Dakika 30 za kifo cha rais John F Kennedy.

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,443
,
bfc478b6348514378d6897f5848e94b8.jpg
 
,
bfc478b6348514378d6897f5848e94b8.jpg

Risasi ya pili kumpata rais (ambayo ilikuwa ni risasi ya tatu kupigwa) ilimpata kichwani upande wa juu kulia.

Risasi hii ilifumua kabisa eneo hilo la kichwa na kusababisha sehemu ya ubongo wa mbele kumwagika.

Damu nyingine ikaruka nyuma ya gari kwenye 'trunk' na nyingine kutua mpaka kwenye mkono wa kushoto wa afisa wa Secret Services aliyekuwa anaendesha gari ya wanausalama waliokuwa gari ya nyuma ya Rais.

Ndani ya sekunde mbili baada ya mumewe kufumuliwa na risasi kichwani, First Lady Jacqueline Kennedy akaruka kutoka kwenye siti yake na kuanza kuparamia nyuma ya gari kwenye trunk.
Tofauti na wengi wanavyodhani kwamba alikuwa anajaribu kukimbia kuokoa maisha yake, ila ukweli ni kwamba alikuwa anaokota kipande cha mfupa wa fuvu la kichwa kilichodondoka kwenye nyuma ya gari kwenye trunk baada ya mumewe kufumuliwa kichwa na risasi. Baada ya kukichukua haraka haraka akarejea kwenye siti yake. (Tazama tena kipande cha video nilichokiweka kwa makini).
ed774439da8ff403342f1b42a1e757ad.jpg

Sekunde hii hii ambayo First Lady alikuwa anaparamia gari kwenye trunk, katika gari ya nyuma (follow up car), Special Agent Clint Hill ambaye alikuwa ananing'inia kwenye mlango wa mbele kushoto akaruka na kuanza kuikimbilia gari iliyombeba rais na first lady.
Dereva wa gari la rais alikuwa ameongeza mwendo baada ya mushkeli kutokea na dhahiri kuonekana kwamba rais yuko hatarini.
Hivyo basi ilimbidi Clint Hill kujaribu kuparamia gari mara kadhaa mpaka alipofanikiwa kuidandia gari na mara moja kuwafunika rais na first lady akiwakinga kwa kutukia mwili wake kama ngao.

Baada ya Agent Clint Hill kuwakinga Rais na mkewe dhidi ya shambulio lingine lolote la risasi kuwafikia, gari ya rais liliendeshwa kwa kasi kubwa likifuatiwa na pikipiki za pembeni na ile follow up car ya maafisa usalama.

Wakati haya yote yanatokea zilikuwa zimebaki takribani dakika tano pekee kufika walikokuwa wanaelekea, Trade Mart.
Kwahiyo baada ya gari iliyombeba rais kuanza kuendeshwa kwa kasi, takribani saa 6 na dakika 35 walipita eneo la Trade Mart na kuelekea moja kwa moja hospitali ya *Parkland Memorial Hospital* ambako waliwasili majira ya saa 6 na dakika 38 na kupokelewa kisha Rais Kennedy alipelekwa moja kwa moja chumba cha dharura.

Licha ya watu wa usalama kujitahidi sana kuratibu taaarifa za kilichotokea zisivuje kabla ya taarifa rasmi ya serikali, lakini majira ya saa 6 na dakika 40 kituo cha televisheni cha CBS kikakatisha Igizo lililokuwa linaonyeshwa kwenye televisheni yao na kutoa "Breaking News" kuwa msafara wa Rais umeshambuliwa huko Dallas.

Baadae kama muda wa saa 6 na dakika 45, Dan Rather mwandishi wa habari wa kituo cha CBS alifanya mawasiliano kwa siri sana na daktari anayemfahamu hapo hospitalini na kuvujishiwa taarifa kuwa kuna uwezekano mkubwa Rais Kennedy hayuko hai.

