kali.Ni uongo mkuu!
Usitulishe matango pori humu mkuu hakuna upumbavu kama huo katika sheria ulifuatilia pale mahakama ya kusutu kuhusu hyo kesi na mtuhumiwa alienda na nin?
 
Hivyo kwa kuwa hutakiwi kuamini inakupasa kumimina risasi tena hovyo...


Bora hata mngekuwa mnafahamu jinsi ya handle a gun na ku-hit a target....ona sasa mlivyojiabisha badala ya ku-hit target likaenda muua mwenzake...

Nyie polisi mlipjitokeza huku kutetea ndio mnaharibu kabisa.....
Wanajivunia hizo gun zao kwa vile wamefundishwa kupiga risasi tu na siyo kulenga shabaha!
Hata hivyo haikuwa mpango wa Mungu kumuua mwanajeshi ndo maana alibaki na huyo sijui nani kulwa akapitiwa kama ile risasi ilokuwa inaenda kwa mbowe ikapaa juu halafu ikakata kona kurudi kwenye daladala na kumpitia akwilina.

aitiviiiiiiii,maraaaaa!!!
 
Hivyo kwa kuwa hutakiwi kuamini inakupasa kumimina risasi tena hovyo...


Bora hata mngekuwa mnafahamu jinsi ya handle a gun na ku-hit a target....ona sasa mlivyojiabisha badala ya ku-hit target likaenda muua mwenzake...

Nyie polisi mlipjitokeza huku kutetea ndio mnaharibu kabisa.....
Humu hakuna polis humu wewe leta hoja zenye mashiko mtu akiongea ukweli mnasema polisi mbona hao walio upande wa jw hamsemi jwtz

Acha ujuha huo nyinyi ndio wale wale mnaongozwa akil na mange kimambi
 
Wewe bila ubishi ni Polisi....

Ukitaka idara yenu ya Polisi iheshimiwe ni pale mtakapoacha kutumiwa na Wanasiasa
Hakuna kitu kama hicho huwa naheshimu saana watu wanao risk maisha yao kwa ajili yetu wakati tunakula mvinyo

Mm sio wew usiekuwa na maarifa ya kutosha kichwani
 
Kifo cha askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Konstebo Kulwa Gilbert, aliyepigwa risasi kwa bahati mbaya na mwenzake, kimezua mshtuko kwa ndugu, jamaa, askari wenzake na majirani aliokuwa akiishi nao nyumbani kwake, Ukonga-Mazizini jijini Dar, Gazeti la Uwazi pekee ndilo lenye mkasa mzima wa tukio hilo.

NI SINZA JIJINI DAR
Tukio hilo la kusikitisha lililotokea Jumanne ya wiki iliyopita, majira ya jioni wakati afande Kulwa na FFU wenzake wakiwa na askari wa kampuni binafsi ya ulinzi wakishusha pesa kwa ajili ya kuziweka kwenye mashine ya ATM ya Benki ya CRDB iliyopo Sinza-Mori pembezoni mwa Kituo cha Mafuta cha Big Bon, jijini Dar.

Mashuhuda wa tukio hilo waliliambia Uwazi kuwa, wakati maafande hao wakiwa kwenye harakati za kushusha pesa hizo karibu na mashine hiyo, kulikuwa na askari wa JWTZ aliyekuwa akitaka kutoa pesa kwenye mashine hiyo hivyo afande Kulwa na wenzake walimuamrisha aondoke haraka eneo hilo kwa sababu za kiusalama.

MASHUHUDA WASIMULIA
Kwa mujibu wa mmoja wa mashuhuda hao, Jimmy Kaishozi, mkazi wa Sinza-Meeda, mwanajeshi huyo, baada ya kupewa amri ya kuondoka haraka eneo hilo, aliona kama amedharauliwa na askari hao hivyo aliwataka wamwambie kistaarabu na siyo kumwamrisha.

Kaishozi alisimulia kuwa, hali hiyo ilizua malumbano kati ya askari hao na mwanajeshi huyo ambapo Kulwa alimfuata jamaa huyo akiwa na bunduki mkononi huku akimuelekezea ambapo mwanajeshi huyo aliikamata na kuelekezea mtutu juu, jambo lililoonekana kuwa alikuwa na utaalam wa masuala ya silaha.

