Hayo mengine tusubiri kikwete akujibu, ila hili la TANESCO siwezi nyamaza, bei ya umeme ipo juu hata kabla net Group hawajapewa tenda, yaani tuseme tangu shirika lilipo anzishwa, huwa gharama zingine zinatokana na ukweli kwamba baadhi ya watumiaji hawalipi bili, kama serikali, chama nk. Hili linasababisha wanaolipa walipe zaidi.
sababu ingine ni mikataba mibovu ya tangu enzi, ama waliingia hiyo mikataba kwa makusudi ili wapate takrima, ama waliingia hiyo mikataba kutokana na shinikizo la WAKOLONI (k.v. Benki ya dunia nk.) Hivyo usitegemee tanesco ishushe bei wakati bado inaingia mikataba ya kinyonyaji kama ya IPTL na SONGAS, tena shirika bado lina madeni zaidi ya bilioni tano! (utaambiwa walinunua vipuri, sijui kwanini hawakulipa "cash"?)
Suluhisho la yote ni kubadili sera ya nishati, lazima nchi ijitegemee katika nihati na tusibinafsishe au kuwapa wageni jukumu la kutuzalishia nishati.
Lolote lile lifanyike ili taifa liendelee na jukumu la kuzalisha umeme ndipo angalau bei inawaza pungua. vyanzo vya umeme wa uhakika tunavyo kama vile Gesi na makaa ya mawe, nahata maporomoko ya maji bado yapo mahala pengi tu nchini?
Umeme wa maji ndio ulio nafuu baada ya ule wa atomoki, juhudi zifanyike ili kuzalisha umeme mdogo mdogo wa maji katika mito yote nchini.
Pia umeme wa nguvu ya upepo na wa mionzi ya jua unafaa sana hasa vijijini ambako miundombinu ya gridi ya taifa haijafika.