kiboksi manyoya
JF-Expert Member
- Nov 16, 2016
- 377
- 311
Leo muda wa 05:25 alfajiri eneo la bahari upande wa Kigamboni, Kivuko cha MV Magogoni kilichokuwa kinatoka Kigamboni kwenda upande wa Magogoni kimegonga boti ya uvuvi iliyokuwa inatoka ferry soko la samaki kwenda Kigamboni eneo la encorage,
Watu waliokuwa kwenye boti walijitosa baharini huku boti hiyo ikiburuzwa na MV Magogoni kwa umbali kadhaa na baadae MV Magogoni ilisimama na kuiacha boti ikielea bila uelekeo maalum, wajuzi wa sheria za bahari watueleze nani mwenye makosa kati ya MV Magogoni na boti ambayo ilitaka kupita mbele ya kivuko ambacho kiko kwenye mwendo, ilikuwa ni usiku sikuweza kupiga picha.
Watu waliokuwa kwenye boti walijitosa baharini huku boti hiyo ikiburuzwa na MV Magogoni kwa umbali kadhaa na baadae MV Magogoni ilisimama na kuiacha boti ikielea bila uelekeo maalum, wajuzi wa sheria za bahari watueleze nani mwenye makosa kati ya MV Magogoni na boti ambayo ilitaka kupita mbele ya kivuko ambacho kiko kwenye mwendo, ilikuwa ni usiku sikuweza kupiga picha.