“Kitendo hicho kilizidisha taharuki ambapo askari mwingine wa FFU naye alitoka kwenye gari lililokuwa limebeba pesa na bunduki nyingine na kumlenga mwanajeshi huyo, lakini katika hali iliyoonekana kama bahati mbaya, risasi hizo zilimpata afande Kulwa na nyingine ilimlenga mwanajeshi huyo.

“Hapo mapambano yalizidi kukolea kama sinema ya kivita ambapo askari aliyekuwa akilenga shabaha, alipoona amempiga mwenzake, aliikoki tena bunduki na kumpiga risasi nyingine mwanajeshi huyo ambapo afande Kulwa na mwanajeshi huyo, wote walianguka chini na kuanza kutapatapa huku wakitokwa na damu nyingi.

“Ilichukua muda wakigaragara chini hadi walipofika askari wa Kituo cha Polisi cha Kijitonyama (Mabatini) na kuwachukua, sijui walipelekwa wapi,” alisimulia Kaishozi.

KITUO CHA MABATINI
Hata hivyo, habari kutoka Kituo cha Polisi cha Kijitonyama (Mabatini) ambapo mwandishi wetu alifika, baadhi ya polisi walithibitisha kutokea kwa tukio hilo, wakisema kuwa majeruhi walikimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambapo wakiwa njiani afande Kulwa aliaga dunia.

MAKAO MAKUU FFU
Mwandishi wetu pia alikwenda Makao Makuu ya Kikosi cha Askari wa Kutuliza Ghasia (FFU), Ukonga-Madafu jijini Dar ambapo aliwakuta askari wenzake marehemu ambao walionesha hisia za majonzi wakati wakizungumzia kifo cha mwenzao huyo.

Askari hao hawakuwa tayari kuandikwa majina kwa maelezo kuwa hawaruhusiwi ambapo walimwelekeza mwandishi wetu nyumbani kwa marehemu Ukonga-Mazizini jijini Dar.

NYUMBANI KWA MAREHEMU
Mwanahabari wetu alifika nyumbani kwa marehemu, lakini alikuta chumba chake kimefungwa ambapo mtu aliyekutwa nyumbani hapo alisema kuwa, msiba ulihamishiwa Tazara-Mchicha kwa dada yake aitwae Doto ambaye ndiye pacha wake.

Mwandishi wetu alizungumza na majirani aliowakuta eneo hilo ambao walisema kuwa, kifo hicho kilisababisha mshtuko mkubwa mtaani hapo na kuibua majonzi makubwa.
Kutokana na afande huyo kuishi vizuri na majirani zake, mwandishi wetu aliwakuta wakiendelea kuchangisha pesa za rambirambi huku wakiwa na picha ya marehemu.
ACP Muliro Jumanne Muliro.

UJIJI, KIGOMA KWA MAZISHI
Mwanahabari wetu pia alifika alipoelekezwa ulipokuwa msiba huo, lakini alipofika alikuta tayari mwili wa marehemu ulishasafirishwa kupelekwa kijijini kwao, Ujiji mkoani Kigoma kwa ajili ya mazishi.

MWANAJESHI MUHIMBILI
Habari kutoka Muhimbili zilidai kuwa mwanajeshi aliyepata kisanga hicho yeye anaendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo japokuwa hakuna afisa habari yeyote katika hospitali hiyo aliyekuwa tayari kuzungumzia tukio hilo.

“Ni kweli huyo mwanajeshi yupo, lakini chini ya ulinzi mkali, itakuwa vigumu ninyi kumuona,” alisema mmoja wa askari ambaye hakupenda jina lake kuandikwa gazetini hospitalini hapo.

KAMANDA MAMBOSASA
Alipoulizwa juu ya tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Lazaro Mambosasa alisema angempigia mwandishi baadaye.

KAMANDA MULIRO
Mwandishi aliamua kumpigia Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, ACP Muliro Jumanne Muliro na alipoulizwa juu ya tukio hilo alisema ni vema kuzungumza na Kamanda wa Kanda Maalum.

“Ndugu yangu si unajua kuwa kuna Kamanda wa Kanda Maalum? Mpigie yeye,” alisema Kamanda Muliro.

