babykailama
JF-Expert Member
- Mar 5, 2012
- 251
- 243
DAKIKA MOJA YA UKIMYA KUTOA HESHIMA:A S-key:
Chukua dakika moja, kaa kimya, weka pembeni kazi uliyotumwa /kujituma hapa JF, sahau msukumo wa itikadi yako ya sasa ya Chadema , CCM , CUF, NCCR au za vyama vinginevyo, na pia hata upendeleo wa imani ya Dini yako, kuheshimu haya maamuzi magumu yanayotakiwa kufanywa ili kuleta ushindi wa kulikomboa Taifa letu muda si mrefu ujao.
Yeyote ktk makundi mawili (A au B), atakaye anza kutekeleza kwa vitendo yanayopendekezwa hapa ndiye atatuongoza kufikia ushindi . Vinginevyo hakuna cha threads za kupasua vichwa toka JF, wala cha Migongano ya Fikra toka kwa Mwanakijiji wala Operation Sangara wala Kauli Mbiu ya Kujivua Gamba wala maandamano ya hapa na pale yaliyopenya kati mwa chujio la Taarifa za ki-Intelijensia yatakayotutoa tulipo!
Mambo yataendelea kuwa yalivyo sasa kwa muda mrefu sana na tukiwa na bahati kizazi hiki kitashihudia Viongozi wa Chama Tawala kuwahurumia Chama kitakachokuwa kinawafuatia kwa karibu katika kura kujilazimisha kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa au ya Mseto ambayo si lazima iwe na Viongozi makini bali tu ya kimpito aka Funika Kombe ya kufurahisha wachache na kuendeleza matakwa ya wachache kama huamini rejea mahusiano ya kikazi na uhalisia wa utendaji kati ya Mugabe & Tsvangirai na kati ya Kibaki & Odinga.
Pazeni sauti za ujumbe huu katika Mikutano Mikuu ya vyama vyenu vya siasa na Asasi zenu, sambazeni mbegu hii katika vilima, mabonde na kwenye uwanda katika kona zote za nchi.:humble:
Shukrani kwa heshima hii, mwaweza endelea na kazi zenu.:wave:
Chukua dakika moja, kaa kimya, weka pembeni kazi uliyotumwa /kujituma hapa JF, sahau msukumo wa itikadi yako ya sasa ya Chadema , CCM , CUF, NCCR au za vyama vinginevyo, na pia hata upendeleo wa imani ya Dini yako, kuheshimu haya maamuzi magumu yanayotakiwa kufanywa ili kuleta ushindi wa kulikomboa Taifa letu muda si mrefu ujao.
- Kama ushindi huu utaongozwa na Vyama Visivyotawala (siviiti vya Upinzani):
- Kama ushindi huu utaongozwa na Chama Tawala (CCM):
- Mazingira ya kufikia ushindi huu ni kuhakikisha kuwa kuna Tume ya Uchaguzi Huru (not on its ID but on its existence and operations).
Yeyote ktk makundi mawili (A au B), atakaye anza kutekeleza kwa vitendo yanayopendekezwa hapa ndiye atatuongoza kufikia ushindi . Vinginevyo hakuna cha threads za kupasua vichwa toka JF, wala cha Migongano ya Fikra toka kwa Mwanakijiji wala Operation Sangara wala Kauli Mbiu ya Kujivua Gamba wala maandamano ya hapa na pale yaliyopenya kati mwa chujio la Taarifa za ki-Intelijensia yatakayotutoa tulipo!
Mambo yataendelea kuwa yalivyo sasa kwa muda mrefu sana na tukiwa na bahati kizazi hiki kitashihudia Viongozi wa Chama Tawala kuwahurumia Chama kitakachokuwa kinawafuatia kwa karibu katika kura kujilazimisha kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa au ya Mseto ambayo si lazima iwe na Viongozi makini bali tu ya kimpito aka Funika Kombe ya kufurahisha wachache na kuendeleza matakwa ya wachache kama huamini rejea mahusiano ya kikazi na uhalisia wa utendaji kati ya Mugabe & Tsvangirai na kati ya Kibaki & Odinga.
Pazeni sauti za ujumbe huu katika Mikutano Mikuu ya vyama vyenu vya siasa na Asasi zenu, sambazeni mbegu hii katika vilima, mabonde na kwenye uwanda katika kona zote za nchi.:humble:
Shukrani kwa heshima hii, mwaweza endelea na kazi zenu.:wave: