Dalili za kanisa la Afrika kuelekea kwenye kujiua

MTAZAMO

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
19,643
33,432
DALILI ZA KANISA LA AFRIKA KUELEKEA KWENYE KUJIUA.

Pd.TITUS AMIGU

Naona namna za dalili za kujitundika na kujininginiza. Kwa nini naona hivyo? Ni kwa sababu makosa yale mawili ya mwanzo ya watu wa Ulaya na Marekani tunayafanya yote; kosa linalotindikia kidogo ni lile la tatu. Lakini pamoja na hayo, makosa tunayoyafanya Afrika ni mengi zaidi ya hayo mawili waliyofanya wenzetu Ulaya na Marekani.

Najieleza. Kosa la kwanza la watu wa Ulaya na Marekani sasa ndilo limepamba moto, tunalifanya kwa bidii , tena bidii kubwa kabisa: kujenga “makanisa majengo” badala ya “kanisa watu”. Kosa la pili ndilo hilo tena, tunahangaika mno na mali, miradi, vitegauchumi eti ili tujitegemee kiasi hata waamini wengine kuona Kanisa halina maana kwa jinsi linavyowadai michango kila mahali na kila wakati. Kwenye jumuiya ndogo ndogo, wakipiga magoti kusali, wakiinuka tu, michango na harambee. Wakiingia kanisani mahubiri na ibada fupi kama “mkia wa mbuzi”, lakini mambo ya matangazo na harambee masaa kwa masaa.

Mahali pengine na wengine wanakasirikiana na kupeana adhabu za kunyimana sakramenti kwa kosa la kutotoa michango, au zaka na sadaka.

Lakini pamoja na makosa haya ni makosa yafuatayo manne, mosi, maaskofu na mapadre kuwaachia peke yao makatekista, pengine wasioandaliwa vizuri, kazi eti ndio wajenge msingi wa imani, mintarafu mafundisho ya ubatizo, kipaimara na ndoa.

Makatekista kwa kadiri ya uwezo wao wanafanya kitu lakini kwa kuwa wanachojenga huwa hafifu, Wakristo wanatindikiwa ubora na hivyo wakija watu wa makanisa mengine wanawafagia kana kwamba walikuwa vipepeo tu. Huwezi kujenga nyumba imara juu ya msingi dhaifu! Eti hapo tunashangaa kwa nini waamini wetu wanakuwa, ashkum si matusi, “changudoa wa imani” wakihama kutoka hapa na kwenda pale na hata mwishowe kugeuka maadui wetu wakali!

Pili, ni kuachilia vyama au vikundi vinavyowatoa watu kwenye imani ya kweli na kuwarudisha watu kwenye imani za jadi au kuwahamishia watu kwenye imani za dini zingine au makanisa mengine. Tunaachilia watu watufundishie watu wetu hofu za uchawi, mizimu, mapepo, majini, kufungwa na kufunguliwa, miti ya ukoo, laana, mikosi na kadhalika. Haya hayakupaswa kuwa mada zetu. Tulipaswa kupigia tarumbeta INJILI (HABARI NJEMA YA FURAHA) na mafundisho sahihi ya Kanisa Katoliki.

Eti hatuna habari Baba Mtakatifu Benedikto XVI alivyotuonya kwenye Mausia yake baada ya Sinodi ya Pili ya Afrika, tujitoe kwenye “KUJISAJILI KUWILI”, kwenye Ukristo na kwenye dini za jadi, katika AFRICAE MUNUS 93, mwaka 2009!

Tatu, ni kukazania Kanisa lijali sana mipaka ya nchi kana kwamba si Kanisa la ulimwengu. Kwa namna hii, nchi mbalimbali zinazidi kujitenga na zingine, hata matokeo yake tunakuwa na labda Kanisa la Kenya tu, ambapo mtu wa Uganda anaitwa na kutengwa kama mgeni; Kanisa la Tanzania tu, ambapo mtu wa Malawi anaitwa na kutengwa kama mgeni; Kanisa la Afrika ya Kusini tu, ambapo mtu wa Msumbiji anaitwa na kutengwa kama mgeni; Kanisa la Kameruni tu, ambapo mtu wa Demokrasia ya Kongo anaitwa na kutengwa kama mgeni; Kanisa la Nigeria tu, ambapo mtu wa Ghana anaitwa na kutengwa kama mgeni na kadhalika.

Matokeo ya jitihada hizi hasi, mtu wa nchi moja, kwa mfano, hawezi kuwa Askofu wa Kanisa Katoliki katika nchi nyingine hapa hapa duniani au hapa hapa Afrika. Inasikitisha, Kanisa linapotea kutoka maana ya neno “katoliki”, yaani “ya ulimwengu wote”.

Lakini vibaya zaidi ni kwamba baada ya ugonjwa huo kuanza, ubaguzi umeshaanza kuchanulia pahala pengine pia, sasa unaikamata mipaka ya makabila kiasi kwamba Mnubi hawezi kuwa Askofu kwa Wadinka; Muigbo hawezi kuwa Askofu kwa Wayoruba; Mshona hawezi kuwa Askofu kwa Wandebele; Mjaluo hawezi kuwa Askofu kwa Wakamba, labda Mmakua hawezi kuwa Askofu kwa Wasukuma na Mmakonde hawezi kuwa Askofu kwa Wanyakyusa.

Lakini maana yake nini mambo haya yote? Maana yake ni moja tu: ule mwendo wa kuwa na Kanisa moja, takatifu, Katoliki na la mitume, unavunjika na ule mwendo wa Kanisa kuwa juu ya mipaka ya nchi na makabila (Efe 2:14-18) unamong’onyoka. Mimi nasema hiyo ni dalili mojawapo ya kujimaliza kwetu, kwani “Bandubandu humaliza gogo.” Si hivyo tu, Seminari nyingi, ndogo kwa kubwa, zinaanza kuwa za majimbo au za maeneo maalumu tu.

Katika mstari huu wa kuharibika mambo, wala haitakuwa ajabu konventi na monasteri nazo zikishambuliwa na virusi sawia. Kifupi, tunanyemelewa na hatari ya kuirefusha mizizi ya ubaguzi kikanda, kikabila, kijimbo, kiparokia na kadhalika. Hivi Kanisa la ulimwengu litakuwa linaimba wimbo wa kuwa Kanisa moja, takatifu, Katoliki na la mitume, wakati ukweli wake ni kinyume chake Kanisa linageuka kuwa la kitaifa, kikabila au kiparokia na kadhalika.

Zaidi ya hayo, Kanisa la ulimwengu litakuwa linajitangaza kusimamia kanuni moja ya imani, sakramenti sawa saba na teolojia iliyo juu ya mipaka yote, wakati wale wanaotakiwa washike vitu hivyo wameshajikatakata vifungu kama dagaa waliofiwa na mama zao. Lakini ukweli ni kwamba makanisa yakiwa makanisa ya nchi au ya makabila yatakwisha nguvu kama yanavyoendelea kiudhaifu makanisa ya Armenia, makanisa ya Urusi na kadhalika. Kwa nini basi hatusomi historia? Lakini, ndugu zanguni, historia ni mwalimu mkuu na ishara za nyakati si mapambo ya kwenye khanga!

Hivi hapa hata jirani zetu Waislamu hawezi kutufundisha kitu? Hatuwezi kuwasoma? Wenzetu, kutokana na dhana yao ya kuwa na UMMA MKUBWA, siku ya kiyama, hawathubutu kujigawagawa na kuchoreana mipaka ya kiimani kwa vigezo vya utaifa, rangi wala makabila. Hija ya Makka na Madina na uvaaji wa shuka zao mbili (ihram) wakati wa hija huwafanya wajisikie daima kuwa na Uislamu mmoja na wote kuwa ndugu. Ndiyo kisa ukikosana na Waislamu mahali fulani wote hujisikia umewakosea. Lakini kwetu kila mtu “kalumanyile”.

Kosa la nne na la mwisho katika mada hii ni waamini kujiweka nyuma katika kujifunza na kujua mafundisho ya Kanisa. Si waamini haba wasiofanya juhudi za kujisomea Biblia na mafundisho msingi ya Kanisa wakijiliwaza tu kwamba siyo wajibu wao namba moja isipokuwa kazi hiyo wenyewe ni makleri (maaskofu, mapadre na mashemasi) na watawa. Hii ni hatari nyororo itakayoliangamiza Kanisa na mwisho kuungamiza pakubwa Ukristo.

Hata wazazi huweza wasifanye lolote mintarafu kuwafundisha watoto wao imani nyumbani mwao, wakilalia mlango wazi kwamba watafundishwa wenyewe wakati wa mafundisho ya komunio ya kwanza au kipaimara. Wanasahau kuwakunja samaki wangali wabichi. Tuseme wengine hufurahia tu jina la kwamba familia ni kanisa la awali, wakati wanazembea kabisa wajibu unaoendana na jina hilo. Kujifunza na kujua mambo ya imani yetu si kazi ya makleri na watawa peke yao.

Kila mtu lazima ajifunze na aijue imani ya Kanisa Katoliki ili naye afanye mahali pake na wajibu wake wa kuikiri, kuiungama, kuipenda, kuitetea, kuilinda, kujivunia, kuistawisha na kuieneza.

Ili yasitupate yanayolipata Kanisa la Ulaya na Marekani, ilitupasa kupigiana sana kelele siku hizi kusudi tudumu kama Wakristo hai (2Tim 4:1-5). Kila Mkristo hai huonesha alama nne. Mosi, husali sala za jumuiya na binafsi. Pili, hupokea masakramenti ya Kanisa.

Tatu, hutimiza wajibu wake kwa Kanisa, kwa mfano, kulipa zaka na michango mingine. Na nne huwa na upendo kwa Mungu na jirani kwa maneno, kwa mawazo, kwa matendo na kwa kutimiza wajibu. Lakini ukweli wa kuuma ni kwamba mahali pengi waamini wanaogelea kwenye matatizo manne: mosi, kuishi katika uchumba sugu; pili, kubatizwa lakini kutokusali (wala kupokea masakramenti); tatu, kusali lakini kutotoa michango na nne, kutoa michango lakini kutokusali.

Kama makosa niliyoeleza katika makala haya hayatathibitiwi, sasa ndiyo tuna mifumo hasi inayotuelekeza kwenye kujiua. Dalili hizo si njema asilani. Ole wetu Kanisa tukijifikisha hapo! Labda hayo tunayafanya kwa sababu “tumelala nusu”.

Lakini kama hayo tunayafanya kwa akili na utashi wetu timamu basi, “MWANA KULITAFUTA, MWANA KULIPATA”.

Mzee wenu Pd. Titus Amigu.
 
Pamoja Pd Amigu amegusia imani yake lakini lipo kubwa la kujifunza kwa ujumla na imani tofauti. Usipojifunza hili leo, ipo siku tutamuelewa huyu mzee
 
Kanisa Katiliki Ulaya linaendeshwa na wahamiaji. Kama mleta mada alivyosema, Katoliki maana yake ni dunia nzima. Kanisa Katoliki halikosi waumini kutoka Latin America, Afrika Magharibi, Philippines, nk.

Kanisa lililo na hatari kubwa ya kupotea Ulaya ni Church of England. Majengo mengi ya kanisa hili huuzwa kwa developers na mara nyingine kugeuzwa misikiti.

Mapadri wengi Ulaya huwa wanatoka Nigeria na Philippines. Nigeria jamii ya Igbo wengi ni Wakatoliki.

Ni muhimu kufuta misingi ya mwanzo ya kueneza dini, hasa kujitoa. Katika jumuia wale wenye uwezo kidogo mkiandaa kifungua kinywa kwa wanajumuia ni sadaka. Kuna wasio na uwezo wa kumudu milo mitatu kwa siku.
 
Kanisa Katiliki Ulaya linaendeshwa na wahamiaji. Kama mleta mada alivyosema, Katoliki maana yake ni dunia nzima. Kanisa Katoliki halikosi waumini kutoka Latin America, Afrika Magharibi, Philippines, nk...
Hata Katoliki mkuu, mfano bora ni huku Afrika. Nitajie Askofu asiye Mtanzania aliyepo Tanzania! Ile mantiki ya ulimwengu inafutika! Si jambo la kupuuza!
 
Hata Katoliki mkuu, mfano bora ni huku Afrika. Nitajie Askofu asiye Mtanzania aliyepo Tanzania! Ile mantiki ya ulimwengu inafutika! Si jambo la kupuuza!
Kanisa Katoliki la awali si kama la sasa hivi. Zamani kanisa Katoliki lilijenga shule walizosoma watoto wa masikini na hospitali zilizotibu wasio na uwezo.

Charity imepingua sana, sasa hivi ada katika shule za Katoliki ujipange na hospitali kadhalika. Sasa hivi ni vigumu kuwapata waumini wapya. Charity ilichangia kuleta waumini. Ndiyo maana nikasema kwenye jumuia walio na uwezo kidogo siku ya sala watoe na chakula. Hata kusaidia ada ya watoto wasiojiweza.
 
Kanisa Katoliki la awali si kama la sasa hivi. Zamani kanisa Katoliki lilijenga shule walizosoma watoto wa masikini na hospitali zilizotibu wasio na uwezo.

Charity imepingua sana, sasa hivi ada katika shule za Katoliki ujipange na hospitali kadhalika. Sasa hivi ni vigumu kuwapata waumini wapya. Charity ilichangia kuleta waumini. Ndiyo maana nikasema kwenye jumuia walio na uwezo kidogo siku ya sala watoe na chakula. Hata kusaidia ada ya watoto wasiojiweza.
Yaani suala la mashule ni balaa.
 
Dini za wakoloni. Na huyo mwandishi anaendelea kusambaza dini za kikoloni. Atuambie ameshawahi kusaidia watanzania wangapi? Wapi? Amewajengea nyumba? Au na yeye anapiga debe. Apambane na hali yake.
 
Dini za wakoloni. Na huyo mwandishi anaendelea kusambaza dini za kikoloni. Atuambie ameshawahi kusaidia watanzania wangapi? Wapi? Amewajengea nyumba? Au na yeye anapiga debe. Apambane na hali yake.
We mwnyw na huyo padre hamna utofauti
Kasumba za kikoloni ,ungekuwa na uafrika hta jina lako lingesomeka hivyo.
 
We mwnyw na huyo padre hamna utofauti
Kasumba za kikoloni ,ungekuwa na uafrika hta jina lako lingesomeka hivyo.
Hilo nilipewa nikiwa mdogo. Wakoloni waliktumia njia ya kutubadilisha majina yetu ya asili ambayo yana nguvu za asili. Mimi niko mbioni kubadilisha. Asante kwa kuliona hilo.
 
Dini za wakoloni. Na huyo mwandishi anaendelea kusambaza dini za kikoloni. Atuambie ameshawahi kusaidia watanzania wangapi? Wapi? Amewajengea nyumba? Au na yeye anapiga debe. Apambane na hali yake.

"Dini" inayokuwa kuliko dini zote ni Dataism, ambapo wenye imani ya Ukristo, Islamu, Hindu, Buddha, Judah n.k Sasa majibu yao matatizo yao waumini wa imani hizo zenye chimbuko za Mashariki ya Kati, Ulaya , Asia badala ya kupata toka kwa Mchungaji, Pastor, Padri, Imamu, Ustadh, Guru/ Asacharya, Bhikkhu, Rabbi n.k wote wanakimbilia mawinguni Intaneti ,Clouds, Google, Amazon n.k kwa Mungu Mpya Dataism kupata majibu.

Kubwa zaidi huyu Mungu wa dini Mpya ya Dataism ukimuuliza kifafa kinasababishwa na nini hata sema kuwa ni pepo wachafu, maruhani au mizimu ndiyo inasababisha kifafa. Mungu huyu mpya wa Dataism atakuambia kwa uhakika kuwa ni matatizo ktk ubongo / neurology ndipo chimbuko la kifafa na kukupatia jibu kuwa operation au dawa za kumeza ndiyo mtatuzi wa kuponyesha kifafa au kukidhibiti kifafa na siyo sala, maombi, mafuta ya upako, kuchoma ubani n.k ndiyo jibu la kukabiliana na tatizo la kifafa.

