Dah!This mature woman is crazy . . .!

Eiyer

JF-Expert Member
Apr 17, 2011
28,258
20,712
Hawa wanandoa wamekaa pamoja kwenye ndoa kwa miaka 25.

Mume ana umri wa miaka 53 na mke ana miaka 50! Wanaishi maeneo ya Nyamanoro, jijini hapa Mwanza.

Tukio la kusikitisha lililotokea miezi mi 2 iliyopita limeniacha na mshangao pale mzee alipomfumania mkewe nyumbani kwake akila tunda na dreva wao.

Kwa maelezo ya dereva ambae ni jamaa yangu na ndie ameniambia mkasa huu,pia ameniruhusu niuweke hapa, jamaa yangu huyu anadai kuwa chanzo cha kuanza kufanya ngono na mama huyo ni baada ya mama huyo kugundua uhusiano wa dereva huyo na mwanae wa kike ambae ni mwanachuo SAUT.

Ndipo mama alimtisha kumwambia mzee mwenye mji uhusiano huo,jamaa aliogopa kutokana na sifa ya ukatili aliyonayo mzee yule. Ndipo yule mama akamwambia atamtunzia siri kama atakubali kufanya nae pia. Kijana kwa woga alikubali na waliendelea kwa muda mrefu huku pia jamaa akiendeleza na binti.

Siku ya fumanizi, mzee alipowafuma alizimia ndipo jamaa akapata mwanya wa kukimbia na amehama kabisa mkoa.Yule mzee hajamfukuza mkewe lakini hawalali chumba kimoja, na wanashirikiana shughuli zingine kama kawaida!

Ama kweli, Utu uzima dawa . . . . . !!
 
Uandishi kama wa riwaya yawe yalitokea au hayakutokea yanatoa fundisho au kufurahisha..............Wewe utakuwa unaleta visa "live" bado vya moto kabisa, unaonaje hii idea yangu

Tatizo haya matukio nakutana nayo kama ajali tu.Mfano huyu jamaa,kilichofanya aniambie huu mkasa ni baada ya kumuuliza sababu ya kukimbia Mwanza!
 
Tatizo haya matukio nakutana nayo kama ajali tu.Mfano huyu jamaa,kilichofanya aniambie huu mkasa ni baada ya kumuuliza sababu ya kukimbia Mwanza!

Ungekuwa na akili za kichaga tayari ungeshamgongea Invisible au Shigongo kutafuta dili...........lakini kwa sababu wewe ni kama mimi ngosha.............."sagalasagala nkohi"
 
Last edited by a moderator:
Ungekuwa na akili za kichaga tayari ungeshamgongea Invisible au Shigongo kutafuta dili...........lakini kwa sababu wewe ni kama mimi ngosha.............."sagalasagala nkohi"

Suala la biashara ni la wenye matukio.Mimi naweka hapa kwa ruksa yao ili wa kujifunza ajifunze!! . . . .Nahene bhabha . . .!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom