Jospina
JF-Expert Member
- Apr 19, 2013
- 2,421
- 1,395
Umeishi nyumbani kwenu kwa miaka lukuki, yaani ukiwa na miaka 32 nd'o ukaondoka nyumbani, sio kwamba ukaanza kujitegemea hapana ukaajiriwa na mjomba ukawa unaishi kwake.
Mama nyumbani akapumua kidogo umempunguzia mzigo... Maana ulikuwa unategemea kila kitu kwake
He! Baada ya miaka miwili tena sio miwili kamilikamili badala ya kuanza kumtumia mama matumizi... Mama anapokea ugeni, umejaza mtu mimba huko halafu unamuagiza tu aende kwa mama yako akaishi ye na mtoto....
Sio kwamba umempa pesa ya matumzi.. Hapana umempa nauli tu ya kumfikisha kwa mama yako....
Jamani eeh! Wanasema mtoto hakui kwa mama.... Ehe! We umekaa kwa mama yako miaka 30 halafu mtoto wako hata mwezi hujakaa naye....
Na sio wanaume pekee wapo wasichana wanatega wanajazwa mimba wanalundika watoto kwa mama zao.
Najua mpo wengi... Mniwie radhi iwapo thread hii itawaharibia siku..
@G.I.M..
Mama nyumbani akapumua kidogo umempunguzia mzigo... Maana ulikuwa unategemea kila kitu kwake
He! Baada ya miaka miwili tena sio miwili kamilikamili badala ya kuanza kumtumia mama matumizi... Mama anapokea ugeni, umejaza mtu mimba huko halafu unamuagiza tu aende kwa mama yako akaishi ye na mtoto....
Sio kwamba umempa pesa ya matumzi.. Hapana umempa nauli tu ya kumfikisha kwa mama yako....
Jamani eeh! Wanasema mtoto hakui kwa mama.... Ehe! We umekaa kwa mama yako miaka 30 halafu mtoto wako hata mwezi hujakaa naye....
Na sio wanaume pekee wapo wasichana wanatega wanajazwa mimba wanalundika watoto kwa mama zao.
Najua mpo wengi... Mniwie radhi iwapo thread hii itawaharibia siku..
@G.I.M..