Ifahamike kwamba maafisa wa Secret Services waliwaleta hapa viongozi wengine wote wakuu waliopo kwenye msafara, yaani First Lady Jacqueline Kennedy, Makamu wa Rais Johnson, Mkewe Lady Bird na Gavana Connally ambaye alikuwa chumba cha wagonjwa mahututi.

Ilipofika saa 7 kamili madaktari wakatoa taarifa yao kwa viongozi wa serikali na wanausalama waliokuwepo hapo kwamba, licha ya kutumia ujuzi wao wote na maarifa yao yote, wameshindwa kuokoa maisha ya Rais JF Kennedy, kwamba Rais Kennedy amefariki.!!

Huko mtaani habari zilikuwa zinaenea kwa kasi kama moto wa kifuu, kuwa Rais Kennedy amefariki, hivyo kwa busara watu wa usalama wakashauri kuwa itolewe taarifa rasmi kuhusu kifo cha Rais Kennedy ili kuepusha mkanganyiko na taharuki iliyopo mtaani.

Makamu wa Rais Johnson akakubali hilo lakini akaamuru taarifa hiyo itolewe kwa umma mara baada ya yeye kuondoka hapo hospitali kwa usababu ya usalama wake, kwamba hataki yeyote ajue kuwa yuko hapo hospitali kwa kuwa kwa vile Rais ameuwawa tayari yawezekana yeye kama Makamu wa Rais akawa ni "next target"!
Saa 7 na dakika 26 Makamu wa Rais Lyndon B. Johnson akaondolewa kwa siri kubwa kutoka Parkland Memorial Hospital na kupelekwa uwanja wa ndege wa Love Field ambako Airforce One ilikuwa imepaki.

Baada ya Makamu wa Rais kuondoka tu, dakika saba baadae yaani saa 7 na dakika 33 Katibu Msaidizi wa Mawasiliano Ikulu Bw. Malcolm Kilduff ya Marekani akafanya mkutano na waandishi wa habari hapo hapo hospitali na kuutangazia rasmi ulimwengu kuwa Rais JF Kennedy amefariki baada ya kudunguliwa na risasi na mtu asiyejulikana.
Bw. Kilduff hakujibu swali lolote la waandishi wala kutoa taarifa nyingine yoyote. Alipotoa taarifa hii tu akaumaliza mkutano na wanahabari.

Baada ya waandishi wote kuondoka na kubakia watu wa serikali pekee na wanausalama ndani ya Hospitali kulitokea kisa ambacho naamini wengi hawajawahi kukisikia.

Ni kwamba, katika sheria za Marekani kipindi hicho zilikuwa zinaelekeza kwamba, endapo Rais atafariki akiwa jimbo Fulani.. Mwili wake unakuwa chini ya mamlaka ya jimbo na sio serikali kuu.

Sasa, yule bwana swahiba wa Rais Kennedy na Katibu wake wa teuzi Kenneth O'Donnell, yule ambaye alimuamuru Afisa wa Secret Services, Agent Kellerman kuwa gari la Rais liondolewe paa na kubaki 'kibnda wazi', akatoa tena maelekezo kwa wanausalama wauondoe mwili wa Rais Kennedy kutoka hapo hospitalini na kuipeleka uwanja wa ndege wa Love Field na kuipakia katika Air Force One.

Lakini madaktari walikataa mwili huo kuondolewa hospitalini bila kufanyiwa 'Autopsy' (uchunguzi wa kina wa kidaktari kuhusu chanzo cha kifo) ukizibgatia kuwa Rais Kennedy amekufa kwa mauaji ya kukusidiwa.

Bw. Kenneth O'Donnell akasisitiza kuwa hakuna muda wa kutosha kufanya Autopsy kwani Air Force One inatakiwa iondoke mara moja kuwarudisha Makamu wa Rais na First Lady Washington kwa sababu za kiusalama na First Lady amekataa kuondoka bila mwili wa mumewe.

Madaktari wakashilia msimamo wao kuwa hawawezi kuuachia mwili wa Rais bila kufanyiwa Autopsy. Na kusisitiza wanalolisema wakatumia kifungu cha sheria nilichokitaja hapo juu kuwaeleza kuwa wao (Kenneth na wanausalama) kama watumishi wa serikali kuu hawana mamlaka juu ya mwili wa Rais bali wao (madaktari) kama watumishi wa jimbo la Texas ndio wenye mamlaka juu ya mwili wa Rais.

Mzozo ukawa mkubwa sana mpaka kufikia hatua Kenneth O'Donnell na wanausalama wakataka kuutoa mwili wa Rais Kennedy kwa kutumia nguvu.
Hii ikawalazimu madaktari kuita maafisa wa polisi (watumishi wa jimbo la Texas) kuwasaidia kuwadhibiti Kenneth na wanausalama wa Secret Services.

Madaktari wakatanda mlangoni pamoja na Maafisa wa polisi wakiwa wameshikilia bastola kuwanyooshea Kenneth O'Donnell na wanausalama wa Secret services kuwaamuru waache mwili wa Rais.
Upande wa pili nao Kenneth na wanausalama walikuwa nao wamechomoa bastola kuwanyooshea madaktari na polisi wa jimbo la Texas kuwa wapishe mlangoni.

Wakati mzozo huo unaendelea hospitali ya Parkland Memorial Hospital, huko uwanja wa ndege wa Love Field, ndani ya Air Force One Jaji wa mahakama Kuu, Sarah Hughes alikuwa anamuapisha Makamu wa Rais Lyndon B. Johnson kuwa Rais wa Marekani.

Na huko mitaani wananchi walikuwa wako kwenye sintofahamu kubwa!! Ni nini kimetokea? Nani amemuua Rais? Amewezaje kutekeleza hilo? Sababu gani imemponza Kennedy kuuwawa??

Maswali yalikuwa mengi na magumu pasipo majibu ya dhahiri!!

Itaendelea…

Cc: Mpalestina Mchizi
Ungemalizia tu au mb mzozo shauku yangu kubwa ni kujua sababu za kuuwawa na nani waliratibu zoezi zima la hayo mauwaji
 
,
bfc478b6348514378d6897f5848e94b8.jpg

Risasi ya pili kumpata rais (ambayo ilikuwa ni risasi ya tatu kupigwa) ilimpata kichwani upande wa juu kulia.

Risasi hii ilifumua kabisa eneo hilo la kichwa na kusababisha sehemu ya ubongo wa mbele kumwagika.

Damu nyingine ikaruka nyuma ya gari kwenye 'trunk' na nyingine kutua mpaka kwenye mkono wa kushoto wa afisa wa Secret Services aliyekuwa anaendesha gari ya wanausalama waliokuwa gari ya nyuma ya Rais.

Ndani ya sekunde mbili baada ya mumewe kufumuliwa na risasi kichwani, First Lady Jacqueline Kennedy akaruka kutoka kwenye siti yake na kuanza kuparamia nyuma ya gari kwenye trunk.
Tofauti na wengi wanavyodhani kwamba alikuwa anajaribu kukimbia kuokoa maisha yake, ila ukweli ni kwamba alikuwa anaokota kipande cha mfupa wa fuvu la kichwa kilichodondoka kwenye nyuma ya gari kwenye trunk baada ya mumewe kufumuliwa kichwa na risasi. Baada ya kukichukua haraka haraka akarejea kwenye siti yake. (Tazama tena kipande cha video nilichokiweka kwa makini).
ed774439da8ff403342f1b42a1e757ad.jpg

Sekunde hii hii ambayo First Lady alikuwa anaparamia gari kwenye trunk, katika gari ya nyuma (follow up car), Special Agent Clint Hill ambaye alikuwa ananing'inia kwenye mlango wa mbele kushoto akaruka na kuanza kuikimbilia gari iliyombeba rais na first lady.
Dereva wa gari la rais alikuwa ameongeza mwendo baada ya mushkeli kutokea na dhahiri kuonekana kwamba rais yuko hatarini.
Hivyo basi ilimbidi Clint Hill kujaribu kuparamia gari mara kadhaa mpaka alipofanikiwa kuidandia gari na mara moja kuwafunika rais na first lady akiwakinga kwa kutukia mwili wake kama ngao.

