nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Sasa Hivi Gazeti La Rai Linafanya Uchambuzi wake kwa Chama Tawala; Very Interesting Article.
Makala na Uchambuzi, Rai
Na Prudence Karugendo
WALIOKUWA marais wa Tunisia na Misri, Ben Ali na Hosin Mubaraka, ilikuwa imefikia kipindi wakawa wanajulikana kama madikteta kutokana na kukaa sana madarakani bila kufikiria kung'atuka.
Lakini katika muda wote waliokuwa madarakani marais hao walikuwa wakiendesha chaguzi kila baada ya kipindi fulani ili ukaaji wao madarakani uonekane ni wa kidemokrasia, ila chaguzi zote walizokuwa wakiziendesha walikuwa wanahakikisha zinawafanya wao wabaki madarakani na hivyo kuufanya udikteta wao uonekane una ridhaa ya umma, ridhaa ya wananchi.
Kwa njia hiyo watawala hao wakawa wameiteka nyara demokrasia ya nchi zao na kuanza kuitumia jinsi walivyotaka wao, kwa manufaa binafsi dhidi ya manufaa ya umma, umma ambao muda wote wa zaidi miongo mitatu umebaki ukitaabika bila kujua la kufanya, sababu kiufundi hali hiyo ya tabu na mateso, kwa umma wa Tunisia na Misri, ni kama ilikuwa ya kujitakia kutokana na kilichoonekana umma huo kutopenda kufanya mabadiliko.
Watawala hao wa Tunisia na Misri, kwa kujinufaisha na hali hiyo waliyojitengenezea ili waonekane wangÕangÕaniwa na wananchi wa nchi zao kubaki madarakani, wakawa wanafikiria kuurithisha utawala wa nchi zao kwa watoto wao kama wafanyanyavyo wafalme. Kwa hiyo demokrasia ikatoka kwa wananchi na kuhamia kwenye familia za madikteta hao.
Wananchi ambao tayari walishazungukwa wakiwa wamepokonywa demokrasia yao na kubaki kama mihuri tu ya kuidhinisha udikteta wapende wasipende, wakaamua kuvunja kuta za ngome za madikteta hao na kuamua kuichukua kwa nguvu ya umma demokrasia yao. Madikteta wakasalimu amri na kukubali kungÕoka madarakani. Kwa hiyo demokrasia katika nchi hizo ni lazima itarudi kwenye mkondo wake baada ya kupotea njia kwa zaidi ya miongo mitatu.
Lakini pamoja na watawala hao kuondoka madarakani kwa njia hizo zinazoonekana ni za aibu, bado wamejitengenezea heshima. Wamekubali kutii amri mbele ya nguvu ya umma. Wamekiri ulaghai wao waliokuwa wakiutumia kuiadaa dunia kuwa wanang'ang'anizwa madarakani na wananchi wan chi zao. Sasa wameyatambua na kuyakubali matakwa halisi ya umma katika njia ambazo hazikuwa na aina yoyote ya uchakachuaji. Tuseme ule ungekuwa ni uchaguzi, kama walivyokuwa wamezoea, wangeweza kuuchakachua ili ionekane kwamba matakwa ya umma bado yanawataka waendelee kubaki madarakani.
Heshima waliyojijengea inakuja namna hii; pamoja na ukweli kwamba umma ulishaamua kuwaondoa madarakani watawala hao, katika njia zisizowezekana kuchakachuliwa, bado Ben Ali na Hosni Mubarak walikuwa wameshikilia turufu kubwa ambazo zingeweza kuwabakisha madarakani kwa njia zozote zile. Kila mmoja wao alikuwa ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya nchi yake.
Hivyo wangesema wabaki madarakani hata kwa kumwaga damu, mpaka sasa wangekuwa bado wako madarakani. Kwahiyo kwa uamuzi wao wa kukubali kuachia madaraka kwa shinikizo la nguvu ya umma ambayo lakini haikuwa na silaha ya aina yoyote zaidi ya umoja, wamejiwekea hazina kubwa ya heshima katika historia ya nchi zao ambayo si rahisi kuisha kwa karne nyingi zijazo.
Ukweli huo unathibitishwa na nguvu za vyombo vya dola vilizonazo vya nchi zile ambazo watawala wale ndio waliokuwa waamiri wake wakuu. Tuchukulie Misri, kwa mfano, kama Mubarak angesema hatoki madarakani bila kujali ni damu kiasi gani ingemwagika, hali ingekuwaje mpaka sasa? Ni wazi kwamba utitiri wa watu ungeishateketea na bado yeye angekuwa yuko madarakani. Lakini hakutaka kufanya hivyo, akaheshimu nguvu ya umma na kuamua kuvikimbia vyombo vya dola ili vibaki kwa manufaa ya nchi na wananchi.
Vile vile upande wa pili nako kunaonyesha kwamba elimu ya uraia ikijengeka vizuri inaleta manufaa kwa nchi na wananchi. Bilashaka vyombo vya dola, Tunisia na Misri, vimejengwa na watu wenye elimu ya uraia inayojitosheleza. Kuanzia Usalama wa Taifa mpaka majeshi ya nchi zile walielewa kwamba wenye nchi ni wananchi, kwahiyo hapakuwepo na ulazima wa kuwaangamiza wananchi ili kuwalinda madikteta ambao wananchi hawawataki. Hivyo ni imani yangu kwamba Ben Ali na Mubarak hawakuamua wenyewe kuzikimbia nchi zao bila kushauriwa hivyo na watu wa usalama wa mataifa yao.
Katika hatua kama hizo ndipo tunapopaswa kuelewa maana halisi ya usalama wa taifa. Sababu katika baadhi ya nchi vitengo vya usalama wa taifa vimekuwa havieleweki majukumu yake hasa pale, kitengo hicho kinapojikita zaidi katika kuhakikisha tu usalama wa watawala vikiwa kimeliacha taifa zima likichungulia shimoni. Hapa maana yake ni kwamba bora taifa zima liangamie watawala wabaki salama. Eti huo ndio usalama wa taifa!
Yanayotokea Kazikazini mwa Afrika yameanza kuwatia kiwewe watawala madikteta wa nchi zilizo chini mwa Jangwa la Sahara kikiwemo Chama Cha Mapinduzi hapa nchini. Wakati tunawaongelea watawala waliokaa madarakani kwa miongo mitatu tumekuwa tukikisahau Chama Cha Mapinduzi ambacho kimedumu madarakani kwa miongo mitano sasa. Chama hiki, tofauti na mtawala wa Libya, Muammar Gaddafi, ambaye kwa sasa naye yuko kwenye kikaango kutokana na kukaa madarakani kwa zaidi ya miongo minne lakini akiwa nalo mkononi la kuonyesha katika kujitetea, CCM haionyeshi lolote zaidi ya propaganda za kichovu zilizopitwa na wakati baada ya kukaa madarakani kwa nusu karne!
Hata kama yapo yanayoelezeka kama ukiukaji wa uhalali yaliyofanywa na Gaddafi dhidi ya watu wa Libya, lakini walau anaweza kusema kwamba amejitahidi kuhakikisha rasilmali za nchi, ambazo yeye amekuwa akizilinda kwa nguvu zake zote dhidi ya wadoeaji wa nje ya nchi yake, zinamnufaisha kila mwananchi. Ushahidi ni kwamba katika Libya hakuna mwananchi anayepanga kwa mwenzake. Taifa lile limehakikisha kila mwananchi anamiliki makazi yake, hiyo ni mbali na posho zinazotolewa kwa watu wasio na ajira.
Hebu tujaribu kulinganisha ushuhuda huo na wa chama tawala hapa nchini kinachopigana kufa na kupona kwa sasa hivi kutaka kulipa makumi ya mabilioni ya shilingi kwa kampuni ya kufua umeme wa dharura wakati nchi iko gizani. Kwa ufupi ni kwamba CCM haina la kuonyesha kwa watu wenye akili timamu wakakubaliana nacho kuwa kinawiana na miaka hamsini ambayo chama hicho kimekaa madarakani.
Isipokuwa kinachoonekana ni kuongezeka kwa kila shida nchini, kuongezeka kwa umasikini wakati rasilmali za nchi zikisombwa kwenda kuwatajirisha watu wa nje. Pengo linalozidi kutanuka kati ya walionacho na wasionacho. Kupanda kwa gharama za maisha kusiko na huruma kwa wanyonge nakadhalika.
Lakini hatahivyo hayo yote ni mambo yaliyokuwa yamedhibitiwa miaka ya mwanzo ya kujitawala kwetu, ambapo kwa upande wa Tanganyika chama cha TANU kilikuwa kimejidhatiti vilivyo kuhakikisha utu wa Mtanganyika na baadaye Mtanzania unalindwa. Vilevile kwa upande wa Zanzibar ASP nacho kikiwa kimejipanga kamili kuhakikisha Mzanzibari na baadaye Mtanzania anaona nini maana ya kujitawala.
Lakini bahati mbaya baada ya vyama hivyo kuungana na kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikaja Kiswahili cha kwamba 'chama kimeshika hatamu'! Baada ya kunogewa na utamu wa hatamu chama hicho kikaamua kujivua gamba lake na kuyapiga teke yote yaliyokuwa yameasisiwa na TANU na ASP. CCM kikawa kimejipindua chenyewe kutoka chama cha wakulima na wafanyakazi na kuwa chama cha mabwenyenye.
Hilo ni kosa kubwa ambalo chama hicho kililifanya kutokana na kulewa upweke na sasa hivi kinalijutia. Sidhani kama CCM, katika ushindani kama huu kilionao kwa sasa, kingethubutu kuwatelekeza wakulima na wafanyakazi na kuwakumbatia mabwenyeye peke yao. Hilo ni kosa la kiufundi lililotokana na kujiona chenyewe ndicho kila kitu.
Siasa, kama mchezo wa mpira wa miguu, adhabu inatolewa pale kosa lilipofanyikia. Kama ni katika eneo la hatari inatolewa adhabu kali, penalty, ambayo ni kama goli la bure. Sasa hivi CCM inaona kama upinzani umepata penalty ndiyo maana inaanza kuhaha kwa propaganda na vitisho vya kila aina. Kiwewe ilichonacho CCM ni cha kwamba penalty hiyo inaweza ikazaa goli la ushindi kwa upinzani na hivyo kukiondoa chama hicho kwenye utamu wa utawala wa miaka 50.
Sasa hivi chama kikuu cha upinzani, Chadema, kimeshika bango nchi nzima kuonyesha yalikofanyikia makosa ya CCM kuwa ni katika eneo la hatari. Badala ya CCM kuomba radhi na kujirekebisha inakuja na vitisho na madai ya kwamba Chadema inatishia amani. Madai hayo pia yanatolewa na mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete, kwamba Chadema inawatia hofu wananchi. Yaani hofu waliyonayo CCM, hasa viongozi, wanailazimisha iwe hofu ya Watanzania wote!
Ni wananchi gani wenye kuwa na hofu na Chadema halafu wajitokeze kwa wingi tunaoushuhudia kuwalaki na kuwasikiliza viongozi wa Chadema? Tena ikumbukwe kwamba mikutano ya Chadema haina burdani, usafiri wa bure wala posho kama vinavyotolewa nyakati fulanifulani kwenye mikutano ya CCM. Eti wananchi wana hofu! Hofu ya nini?
Uwezekano wa kuvunjika kwa amani kutokana na Chadema kuendelea kuwaelewesha wananchi musitakabali wa kisiasa katika nchi yao, unaweza ukaletwa na hofu waliyonayo CCM, na si hofu ya wananchi. CCM wanaelewa makosa yao ndiyo maana wanakuwa wepesi kutaharuki wakiwa wanaelewa hukumu inayoweza kutolewa dhidi yao. Kwahiyo hofu ni lazima wawe nayo, ni hofu ya kunyangÕanywa tonge mdomoni na wala siyo hofu ya kuvunjika kwa amani.
Lakini iwapo CCM wangekuwa na elimu ya uraia ya kutosha, wakielewa kwamba kila chama cha siasa kilichosajiliwa nchini kinayo haki ya kutawala, wasingekuwa na hofu ila wangejipanga kukabiliana na changamoto za Chadema bila woga wala mizengwe, na kupitia njia hiyo wangekuwa wameepusha kile kinachodaiwa kwamba kinaweza kutokea, umwagaji wa damu. Lakini kwa mtindo huu wa kutojiamini unaosindikizwa na woga uliopita mipaka, sielewi kama CCM watatunusuru. Ila nina imani kwamba katika hali yoyote iwayo ukweli utasimama.
Makala na Uchambuzi, Rai
Na Prudence Karugendo
WALIOKUWA marais wa Tunisia na Misri, Ben Ali na Hosin Mubaraka, ilikuwa imefikia kipindi wakawa wanajulikana kama madikteta kutokana na kukaa sana madarakani bila kufikiria kung'atuka.
Lakini katika muda wote waliokuwa madarakani marais hao walikuwa wakiendesha chaguzi kila baada ya kipindi fulani ili ukaaji wao madarakani uonekane ni wa kidemokrasia, ila chaguzi zote walizokuwa wakiziendesha walikuwa wanahakikisha zinawafanya wao wabaki madarakani na hivyo kuufanya udikteta wao uonekane una ridhaa ya umma, ridhaa ya wananchi.
Kwa njia hiyo watawala hao wakawa wameiteka nyara demokrasia ya nchi zao na kuanza kuitumia jinsi walivyotaka wao, kwa manufaa binafsi dhidi ya manufaa ya umma, umma ambao muda wote wa zaidi miongo mitatu umebaki ukitaabika bila kujua la kufanya, sababu kiufundi hali hiyo ya tabu na mateso, kwa umma wa Tunisia na Misri, ni kama ilikuwa ya kujitakia kutokana na kilichoonekana umma huo kutopenda kufanya mabadiliko.
Watawala hao wa Tunisia na Misri, kwa kujinufaisha na hali hiyo waliyojitengenezea ili waonekane wangÕangÕaniwa na wananchi wa nchi zao kubaki madarakani, wakawa wanafikiria kuurithisha utawala wa nchi zao kwa watoto wao kama wafanyanyavyo wafalme. Kwa hiyo demokrasia ikatoka kwa wananchi na kuhamia kwenye familia za madikteta hao.
Wananchi ambao tayari walishazungukwa wakiwa wamepokonywa demokrasia yao na kubaki kama mihuri tu ya kuidhinisha udikteta wapende wasipende, wakaamua kuvunja kuta za ngome za madikteta hao na kuamua kuichukua kwa nguvu ya umma demokrasia yao. Madikteta wakasalimu amri na kukubali kungÕoka madarakani. Kwa hiyo demokrasia katika nchi hizo ni lazima itarudi kwenye mkondo wake baada ya kupotea njia kwa zaidi ya miongo mitatu.
Lakini pamoja na watawala hao kuondoka madarakani kwa njia hizo zinazoonekana ni za aibu, bado wamejitengenezea heshima. Wamekubali kutii amri mbele ya nguvu ya umma. Wamekiri ulaghai wao waliokuwa wakiutumia kuiadaa dunia kuwa wanang'ang'anizwa madarakani na wananchi wan chi zao. Sasa wameyatambua na kuyakubali matakwa halisi ya umma katika njia ambazo hazikuwa na aina yoyote ya uchakachuaji. Tuseme ule ungekuwa ni uchaguzi, kama walivyokuwa wamezoea, wangeweza kuuchakachua ili ionekane kwamba matakwa ya umma bado yanawataka waendelee kubaki madarakani.
Heshima waliyojijengea inakuja namna hii; pamoja na ukweli kwamba umma ulishaamua kuwaondoa madarakani watawala hao, katika njia zisizowezekana kuchakachuliwa, bado Ben Ali na Hosni Mubarak walikuwa wameshikilia turufu kubwa ambazo zingeweza kuwabakisha madarakani kwa njia zozote zile. Kila mmoja wao alikuwa ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya nchi yake.
Hivyo wangesema wabaki madarakani hata kwa kumwaga damu, mpaka sasa wangekuwa bado wako madarakani. Kwahiyo kwa uamuzi wao wa kukubali kuachia madaraka kwa shinikizo la nguvu ya umma ambayo lakini haikuwa na silaha ya aina yoyote zaidi ya umoja, wamejiwekea hazina kubwa ya heshima katika historia ya nchi zao ambayo si rahisi kuisha kwa karne nyingi zijazo.
