Arusha,Zanzibar,Kilimanjaro,Mara na Mbeya ni moja kati ya sehemu ambazo zimekuwa ukipata sifa lukuki juu ya uzuri wa maeneo ndani ya mikoa hiyo.
Uzi huu ni maalum kwa ajili ya kuonesha uzuri wa Dar,Jiji ambalo mamillion ya watu pamekuwa nyumbani....Kuna maeneo mengi mazuri na vivutio vingi ndani ya mkoa huu ambavyo wengi hawavijui tu.
Tutaanza kwa kuangazia Vivutio vilivyopo Wilaya ya Kinondoni.
MBEZI BEACH : I
Fukwe za Mbezi,
Kata : Kawe
Wilaya : Kinondoni
Utafaidi:
- Kuogelea kwenye fukwe na swimming pool
- Upepo mzuri wa Fukwe
- Chakula kizuri na Vinywaji
- Michezo ya kwenye maji
- Kuendesha boti ndogo
Eneo lenye uzuri wa kipekee ambalo lina mchanganyiko wa Mazingira ya asili pamoja na yale ya Kujengwa na binadamu.
- Mazingira hayo ya asili ni ufuko wenye mchanga mweupe,Uoto wa mikoko pamoja Bahari.
- Mazingira ya Kujengwa ni Hoteli kubwa zilizopo maeneo hayo pamoja na sehemu za michezo ya kuogelea.
- Hotel:Jangwani,Landmark,White Sands
- Water world
Hii ni picha iliyopigwa kwa juu
unafikaje :
Panda gari/bajaji/bodaboda hadi ufike kituo cha basi cha Mbezi Afrikana..ulizia wenyeji Fukwe ya Africana ilipo
Gharama : Nauli kutokea Africana,haizidi 1,000 kwa Bajaj
Kwa huduma za Hotel,Migahawa uwe na takribani 20,000 tsh
Usalama : 90 %
wajuze wenzio