Hata wenye mamlaka na nguvu duniani kama watawala, wafalme , marais hawamtegemei tena kama zamani Mungu kuwaweka madarakani, wamewekeza kwa Mungu Mpya wa Dataism ktk kompyuta, intaneti, clouds / mawingu, tafiti mitandaoni n.k kuhalalisha kuchaguliwa kwao kwa kura au kubaki madarakani. Kihistoria wenye Mamlaka na Nguvu kama wafalme, marais, majemedari wa kivita ndiyo walisaidia kusambaza dini za Kikristo, Islamu, Buddha, Hindu n.k lakini sasa majemedari wa kivita wanashinda mapambano ktk uwanja wa kivita kutumia Dataism yaani muunganiko wa binadamu na teknolojia (bioteknolojia) Homo Deus. Vifaa kama drones, radar, vifaru vya kisasa, makombora ni mfano mzuri wa Human God Homo Deus Mungu mpya wa "Mawinguni / Clouds". Vyombo vya media navyo havijabaki nyuma kueneza ushawishi kutumia "mawingu" kwa kutaja watu na vyombo vyenye ushawishi vinavyotumia nguvu ya Dataism kupitia Mungu teknolojia.

Mungu huyu wa Dataism naye makao yake mawinguni /clouds na ana majibu ya matatizo yako yote iwe maradhi, mahusiano , kukupa maono, "kukusomea nyota" kupitia data au formular nyingi zenye uthibitisho wa majibu yako. Viongozi wa makanisa , misikiti , mahekalu kupitia vyao vitabu vitakatifu wanazidi kukosa majibu kwa maswali mengi waumini wao wanaoyauliza.

Kukosekana majibu ya kuridhisha kwa "waumini" ndiyo kifo kwa Imani hizi za waendao makanisani, misikitini, mahekaluni n.k

Vitabu vitakatifu vya bibilia, Quran, torati n.k ndiyo vilikuwa na majibu mengi kuhusu kujiepusha na magonjwa ambukizi n.k kwa kifupi ndiyo vilikuwa vitabu kimbilio vya watu wa kitabu na wanazuoni kwa karne nyingi.

Kuibuka maktaba na sasa intaneti / Google walimwengu hawategemei tena ilmu wala elimu kutoka vyanzo vya kiimani vya Bibilia , Quran , Torati n.k sasa Mungu wa dini ya Dataism kupitia intaneti, Google, Amazon, Clouds, mitandao ya kijamii ana taarifa nyingi za elimu, sayansi, teknolojia n.k kupita vitabu vitakatifu vya zamani vilivyotumika "kutujuza" visivyofahamika kwa kutumia imani tu siyo utafiti na sayansi yenye majibu pasipo shaka.

Zamani tukisoma historia tunakutana na viongozi wenye mamlaka na ushawishi mkubwa ktk dini za Kikristo, Kiislamu, Hindu, Buddha, Yahudi wakiongoza harakati za kuchoma vitabu vilivyotishia imani zao vilivyokuwa na elimu mpya au majubu ya kuhusu jiografia, maradhi, filosofia, siasa n.k Zama hizo haziwezi tena kutokea kwani kila kitu kipo juu Mawinguni na watu wana uwezo wa kuvisoma kupitia saa ya mkononi, simu janja, kompyuta mpakato n.k mahali popote bila kusomewa na kuhani au msomi wa imani za "dini tulizozoea " kutoka ktk majengo ya kanisa, msikiti, hekalu au mhadhara.

C.C MTAZAMO , Pd. Titus Amigu.
Historian Yuval Noah Harari became an international sensation when he argued in his best-selling book Sapiens that humans conquered the world through our ability to believe in collective myths about gods, money and freedom. In this excerpt, Harari discusses the authoritative role of big data and algorithms.
 
Kanisa Katoliki la awali si kama la sasa hivi. Zamani kanisa Katoliki lilijenga shule walizosoma watoto wa masikini na hospitali zilizotibu wasio na uwezo.