Ukweli huo unathibitishwa na nguvu za vyombo vya dola vilizonazo vya nchi zile ambazo watawala wale ndio waliokuwa waamiri wake wakuu. Tuchukulie Misri, kwa mfano, kama Mubarak angesema hatoki madarakani bila kujali ni damu kiasi gani ingemwagika, hali ingekuwaje mpaka sasa? Ni wazi kwamba utitiri wa watu ungeishateketea na bado yeye angekuwa yuko madarakani. Lakini hakutaka kufanya hivyo, akaheshimu nguvu ya umma na kuamua kuvikimbia vyombo vya dola ili vibaki kwa manufaa ya nchi na wananchi.
Vile vile upande wa pili nako kunaonyesha kwamba elimu ya uraia ikijengeka vizuri inaleta manufaa kwa nchi na wananchi. Bilashaka vyombo vya dola, Tunisia na Misri, vimejengwa na watu wenye elimu ya uraia inayojitosheleza. Kuanzia Usalama wa Taifa mpaka majeshi ya nchi zile walielewa kwamba wenye nchi ni wananchi, kwahiyo hapakuwepo na ulazima wa kuwaangamiza wananchi ili kuwalinda madikteta ambao wananchi hawawataki. Hivyo ni imani yangu kwamba Ben Ali na Mubarak hawakuamua wenyewe kuzikimbia nchi zao bila kushauriwa hivyo na watu wa usalama wa mataifa yao.
Katika hatua kama hizo ndipo tunapopaswa kuelewa maana halisi ya usalama wa taifa. Sababu katika baadhi ya nchi vitengo vya usalama wa taifa vimekuwa havieleweki majukumu yake hasa pale, kitengo hicho kinapojikita zaidi katika kuhakikisha tu usalama wa watawala vikiwa kimeliacha taifa zima likichungulia shimoni. Hapa maana yake ni kwamba bora taifa zima liangamie watawala wabaki salama. Eti huo ndio usalama wa taifa!
Yanayotokea Kazikazini mwa Afrika yameanza kuwatia kiwewe watawala madikteta wa nchi zilizo chini mwa Jangwa la Sahara kikiwemo Chama Cha Mapinduzi hapa nchini. Wakati tunawaongelea watawala waliokaa madarakani kwa miongo mitatu tumekuwa tukikisahau Chama Cha Mapinduzi ambacho kimedumu madarakani kwa miongo mitano sasa. Chama hiki, tofauti na mtawala wa Libya, Muammar Gaddafi, ambaye kwa sasa naye yuko kwenye kikaango kutokana na kukaa madarakani kwa zaidi ya miongo minne lakini akiwa nalo mkononi la kuonyesha katika kujitetea, CCM haionyeshi lolote zaidi ya propaganda za kichovu zilizopitwa na wakati baada ya kukaa madarakani kwa nusu karne!
Hata kama yapo yanayoelezeka kama ukiukaji wa uhalali yaliyofanywa na Gaddafi dhidi ya watu wa Libya, lakini walau anaweza kusema kwamba amejitahidi kuhakikisha rasilmali za nchi, ambazo yeye amekuwa akizilinda kwa nguvu zake zote dhidi ya wadoeaji wa nje ya nchi yake, zinamnufaisha kila mwananchi. Ushahidi ni kwamba katika Libya hakuna mwananchi anayepanga kwa mwenzake. Taifa lile limehakikisha kila mwananchi anamiliki makazi yake, hiyo ni mbali na posho zinazotolewa kwa watu wasio na ajira.
Hebu tujaribu kulinganisha ushuhuda huo na wa chama tawala hapa nchini kinachopigana kufa na kupona kwa sasa hivi kutaka kulipa makumi ya mabilioni ya shilingi kwa kampuni ya kufua umeme wa dharura wakati nchi iko gizani. Kwa ufupi ni kwamba CCM haina la kuonyesha kwa watu wenye akili timamu wakakubaliana nacho kuwa kinawiana na miaka hamsini ambayo chama hicho kimekaa madarakani.
Isipokuwa kinachoonekana ni kuongezeka kwa kila shida nchini, kuongezeka kwa umasikini wakati rasilmali za nchi zikisombwa kwenda kuwatajirisha watu wa nje. Pengo linalozidi kutanuka kati ya walionacho na wasionacho. Kupanda kwa gharama za maisha kusiko na huruma kwa wanyonge nakadhalika.
Lakini hatahivyo hayo yote ni mambo yaliyokuwa yamedhibitiwa miaka ya mwanzo ya kujitawala kwetu, ambapo kwa upande wa Tanganyika chama cha TANU kilikuwa kimejidhatiti vilivyo kuhakikisha utu wa Mtanganyika na baadaye Mtanzania unalindwa. Vilevile kwa upande wa Zanzibar ASP nacho kikiwa kimejipanga kamili kuhakikisha Mzanzibari na baadaye Mtanzania anaona nini maana ya kujitawala.
Lakini bahati mbaya baada ya vyama hivyo kuungana na kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikaja Kiswahili cha kwamba 'chama kimeshika hatamu'! Baada ya kunogewa na utamu wa hatamu chama hicho kikaamua kujivua gamba lake na kuyapiga teke yote yaliyokuwa yameasisiwa na TANU na ASP. CCM kikawa kimejipindua chenyewe kutoka chama cha wakulima na wafanyakazi na kuwa chama cha mabwenyenye.
Hilo ni kosa kubwa ambalo chama hicho kililifanya kutokana na kulewa upweke na sasa hivi kinalijutia. Sidhani kama CCM, katika ushindani kama huu kilionao kwa sasa, kingethubutu kuwatelekeza wakulima na wafanyakazi na kuwakumbatia mabwenyeye peke yao. Hilo ni kosa la kiufundi lililotokana na kujiona chenyewe ndicho kila kitu.
Siasa, kama mchezo wa mpira wa miguu, adhabu inatolewa pale kosa lilipofanyikia. Kama ni katika eneo la hatari inatolewa adhabu kali, penalty, ambayo ni kama goli la bure. Sasa hivi CCM inaona kama upinzani umepata penalty ndiyo maana inaanza kuhaha kwa propaganda na vitisho vya kila aina. Kiwewe ilichonacho CCM ni cha kwamba penalty hiyo inaweza ikazaa goli la ushindi kwa upinzani na hivyo kukiondoa chama hicho kwenye utamu wa utawala wa miaka 50.
Sasa hivi chama kikuu cha upinzani, Chadema, kimeshika bango nchi nzima kuonyesha yalikofanyikia makosa ya CCM kuwa ni katika eneo la hatari. Badala ya CCM kuomba radhi na kujirekebisha inakuja na vitisho na madai ya kwamba Chadema inatishia amani. Madai hayo pia yanatolewa na mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete, kwamba Chadema inawatia hofu wananchi. Yaani hofu waliyonayo CCM, hasa viongozi, wanailazimisha iwe hofu ya Watanzania wote!
Ni wananchi gani wenye kuwa na hofu na Chadema halafu wajitokeze kwa wingi tunaoushuhudia kuwalaki na kuwasikiliza viongozi wa Chadema? Tena ikumbukwe kwamba mikutano ya Chadema haina burdani, usafiri wa bure wala posho kama vinavyotolewa nyakati fulanifulani kwenye mikutano ya CCM. Eti wananchi wana hofu! Hofu ya nini?
Uwezekano wa kuvunjika kwa amani kutokana na Chadema kuendelea kuwaelewesha wananchi musitakabali wa kisiasa katika nchi yao, unaweza ukaletwa na hofu waliyonayo CCM, na si hofu ya wananchi. CCM wanaelewa makosa yao ndiyo maana wanakuwa wepesi kutaharuki wakiwa wanaelewa hukumu inayoweza kutolewa dhidi yao. Kwahiyo hofu ni lazima wawe nayo, ni hofu ya kunyangÕanywa tonge mdomoni na wala siyo hofu ya kuvunjika kwa amani.
Lakini iwapo CCM wangekuwa na elimu ya uraia ya kutosha, wakielewa kwamba kila chama cha siasa kilichosajiliwa nchini kinayo haki ya kutawala, wasingekuwa na hofu ila wangejipanga kukabiliana na changamoto za Chadema bila woga wala mizengwe, na kupitia njia hiyo wangekuwa wameepusha kile kinachodaiwa kwamba kinaweza kutokea, umwagaji wa damu. Lakini kwa mtindo huu wa kutojiamini unaosindikizwa na woga uliopita mipaka, sielewi kama CCM watatunusuru. Ila nina imani kwamba katika hali yoyote iwayo ukweli utasimama.