Alipoambiwa amepigiwa hajajibu swali ndiyo maana akapigiwa yeye RPC, Muliro alisema atampigia yeye Mambosasa.

Mwandishi alimpigia simu tena Kamanda Mambosasa na kumueleza kuhusiana na tukio hilo ndipo akasema yupo chumba cha daktari na akaahidi kumpigia mwandishi baadaye.

MSEMAJI WA POLISI
Hata hivyo, ili kupata undani wa tukio hilo, pia Uwazi lilimtafuta Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, ACP Barnabasi Mwakalukwa na kumuuliza juu ya taarifa za tukio hilo ambapo aliomba atafutwe Kamanda Mambosasa.

“Hilo jambo anayepaswa kulizungumzia ni Kamanda Mambosasa, mtafuteni huyo,” alisema Kamanda Mwakalukwa.

UWAZI LAMRUDIA MAMBOSASA
Uwazi lilimrudia tena Kamanda Mambosasa na kumtaka kulizungumzia tukio hilo ambapo alikiri na kusema kuwa, kulikuwa askari waliofanya tukio hilo walimdhania mwanajeshi huyo kuwa ni jambazi.

Haikujulikana mara moja kama polisi aliyempiga risasi mwenzake pamoja na mwanajeshi huyo kama amekamatwa au la.

KUMRADHI
Jina la Konstebo Justine Mtesigwa, ambalo awali lilitumika kwenye habari hii kwenye gazeti la Uwazi leo kwamba ndiye aliyeuawa lilikosewa, jina sahihi ya aliyeuawa ni konstebo Kulwa Gilbert. Justine na Kulwa walikuwa ni marafafiki na walikuwa wakifanyakazi pamoja Ukonga. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza kwa Justine, ndugu, jamaa, marafiki na wafanayakazi wenzake – Mhariri.

Stori: Richard Bukos, Dar.

My Take;
Polisi wawili kupambana na Mwanajeshi mmoja asiye na silaha na kuishia kuuana wenyewe ni picha kuwa hawa wanahitaji mafunzo ya uhakika ili unyonge wao wasiutumie kuwaonea raia wasio hatia
askari wa jeshi la police na wale wa jwtz ni kama kaka na dada wa tumbo moja kwa maana lengo lao ni moja nalo ni kulinda usalama wa taifa letu hili pendwa kwa njia tofauti tofauti.
hizi tofauti ndogondogo (skirmishes) huwa ni za kibinadamu sana kwa watu wa familia moja, hata ninyi leo hakuna mmoja wenu anayeweza kusema hakuwahi kugombana na ndugu zake angali anakaa na wazazi wake. tusiwe tunapenda kukuza mambo madogo na kuyafanya yanakusa ni issue kubwa sana zisizo na faida zozote zile za msingi.
 
Nchi yeyeto ile polisi siyo lolote siyo chochote mbele ya Jeshi. Kikinuka polisi wanaamriwa KAENI KAMA RAIA! Amini usiamini polisi wanavua magwanda na kwenda kujificha mvunguni mwa vitanda vyao. Jeshi siyo polisi bwana.
 
Karma is a bit....ch
Jeshi la polisi lilifaa liundwe na wasome yaani wenye elimu ngazi ya degree na masters wenye G.P.A 2.5 kwasbb polisi ni msimamizi na muangalizi wa sheria.
Waliofeli form 4 walipaswa kwenda JWTZ, na magereza. Km jeshi la polisi linageuzwa tawi la chama fulani. Unategemea nini kitatokea? Raisi anasema hakuna siasa. Je, sheria na katiba zinasemaje? Leo ccm wakifanya mkutano hakuna shida sasa ngoja vyama upinzani vifanye mkutano. Polisi watakuja kuvamia utafikiri hapo ni mkutano wa kikundi cha magaidi.
Jiulize km hapo. Mtu hana bunduki lkn unamtishia bunduki halafu cha kushangaza mwenzake analenga tu hana hata shabaha.
Hapo kulikuwa hakuna haja ya kutumia silaha. Ni mazungumzo tu sbb wote wapo kwenye sekta moja lkn vitengo tofauti.
Kazi kweli kweli
Jeshi ni Kitu sensitive sana katika nchi! Jeshi ni zaidi ya mapigano leo unataka kupeleka failure uko Utangamiza nchi wewe, Taifa lolote Swala la Security na Elimu ni lazima lipewe kipaumbele kikubwa sana.
 
Dah nchi hii POLISI hata wakienda kikosi kizima kupambana askari wa JWTZ tena PRIVATE asiye na silaha wanaweza kufa WOTE.
Na wanabahati mwenzetu hajafa maana tungewafuata palepale FFU-Ukonga tukitumia askari wa AIRWING 603KJ Au Gongo la mboto 511KJ

Na niwaambie ukweli mchungu wanaJF msioelewa haya mambo ya kijeshi kuwa mjeshi anatibiwa na akipona anarudi kuendelea na kazi kama kawaida na pongezi atapewa za kutosha na muda sio mrefu atapanda na cheo.

Huu ni kweli mchungu,msiamini mtakacho tangaziwa kuwa kapewa adhabu kali.Ni uongo mkuu hata kama kesi itafika kisutu!
We jamaa ni askari au mwanafunzi wa 4th year??
 
Bhana waende zao...pole mjeda...Nimekumbuka tukio moja la yule Traffic alikuwa anavua koti ili amwajibishe mshikaji walikuwa kama watatu kama sijakosea akampiga jamaa akawa ametulia tuu.Sasa angekuwa mjeda yule traffic angeisoma namba

Nakumbuka matukio polisi wakija mtaani kwetu wamekuta vijana wamekaa nje usiku wanapiga soga kama unavyojua uswahilini huwa tunakaa nje usiku maana ndani joto...wakija wanavamia tunakula virungu wakati hatuna hatia wala silaha yoyote tuna pandishwa kwenye defender lao tunapelekwa kituoni hapo umesha sachiwa kama una pesa imeenda na maji.

Ukifika kule kituoni waanza kukuangalia mdomo na mavazi(muonekano) ili wajue wakupe kosa gani...Ukiwa mweusi mweusi tayari wewe mvuta banghi....Ukiwa umekonda konda utasikia huyu anatumia madawa ya kulevya. Sasa jifanye hata kunyanyua mdomo uone virungu utakavyo pigwa.

Najua jeshi la polisi na polisi mpo huku viovu vyote mnavyo vifanya ni mnapandikiza chuki kwa raia...Mfano mdogo ni hata maoni mnayo yaona sasa ni kutokana na chuki ya jamii juu yenu. Raia wanawaombea mabaya kuliko mazuri.

Tatizo kubwa kwenu ni ELIMU TU....Elimu humfanya mtu kustaarabika na kujua kumanage mazingira ya aina tofautitofauti kwa resources zinazomzunguka. Sasa nyie ubabe,ulimbukeni,majivuno na masifa ndio yamewajaa

Mfano umenikuta ATM natoa pesa nina haraka nawahi hospital kumuuguza mwanangu...Wewe Askari ukaja ukaniambia Samahani mzee tunaomba tukukatishe unachofanya tunashusha mzigo wa pesa ni hatari kwa raia wa kawaida kuwepo karibu nasi....Unafikiri nitaacha kukupisha??

Sasa nyie mnaenda Weee wee toka hapo haraka...sogea kule....ptuu mimi kwa sababu sina hata bakora nitasogea nikiwa nasononeka moyoni BUT ningekuwa mjeda Wallahi ningetaka mtumie lugha nzuri kuniondoa .
 
Haka kagazeti uchwara ila kameandika vizuri mimi huwa sisomi hivi vipeperushi
 
Jeshi ni Kitu sensitive sana katika nchi! Jeshi ni zaidi ya mapigano leo unataka kupeleka failure uko Utangamiza nchi wewe, Taifa lolote Swala la Security na Elimu ni lazima lipewe kipaumbele kikubwa sana.
Huko hakuna shida sbb ukiingia vitani ni mwendo wa kuua tu. Huyu failure unamuachia kulinda raia na mali zao si ataendelea kuua tu. Angalia kwa Akwilima, angalia kwa mwandishi yule aliyeuwawa.
Huyo aliyempiga risasi mwenzake unafikiri alikuwa sahihi?
Yaan hata km raia umepewa bunduki, unaweza kumsogelea adui mpaka karibu? Wanashindwa hata technics wanazotumia majambazi
 
Back
Top Bottom