Gorgeousmimi
JF-Expert Member
- Jun 21, 2010
- 9,296
- 7,688
Habari za saa hizi waungwana.
Tuanze na kama title ya uzi huu inavyowakilisha.Cyberbullying ni nini?Kama tunavyojua kuna wambea,wasengenyaji,wazushi na wanafiki kwenye kila jamii.
Cyberbullying ni uzushi wa kwenye internet kupitia kwenye mitandao.Uzushi huo unaweza kuwa wa aina tofauti,unaweza kuwa kama mtu anakufatilia maisha yako na kuzusha vitu visivyo na ukweli au hata vyenye ukweli lakini aongeze pilipili na chumvi ili apate attention.
Kwenye cyber bullying kuna victim na kuna bully.Bully/mzushi ni mtu ambaye kwa lugha ya rahisi anayependa "ATTENTION", au tumuite "ATTENTION SEEKER"mtu huyo anakuwa na character ya kutokujiamini,kuwa na low-self esteem na mpweke.
Anakuwa mpweke kiasi cha kwamba anaona njia pekee ya yeye kuonekana ni kuzusha vitu visivyo na ukweli.Ni mtu ambae muda wote anataka aonekane na yeye yumo anavuma na hajachacha.
Mtu huyo huyo hajali maslahi ya athari atazozipata victim,kwasababu kwake yeye akipata attention ni furaha,anaona furaha watu wakifanya masikhara.
Bully ni mtu ambae anakuwa anafikiri na kufatilia sana maisha ya wengine baadala ya kutumia muda wake kufikiri vitu vyenye maendeleo na manufaa kwenye maisha yake.Nimeshashuhudia kesi tofauti ambazo watu wamekuwa bullyed mpaka kupelekea kifo,ni kitu kinachosikitisha mno.
Wanasema njia pekee ya kuepuka kuwa bullyed ni kuwa na nguvu za kukabiliana na mzushi na kumueleza kuwa hutovumilia upuuzi wake tena.Lakini swali linakuja tutazuia vipi cyberbullying wakati hali hio inatokea kwenye mitando na kuna uwezekano mkubwa humfahamu muhusika.Naelewa kuna wahanga wengi walopitia cyberbullying au hata bullying katika jamii tunazoishi.
Je mlichukua hatua gani hali hiyo ilipowakuta?Kuna kitu ambacho ulikifanya ungekifanya tofauti?Unadhani ni jukumu la nani kuhakikisha hali hio haitokei tena?Wahusika wa mitandao?Je kama umewajulisha kuhusu hali hio na hawakuchukua hatua zozote utakuwa na imani nao na mtandao wanaowakilisha?
Karibuni mtoe michango yenu.
Gorgeousmimi
Tuanze na kama title ya uzi huu inavyowakilisha.Cyberbullying ni nini?Kama tunavyojua kuna wambea,wasengenyaji,wazushi na wanafiki kwenye kila jamii.
Cyberbullying ni uzushi wa kwenye internet kupitia kwenye mitandao.Uzushi huo unaweza kuwa wa aina tofauti,unaweza kuwa kama mtu anakufatilia maisha yako na kuzusha vitu visivyo na ukweli au hata vyenye ukweli lakini aongeze pilipili na chumvi ili apate attention.
Kwenye cyber bullying kuna victim na kuna bully.Bully/mzushi ni mtu ambaye kwa lugha ya rahisi anayependa "ATTENTION", au tumuite "ATTENTION SEEKER"mtu huyo anakuwa na character ya kutokujiamini,kuwa na low-self esteem na mpweke.
Anakuwa mpweke kiasi cha kwamba anaona njia pekee ya yeye kuonekana ni kuzusha vitu visivyo na ukweli.Ni mtu ambae muda wote anataka aonekane na yeye yumo anavuma na hajachacha.
Mtu huyo huyo hajali maslahi ya athari atazozipata victim,kwasababu kwake yeye akipata attention ni furaha,anaona furaha watu wakifanya masikhara.
Bully ni mtu ambae anakuwa anafikiri na kufatilia sana maisha ya wengine baadala ya kutumia muda wake kufikiri vitu vyenye maendeleo na manufaa kwenye maisha yake.Nimeshashuhudia kesi tofauti ambazo watu wamekuwa bullyed mpaka kupelekea kifo,ni kitu kinachosikitisha mno.
Wanasema njia pekee ya kuepuka kuwa bullyed ni kuwa na nguvu za kukabiliana na mzushi na kumueleza kuwa hutovumilia upuuzi wake tena.Lakini swali linakuja tutazuia vipi cyberbullying wakati hali hio inatokea kwenye mitando na kuna uwezekano mkubwa humfahamu muhusika.Naelewa kuna wahanga wengi walopitia cyberbullying au hata bullying katika jamii tunazoishi.
Je mlichukua hatua gani hali hiyo ilipowakuta?Kuna kitu ambacho ulikifanya ungekifanya tofauti?Unadhani ni jukumu la nani kuhakikisha hali hio haitokei tena?Wahusika wa mitandao?Je kama umewajulisha kuhusu hali hio na hawakuchukua hatua zozote utakuwa na imani nao na mtandao wanaowakilisha?
Karibuni mtoe michango yenu.
Gorgeousmimi