CWT kukata mshahara bila idhini ya mwalimu

CWT kukata mshahara bila idhini ya mwalimu

Kwa mujibu wa sheria ya ajira na mahusiano kazini, makato ya agency fees hufanyika baada ya makubaliano ya pande tatu(mwajiliwa, mwajili na chama)Makubaliano hayo lazima yaoneshe chama kitamfanyia nini mwajiliwa. Walimu wenzangu tambueni kuwa malipo yeyote unayo towa kwa chama cha wafanyakazi unanunua huduma, sasa kama huduma unayopata ni ndogo kuliko fedha unayo katwa, kimbia kwani unaibiwa. Sasa hiyari ni yako kuendelea kuibiwa au kukataa kuibiawa kwani she ria zipo wazi tatizo ni uvivu wako.
 
Mwalimu nikuombe tu kabla hayajakukuta usikiseme vibaya chama cha walimu kimsingi tuombe maboresho lakini usiseme hakifai.Walimu hasa mnaoanza kazi na hasa Kwa kuzingatia mnamaliza vyuo bado wabichi chama kimewanusuru wengi nusura wafukuzwe kazi na utumishi Kwa sababu yakupenda watoto Wa shule.Waulize walimu Wa Mihama secondary iliyoko mjini MWANZA watakusimlia.
 
"Chama kimewanusuru wengi nusura wafukuzwe kazi na utumishi kwa sababu ya kupenda watoto wa shule" sentensi hii imesababisha nipate maswali yafuatayo. 1.mwandishi amelenga walimu wazinifu wajiunge na chama hiki ili wanapo wazini watoto wa shule chama kiwatete wasifukuzwe kazi? 2. Hii ndio kazi ya CWT. 3. Kiwango cha michango ya wanachama kinacho kusanywa kinaweza kuthamanishwa na idadi ndogo ya kesi hizi na zingine? SAMAHANI NAWAZA TU.
 
Tatizo lako ni uelewa, nimetolea mfano Wa kesi zinazo gharimikiwa na chama kama moja ya majukumu yake. Nikushauri tu kama umeshaanza kukatwa nenda office ya chama uonane na Katibu atakupa utaratibu kwingine vinginevyo ikiendelea kulalamika wala haikusaidii.
 
Tatizo lako ni uelewa, nimetolea mfano Wa kesi zinazo gharimikiwa na chama kama moja ya majukumu yake. Nikushauri tu kama umeshaanza kukatwa nenda office ya chama uonane na Katibu atakupa utaratibu kwingine vinginevyo ikiendelea kulalamika wala haikusaidii.

Kisheria
Kama hajajiunga hatakiwi kukatwa. Ni lazima Mwalimu, Mwajiri na CWT kama agency wakubaliane ndio wamkate huyu mwalimu.
 
mm kwa uelewa wangu kuna fom ya TUF6 kama sikosei ukishajaza ndo utaanza kukatwa, kinyume na hapo ni wizi huo, chama siyo kibaya ila tungeungana kwa pamoja kudai yafanyike marekebisho ikiwa ni pamoja na kupunguza makato, pia lingine waweke wazi kuhusu mapato ya vitega uchumi vilivyopo.
 
Back
Top Bottom