CV ya Dickson Maimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa

Well said mkuu, hila hapo kwenye red nadhani umeghafilika kidogo - kama kuna GUI kuna haja gani tena ya kuandika CODE ya kusave file kwa kutumia CLI? One more thing, hivi kwenye 1980s Treasury ilikuwa na Mainframe au Minicomputer - 'am just curious! Thanks.

Nilichanganya mkuu nilikua na maana hakukuwa na GUI ndio maana code ilikua inaandikwa ya hata kusave files, Treasury walikua na Mainframe ICL ME29. Kama sijakosea
 
weewe unayetaka cv ya wenzio yawezekana unayo ya cafteria au ya underweaR,,,, CV siyo issue ...weledi + cv
 
Ni kweli mkuu asikudanganye mtu, vyeti kama siyo vya kugushi ni vya muhimu sana, mtu kama amesoma vizuri ni rahisi sana kukabiriana na changa moto za kila sampuli ukiwa kazini hata kama huna handon experience katika nyanja husika, itakuchukua muda mfupi kujipanga na kukabiliana na kila kitu kwa kujiamini.

Mimi sijakataa kusoma kuzuri maana na mimi nimesoma tuu ila sikusoma kama Tanzania wanavyotaka Degree ya Kwanza na Masters - hawatambui Advanced Diploma na vyeti vinginewe vingi tuu kama ni kusoma, tunapotofautiana ni aina gani ya elimu.

Na kama mchangiaji mmoja alivyosema unasoma kwa malengo sio kujisomea tuu , mimi nikienda sasa hivi kuchukua Degree na Masters ya Computer Science nitakuwa na malengo gani ?, kama malengo nikupata kazi Tanzania yes I need to do that maana ndio mfumo uliopo

Kwa huku nilipo hata ningeenda na nikamaliza hiyo nikaenda kuajiriwa sitaongezea chochote kwenye Malipo yangu au Cheo, wataangalia tuu accomplishment zangu , yaani niende kusoma tuu ili nibandike cheti ukutani

Kama ingekuwa biashara zangu za consultancy zinakufa shauri sina MBA or CPA na nikafanya cost analysis nikaona kuajiri MBA na CPA at a long run its more expensive na kusoma kutanisaidia hapo nitaenda haraka kuzichukua maana sina hiyo backround lakini sitaenda tuu kusoma shauri niziweke kwenye Ukuta

Kuna watu wengi wamekuja Marekani na kusoma bila malengo na wakajikuta wako kwenye kazi zile zile na sana sana wametumia email ya pongezi kumaliza Masters, wako waliosoma kwa malengo kuangalia walichonacho wakabuild kidogo wamefanikiwa

Na kuna wengi waliosoma wakiwa na malengo ya kurudi bongo wakachukua Masters haraka sana wakafanikiwa sana waliporudi Tanzania
 
Hizo ni kama porojo,tuliokuwa tupo Moshi enzi hizo za Kamanda Chico tunajua nini kilikuwa kinafanyika pale CCP-Moshi so hizo hhabari za kuwa na passport nyingi ni hadithi tu za alinacha .Mimi nafahamu watu wengi tu kwenye hilo Jeshi la polisi waliotumia vyeti vya watu kuingia CCP.[/QUOTE

Thanks very much Mwakalinga. You nailed it well. Ninakubaliana na wewe kwa asilimia 50-60 ya askari polisi wa enzi hizo wa miaka ya nyuma (sijui kwa miaka ya karibuni hasa kuanzia 2005 tangu NECTA wafunguke macho) wengi wao ni vyeti fake. Nina watu kibao ambao walikuwa wananiomba copy ya vyeti vyangu ili wakafotoe kwa bahati nzuri sikuwahi kuwapa na kama kuna ambaye ameiba cheti changu nafikiri this time ni lazima mambo yawe hadharani. Thanks so much Mr. Maimu. He is doing his job!!!!!! Watu hamkumuelewa, hata kama askari wa sehemu nyeti iwe majeshi au polisi kama alibadilishwa jina ni lazima itaonekana maana katika zoezi hili wanahitaji cheti chako cha kuanzia ubatizo (wakristu), shule ya msingi, sekondari level zote, vyuo, passport, mpiga kura, TIN number, Drivers lisence, Birth certificate, etc. Sasa basi hata kama wewe ni usalama wa taifa cheti chako cha ubatizo hadi Chuo ni lazima kiwe na majina ya kufanana!!! Kama ulirudia shule ukapewa jina lingine hii inakuwa zaidi kwa ngazi ya shule ya msingi na ina maana cheti chako cha shule ya msingi kitakuwa tofauti na cha ubatizo. Kama kweli mtu amekuwa na cheti cha form iv na vi na kuendelea ambacho ni tofauti na cha darasa la saba halafu eti unasema ni jina tofauti alilopewa kiusalama nitakataa. Ninachofahamu ukiwa umeshaingia hizo sehemu nyeti ndipo unapewa jina la kazi but wanajuwa kabisa jina lako halisia ni MAAANE na si vinginevyo na unaweza kupewa majina hata hamsini kulingana na issue tofauti za kiusalama unazoshughulikia. Tatizo langu kwa nini cheti chako cha kidato cha nne kiwe tofauti na cha darasa la saba? Kweli utajitetea form four ulishakuwa na majukumu ya kiusalama ukawa umebadilishwa jina? Na hayo majina unayopewa ya bandia ni pale unapokuwa na cheo na jukumu kubwa kiusalama!!!!

Nchi hii wapo wenye vyeti fake tena vina division 1 au upper second za vyuo!!! Sasa tunawataka hadharani!!!

Long live Maimu and your team!!
 
wekeni cv wakuu tunataka tusome tuone uwezo wake kabla hatuja hukumu
wewe wacha majungu mbona cv yako ujaweka toa buruti kwenye jiccho lako watu wengine mtawakuta maneno tuuu
kumbe ni mambu mbumbu kwisha weka CC yako tukupe kazi ya kuwa mkurungenzi mkuu wa vitambulisho vya Taifa
mnapenda tu kupost lakini hakuna vitendo .
 
Wakuu naomba sana mwenye CV ya mkuu huyu Dickson Maimu,kila wakati huyu akitokea kwenye Tv ninakuwa na mashaka sana na uwezo wake,kipindi cha nyuma alikuwa anatokea akiwa amevaa cheni shingoni na mapete kibao na mkufu mkononi,kwa kweli inanitia mashaka sana kama kweli ni mtu anayefaa kwa kazi hii,,vile vile kuongea kwake ni kama mtu wa kawaida wa kijiweni nashindwa nimweke kwenye kundi gani kiuwezo,naomba kujua kama kweli ni mtu aliye tayari kufanya kazi hiyo ya muhimu kabisa ya kuwapatia watanzania vitambulisho vya taifa kwa mara ya kwanza kabisa

Lazima tuhoji inaelekea hana ethics za Kudress officially
 
Back
Top Bottom