Charity imepingua sana, sasa hivi ada katika shule za Katoliki ujipange na hospitali kadhalika. Sasa hivi ni vigumu kuwapata waumini wapya. Charity ilichangia kuleta waumini. Ndiyo maana nikasema kwenye jumuia walio na uwezo kidogo siku ya sala watoe na chakula. Hata kusaidia ada ya watoto wasiojiweza.
Umenena vyema. Tunachangia ujenzi wa hayo mashule ama kabla hayajajengwa au kwenye ada wakati mtoto anapoanza Kidato cha kwanza au cha tano. Kimbembe kipo kwenye ada. Sekondari si chini ya milioni 2. High School tayarisha milioni 4.5.
 

Dataism: The new religion​


Religious ideas have evolved through the ages. Human beings have worshiped the sun and the stars, God, and humanism. The next religion is dataism.
Source : Allen Johnson

Dataism – the 21st Century Religion​

Mayank Lau December 2, 2018 No Commentson Dataism – the 21st Century Religion

Today the universe’s pulse is data flow; the value of humans or an enterprise is assessed by its ability to contribute to data processing and reaping fruits out of it. It is believed that Dataism came into existence with the amalgamation of Charles Darwin’s Origin of Species and Alan Turing’s Turing Machine. It puts both together, claiming mathematical rules are applicable to both bio-chemical and electronic algorithms. As per the concept of Dataism, stock exchange data, flu virus, fifth symphony and genetic pool are patterns which can be analysed with similar tools and techniques. The idea seems as an eccentric far-flung notion, but it has permeated significantly into Homo sapiens lives. This is ground breaking, providing all experts a standard language, building bridges contrary to rifts and opportunity to extract insights spanning across various domain frontiers.
As per the teachings and rituals of Dataism, Homo sapiens experiences are not sacrosanct and we are not an apex of creation, rather humans have emerged as a means to create internet of all things, which will propagate from earth to the complete galaxy and may be universe. If this happens, the scale to which data will be processed is expected to be cosmic, similar to creating God like system. This system is expected to be omnipresent and may control everything, and Homo sapiens’ merger with it is inevitable. It is a reminiscent of a typical traditional religion.
dataism-300x250.jpg
If it will emerge as a religion, what will be its commandments? (I) Maximising dataflow usage by Dataist with increased connections of medias, generating and consuming cosmic scale of information (II) To build linkages of systems with everything, with a single motto that does not leave anything which is not connected with the great web of life; it would be a sin to limit the dataflow (III) Providing freedom to information and many more, left to the imaginations of readers.
The revolution of data resulting in dataism may take a few decades, may be a century. If we go back in history, humans kept on believing in God, debating on ‘value of humans’ as sacred entity created by God for divine purposes. Few centuries later, it was mentioned that humans are sacred but without Gods. Today followers of dataism are trying to preach, internet of all things is sacred, as created by humans only. Eventually internet of all things may become sacred without human existence or dependence on them. This will be termed as a shift from homo-centric world to a data centric universe. Will it be another philosophical revolution, rather it may emerge as a pragmatic revolution. The core belief would be ‘organisms are algorithms’.
What is the origin of these algorithms? This is the mystery of Dataism, as according to some religions, humans are unable to understand God’s plan. Similarly, we cannot fathom the master algorithm of dataism. As of now, algorithms are developed by humans in team and each one knows its seed only, the master algorithm which will be the God of dataism may initially be designed by humans, than taking the course where no humans have ventured so far and no one will be able to follow.
No one can predict the future, as today’s technology is not deterministic, rise of AI and biotechnology is expected to transform the world but not with a single deterministic outcome. Hence, Dataism as a probable scenario, as outlined above should be considered as a possibility rather than a prophecy. Nobody knows which forces will dominate in 2050 or 2100, a truly exciting time ahead for Homo sapiens.
This blog is an inspiration from the author Yuval Noah Harari book ‘Homodeus’.
Dataism – the 21st Century Religion – Data Security Council of India (DSCI) Blog
 
Back
Top Bottom