Dar es Salaam -dirtiest city and beaches

Dar es Salaam -dirtiest city and beaches

Firigisi

Member
Joined
Feb 13, 2009
Posts
91
Reaction score
33
Pamoja na Dar es Salaam kuwa na upepo mwanana na mandhari nzuri kutokana na uwepo wa Bahari, Fukwe za Jiji la Dar es Salaam limejaa uchafu wa plastic bags , bottles , na kila aina ya uchafu. Tunaomba mamlaka husika zijipange vizuri kufuatilia usafi wa fukwe mara kwa mara, labda kwa kushirikisha wamiliki wa hoteli zinazozunguka maeneo yenye fukwe, kampuni za usafi za binafsi na wananchi ili kurejesha mandhari nzuri yenye uhalisia wa fukwe zenye hali ya usafi zitakazovutia . Uchafu huu sio tu ni hatari kwa nchi inayotegemea sana mapato kwenye utalii , bali pia ni hatari kwa uhai na ustawi wa viumbe wa majini na madhara mengine ya kiafya kwa watumiaji na hasa watoto.
Hili linakera sana na wengi waliotembelea baadhi ya fukwe zetu mtakubaliana kuwa hali si nzuri hata kidogo (angalia picha).Jambo hili linahitaji ufuatilia wa karibu Wizara ya Muungano na Mazingira na Utawala wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Usafi wa fukwe na maeneo mengine unategemea sana upigaji marufuku chupa na mifuko ya plastiki. Hili jambo limeshaongelewa mara kadhaa , Zanzibar , Kenya na Rwanza wameweza bila plastiki , tuchukue hatua tuache kigugumizi.

Nawasilisha kero yangu kwa wahusika
 

Attachments

  • 2017 DSM (1).jpg
    2017 DSM (1).jpg
    120.7 KB · Views: 31
  • 2017 DSM (2).jpg
    2017 DSM (2).jpg
    139.8 KB · Views: 31
  • 2017 DSM (3).jpg
    2017 DSM (3).jpg
    143.7 KB · Views: 27
dar ndo inaongoza kwa vijana wanaotembeza pumbu mchana kutwa na hawan ajira,usidanganyike na kupendeza kwao wengi hawana hata mahala pa uhakika pa kulala,wakamatwe hao kila siku wakasafishe fukwe hizo.
 
Naona unamtafuta mtu ili aliwe kichwa maana, hii thread inagusa maeneo.

Ngoja wenyewe waje!!
 
Back
Top Bottom