Cylinder head gasket kungua kila mara kwenye vitz

Watanzania Bwana kwani kipaombele Cha Kila Mtu ni Nyumba??

Nimejibu kulingana na changamoto yake.

Hiyo gari kwa namna ilivyo, hata akifanya tax, siyo asset bali ni liability. Kanunua rahisi ila kiuhalisia ni gharama kubwa. Ndiyo maana nikasema angenunua ardhi kwa hiyo pesa ndogo ingekuwa sawa kuliko hilo gari bovu lake
 
Tafuta hela kijana vitz sio gari itakua hyo ni baskeli ya shamba boy wangu kwenda kukatia majani nguruwe zangu
 
Wadau habari,nina kagari kangu ka vitz old model.Kumbukeni mimi ni kabwela nimejichanga changa tu japo na mm nipate kausafiri.

Sasa kalikuwa na leakage, fundi akafungua cylinder head akatibu leakage akafunga.Baada ya hapo kakawa kanazima zima mguu usipokuwa kwenye accelerator.Nikakarudisha kwa fundi,akafungua,akakuta cylinder head gasket imeungua.

Akabadilisha,akakawasha kakaunguruma kidogo,kakawa kana kanachanganya compresion.Akafungua cylinder head tena.Kakuta gasket imeungua.Akabadilisha tena akapiga pasi cylinder head.

Akafunga,akawasha,imeungua tena. Wadau naombeni msaada.Shuda iyakuwq ni nini hapa

Fanya yafuatayo
1. Fungua na osha radiator
5. Weka coolant ya abro kopo tatu au nne bila kuchanganya na maji
2. Pima injini block kujua kama imepinda, ina crack au la
3.nunua gasket mpya , paka block na cylinder head na gasket sealer kabla ya kuifunga.
4. Badilisha water pump
6. Umemaliza kazi
 
It seems gari umeinunua bei rahisi sana. Dah!

Kuna mzee alinihusia akaniambia 'kijana, ukitaka kuendelea wekeza kwenye nyumba, siyo magari'. Mfano, hela yako ungenunulia kiwanja, then baadaye ukiwa na hela nzuri unanunua gari nzuri.

Ila sasa hiyo nzuri nayo si itaharibika tu! Cheap is expensive!
Kupanga ni kuchagua. Na kila mtu ana kipaumbele chake. Mimi nilianza kazi tu mwaka mmoja nikanunua gari. Tena si kwa mkopo bank. Watu walianza na hizo stories.nliwaambia tu wasinipangie maisha. Wakitaja kujenga wajenge sili kwao,silali kwao. Siwategemei.

Haukupita muda wakaanza kupishana banks kutafuta mikopo. Walipoona na enjoy life. Miaka hiyo ya 2000s. Acha mtu aishi alivyopanga. Maisha hayana kanuni.
 
Tafuta hela kijana vitz sio gari itakua hyo ni baskeli ya shamba boy wangu kwenda kukatia majani nguruwe zangu
Sasa wenye pesa na akili hawawezi mnunulia shamba boy Vitz. Huwa wananunua Pick Up. Inaweza kuwa Nissan, Toyota, Ford n.k wewe umeusikia huu msemo kwa shemeji yako yule mlevi akiwa amelewa umeubeba hivyo hivyo. Ngoja siku shemejio awape talaka.
 
Nimejibu kulingana na changamoto yake.

Hiyo gari kwa namna ilivyo, hata akifanya tax, siyo asset bali ni liability. Kanunua rahisi ila kiuhalisia ni gharama kubwa. Ndiyo maana nikasema angenunua ardhi kwa hiyo pesa ndogo ingekuwa sawa kuliko hilo gari bovu lake
Watanzania wengi hasa hawa middle class. Hununua LIABILITIES wakati mwingine wakidhania ni asset.
 
Mkuu, hiyo block imepinda mkuu...badili block au fanya re- surfacing kama block haijaharibika sana au nunua mswaki... remember vitz ina super reliable and durable engine..hiyo engine umeiua kwa overheating....
 
Back
Top Bottom