Baada ya Agent Clint Hill kuwakinga Rais na mkewe dhidi ya shambulio lingine lolote la risasi kuwafikia, gari ya rais liliendeshwa kwa kasi kubwa likifuatiwa na pikipiki za pembeni na ile follow up car ya maafisa usalama.

Wakati haya yote yanatokea zilikuwa zimebaki takribani dakika tano pekee kufika walikokuwa wanaelekea, Trade Mart.
Kwahiyo baada ya gari iliyombeba rais kuanza kuendeshwa kwa kasi, takribani saa 6 na dakika 35 walipita eneo la Trade Mart na kuelekea moja kwa moja hospitali ya *Parkland Memorial Hospital* ambako waliwasili majira ya saa 6 na dakika 38 na kupokelewa kisha Rais Kennedy alipelekwa moja kwa moja chumba cha dharura.

Licha ya watu wa usalama kujitahidi sana kuratibu taaarifa za kilichotokea zisivuje kabla ya taarifa rasmi ya serikali, lakini majira ya saa 6 na dakika 40 kituo cha televisheni cha CBS kikakatisha Igizo lililokuwa linaonyeshwa kwenye televisheni yao na kutoa "Breaking News" kuwa msafara wa Rais umeshambuliwa huko Dallas.

Baadae kama muda wa saa 6 na dakika 45, Dan Rather mwandishi wa habari wa kituo cha CBS alifanya mawasiliano kwa siri sana na daktari anayemfahamu hapo hospitalini na kuvujishiwa taarifa kuwa kuna uwezekano mkubwa Rais Kennedy hayuko hai.

Ifahamike kwamba maafisa wa Secret Services waliwaleta hapa viongozi wengine wote wakuu waliopo kwenye msafara, yaani First Lady Jacqueline Kennedy, Makamu wa Rais Johnson, Mkewe Lady Bird na Gavana Connally ambaye alikuwa chumba cha wagonjwa mahututi.

Ilipofika saa 7 kamili madaktari wakatoa taarifa yao kwa viongozi wa serikali na wanausalama waliokuwepo hapo kwamba, licha ya kutumia ujuzi wao wote na maarifa yao yote, wameshindwa kuokoa maisha ya Rais JF Kennedy, kwamba Rais Kennedy amefariki.!!

Huko mtaani habari zilikuwa zinaenea kwa kasi kama moto wa kifuu, kuwa Rais Kennedy amefariki, hivyo kwa busara watu wa usalama wakashauri kuwa itolewe taarifa rasmi kuhusu kifo cha Rais Kennedy ili kuepusha mkanganyiko na taharuki iliyopo mtaani.

Makamu wa Rais Johnson akakubali hilo lakini akaamuru taarifa hiyo itolewe kwa umma mara baada ya yeye kuondoka hapo hospitali kwa usababu ya usalama wake, kwamba hataki yeyote ajue kuwa yuko hapo hospitali kwa kuwa kwa vile Rais ameuwawa tayari yawezekana yeye kama Makamu wa Rais akawa ni "next target"!
Saa 7 na dakika 26 Makamu wa Rais Lyndon B. Johnson akaondolewa kwa siri kubwa kutoka Parkland Memorial Hospital na kupelekwa uwanja wa ndege wa Love Field ambako Airforce One ilikuwa imepaki.

Baada ya Makamu wa Rais kuondoka tu, dakika saba baadae yaani saa 7 na dakika 33 Katibu Msaidizi wa Mawasiliano Ikulu Bw. Malcolm Kilduff ya Marekani akafanya mkutano na waandishi wa habari hapo hapo hospitali na kuutangazia rasmi ulimwengu kuwa Rais JF Kennedy amefariki baada ya kudunguliwa na risasi na mtu asiyejulikana.
Bw. Kilduff hakujibu swali lolote la waandishi wala kutoa taarifa nyingine yoyote. Alipotoa taarifa hii tu akaumaliza mkutano na wanahabari.

Baada ya waandishi wote kuondoka na kubakia watu wa serikali pekee na wanausalama ndani ya Hospitali kulitokea kisa ambacho naamini wengi hawajawahi kukisikia.

Ni kwamba, katika sheria za Marekani kipindi hicho zilikuwa zinaelekeza kwamba, endapo Rais atafariki akiwa jimbo Fulani.. Mwili wake unakuwa chini ya mamlaka ya jimbo na sio serikali kuu.

Sasa, yule bwana swahiba wa Rais Kennedy na Katibu wake wa teuzi Kenneth O'Donnell, yule ambaye alimuamuru Afisa wa Secret Services, Agent Kellerman kuwa gari la Rais liondolewe paa na kubaki 'kibnda wazi', akatoa tena maelekezo kwa wanausalama wauondoe mwili wa Rais Kennedy kutoka hapo hospitalini na kuipeleka uwanja wa ndege wa Love Field na kuipakia katika Air Force One.

Lakini madaktari walikataa mwili huo kuondolewa hospitalini bila kufanyiwa 'Autopsy' (uchunguzi wa kina wa kidaktari kuhusu chanzo cha kifo) ukizibgatia kuwa Rais Kennedy amekufa kwa mauaji ya kukusidiwa.

Bw. Kenneth O'Donnell akasisitiza kuwa hakuna muda wa kutosha kufanya Autopsy kwani Air Force One inatakiwa iondoke mara moja kuwarudisha Makamu wa Rais na First Lady Washington kwa sababu za kiusalama na First Lady amekataa kuondoka bila mwili wa mumewe.

Madaktari wakashilia msimamo wao kuwa hawawezi kuuachia mwili wa Rais bila kufanyiwa Autopsy. Na kusisitiza wanalolisema wakatumia kifungu cha sheria nilichokitaja hapo juu kuwaeleza kuwa wao (Kenneth na wanausalama) kama watumishi wa serikali kuu hawana mamlaka juu ya mwili wa Rais bali wao (madaktari) kama watumishi wa jimbo la Texas ndio wenye mamlaka juu ya mwili wa Rais.

Mzozo ukawa mkubwa sana mpaka kufikia hatua Kenneth O'Donnell na wanausalama wakataka kuutoa mwili wa Rais Kennedy kwa kutumia nguvu.
Hii ikawalazimu madaktari kuita maafisa wa polisi (watumishi wa jimbo la Texas) kuwasaidia kuwadhibiti Kenneth na wanausalama wa Secret Services.

Madaktari wakatanda mlangoni pamoja na Maafisa wa polisi wakiwa wameshikilia bastola kuwanyooshea Kenneth O'Donnell na wanausalama wa Secret services kuwaamuru waache mwili wa Rais.
Upande wa pili nao Kenneth na wanausalama walikuwa nao wamechomoa bastola kuwanyooshea madaktari na polisi wa jimbo la Texas kuwa wapishe mlangoni.

Wakati mzozo huo unaendelea hospitali ya Parkland Memorial Hospital, huko uwanja wa ndege wa Love Field, ndani ya Air Force One Jaji wa mahakama Kuu, Sarah Hughes alikuwa anamuapisha Makamu wa Rais Lyndon B. Johnson kuwa Rais wa Marekani.

Na huko mitaani wananchi walikuwa wako kwenye sintofahamu kubwa!! Ni nini kimetokea? Nani amemuua Rais? Amewezaje kutekeleza hilo? Sababu gani imemponza Kennedy kuuwawa??

Maswali yalikuwa mengi na magumu pasipo majibu ya dhahiri!!

Itaendelea…

Cc: Mpalestina Mchizi
Can't wait mkuu
 
Back
Top Bottom