CUF wafuta maandamano yao

Mzee wa Rula

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
8,171
3,346
Wana JF Prof. Ibrahimu Lipumba ametangaza kuwa kesho hakutakuwa na maandamo ya chama kama ilivyotangazwa na Julius Mtatiro baada ya kuombwa na waziri mkuu Mizengo Pinda. Hivyo amewataka wanachama na mashabiki kutojitokeza kesho kwenye maandamano na wale ambao hawatakuwa na taarifa ya kufuta maandamano basi wasibugudhiwe bali waalimishe.
Source TBCI 20:00 Taarifa ya Habari.
 
Wana JF Prof. Ibrahimu Lipumba ametangaza kuwa kesho hakutakuwa na maandamo ya chama kama ilivyotangazwa na Julius Mtatiro baada ya kuombwa na waziri mkuu Mizengo Pinda. Hivyo amewataka wanachama na mashabiki kutojitokeza kesho kwenye maandamano na wale ambao hawatakuwa na taarifa ya kufuta maandamano basi wasibugudhiwe bali waalimishe.
Source TBCI 20:00 Taarifa ya Habari.

Hii ndio shida ya CCM B kutaka kupinga serikali wakati na yenyewe ni sehemu ya serikali. Nilikuwa najiuliza hivi lini alipewa talaka? Au alikuwa hajanunuliwa kanga kwa muda mrefu kwa hiyo alikuwa anatingisha kiberiti?
 
Wana JF Prof. Ibrahimu Lipumba ametangaza kuwa kesho hakutakuwa na maandamo ya chama kama ilivyotangazwa na Julius Mtatiro baada ya kuombwa na waziri mkuu Mizengo Pinda. Hivyo amewataka wanachama na mashabiki kutojitokeza kesho kwenye maandamano na wale ambao hawatakuwa na taarifa ya kufuta maandamano basi wasibugudhiwe bali waalimishe.
Source TBCI 20:00 Taarifa ya Habari.

Kwa sababu ati ya ugeni wa kitaifa wa Mama Clinton. Na kweli ni ugeni wa kitaifa kwaa kuwa nimeona Red carpet nikashangaa. Mimi Nadhani mkuu wa nchi ndio anakanyaga red carpet kumbe hata waziri wa mambo ya nje.

Kuhusu hao ambao hawatapata taarifa nadhani Mwenyekiti wao anataka kuwaponza kwa kuwa Tanzania hatuna jeshi la polisi la kuelimisha tuna jeshi la kupiga!! Watapigwa!!
 
Kesho ilikuwa siku nzuri kuandamana coz Bi. Clinton yupo hapa. Wangekuwa CDM nadhan wangeitumia vema hii chance kama walivyowalk out bungeni. CUF hawako serious coz kama lengo ni kupinga uonevu wasingesubiri kunegociate na CCM ambaye ndiye muonezi mkuu.
 
Kumbe pinda yupo, hazuii mauaji anazuia maandamano! Kama cuf walimaanisha wangetangaza kuyafanya next weekend, au labda clinton atakuwepo bado!
 

Mwenyekiti Taifa wa chama cha CUF Profesa Ibrahim Lipumba
----
Mwenyekiti Taifa wa chama cha CUF Profesa Ibrahim Lipumba ametangaza kufuta maandamano yaliyopangwa na chama hicho kufanyika kesho..Profesa Lipumba Amesema uamuzi huo umekuja baada ya kuombwa na Mhe Waziri Mkuu, Mizengo Pinda!Hivyo kesho hakutakuwa na maandamano hayo tena hadi siku yatakapotangazwa tena.

CUF ilitangaza kufanya maandamano makubwa kesho kuanzia saa 3:00 asubuhi kutoka Ubungo hadi Manzese Bakheresa, lengo likiwa kupinga mauji yanayofanywa na polisi dhidi ya raia nchini.​
 
Wanamuugopa clinton kuliko Mungu, kwamba ni aibu kwa taifa kwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa marekani kuona watanzania wakiandamana kuiambia serikali yao iache kuua raia ambao wameiweka madarakani kwa tofauti zinazosababishwa na uwekezaji usiojali haki za msingi za wananchi wake. Hilary anaweza asione akiwa Tanzania lakini amesikia akiwa Marekani. Hata hivyo Mungu ameona na tayari ameisha fanya hukumu, kwani katika maagizo yake amekataza kuua, kwake hatuwezi kufanya unafiki kwani anatuona mpaka rohoni.
 
CUF ni vibaraka wa CCM kwahiyo sishangai wao kumwabudu mgeni wa ccm HILARY CLITTON
 
CUF ISHA ISHA.ET MAANDAMANO WAPI! Propesa li pumba hana chochote zaidi ya pumba kichwani mwake.
 
CUF ISHA ISHA.ET MAANDAMANO WAPI! Propesa li pumba hana chochote zaidi ya pumba kichwani mwake.
Prof Lipumba bado atabaki kuwa lulu nchi hii kutokana na michango yake katika mambo mbali mbali mf. jinsi alivyoichambua bajeti iliyosomwa majuzi. Kasoro kubwa iliyomkumba ni nuru ya chama chake imeanza kufifia.
 
MarkoMAANDAMANO yaliyokuwa yafanywe jana na Wanachama wa CUF, yaliahirishwa baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwaomba wasitishe kama walivyoambiwa na Jeshi la Polisi kutokana na ugeni wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton.

Cliton ambaye aliwasili nchini juzi kwa ziara ya siku tatu, jana alitembelea mitambo ya kuzalisha Umeme ya Symbion iliyopo Ubungo Dar es Salaam ambapo ndipo maandamano ya CUF yalitakiwa kuanzia na kumalizikia Manzese Bakhresa.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro aliliambia gazeti hili jana kuwa waliahirisha maandamano hayo kutokana na ombi la Waziri Pinda kupitia Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba ambalo alimtaka asitishe maandamano kutokana na ugeni uliopo.

Mtatiro alisema jana kwamba Profesa Lipumba alipokea barua kutoka kwa Pinda iliyoitaka CUF kusitisha maandamano hayo kwa sababu maeneo yalipotakiwa kuanzia ni moja ya sehemu ambazo mgeni huyo angetembelea.

Alisema Pinda aliwataka kusitisha maandamano hayo kwa sababu za kiusalama kwa kiongozi huyo wa Marekani.“Busara za uongozi wa Waziri Mkuu zilitumika, wakatuambia kuwa maeneo ambayo tungefanyia maandamano hayo ndiko msafara wa kiongozi huyo ungepita kwa hiyo viongozi waandamizi wa CUF tulikaa pamoja na kukubaliana tuyaahirishe,”alisema na kuongeza kuwa;“Pinda alitushauri na kutueleza kuwa kama sisi tungekuwa ndiyo viongozi wa nchi halafu kuna ujio wa kiongozi mkubwa kama huyo anayekuja akakuta maandamano ingekuwaje?

Tulimuelewa na ndio maana tumeahirisha.”Hata hivyo Mtatiro alilishutumu Jeshi la Polisi kutokuwa wawazi kwa kudai kuwa walikataa maandamano hayo kwa sababu za kiusalama bila kueleza kuwa Clinton atafanya ziara katika maeneo ambayo yatakuwapo maandamano.

“Baada ya ufafanuzi huo wa barua ya Waziri Pinda tulikaa kikao na viongozi waandamizi wa chama tukajadili na kuona ni vema tukaahirisha ili hata msafara wa Clinton ukipata tatizo tusilaumiwe,” alisema Mtatiro.

Pia alisema baada ya kuondoka kwa kiongozi huyo wa Marekani, CUF itakaa kikao na viongozi waandamizi wa chama hicho ili kupanga siku ambayo watafanya maandamano. Juni 6 mwaka huu, CUF ilitangaza kufanya maandamano makubwa ambayo yangefanyika jana kuanzia Ubungo hadi Bakhresa Mazense kwa lengo la kupinga mauaji yanayofanywa na polisi dhidi ya raia nchini.
Lakini kulikuwa na mvutano mkubwa baina yao na polisi ambao waliwataka CUF kutofanya maandamano lakini walisisitiza kuendelea na msimamo wao wakidai kuwa Clinton si kiongozi wao, bali ni Mmarekani hivyo hawezi kuzuia maandamano hayo yanayodai haki za Watanzania.
Akitolea mfano Tamko la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu (UDHR) la mwaka 1945 linatoa haki ya kuandamana ikiwa watu au chama kinataka kuonyesha hisia zake kwa jamii na kwamba Tanzania ni mjumbe wa umoja huo na imeridhia.
“Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 ambayo tayari ina viraka zaidi ya 14 inatoa haki kwa raia wa Tanzania, vikundi au taasisi kutoa mawazo au hisia zao na hii iko kifungu ch 1 ibara ya 20,”alisema.

Aidha Mtatiro alisema kifungu cha 43(3) kinaeleza kuwa Ofisa wa Polisi hawezi kukataza maandamano chini ya kifungu cha 43 (2), isipokuwa iwapo atajiridhisha kuwa mkusanyiko huo utasababisha uvunjifu wa amani au utaathiri usalama wa nchi.
Alisema maandamano yatakayofanywa na CUF yatakuwa ya amani na kwamba hayatakuwa na silaha za moto isipokuwa watabeba mabango na kufikisha ujumbe walioukusudia kwa wananchi.“Kwa mantiki hiyo kukataza maandamano bila polisi kusema yatavuruga vipi amani ni uzembe wa dhahiri na kamwe chama hakiwezi kusitisha maandamano kwa kutekeleza uzembe,”alisema.
 
aaahg,.................. mbona hapo ndipo palikuwa pazuri sasa na ujumbe wao ungeifikia marekani na dunia nzima instantly???...................... hawa cuf nao vipi??.................. they had knowingly given up a golden chance!!.................
 
MarkoMAANDAMANO yaliyokuwa yafanywe jana na Wanachama wa CUF, yaliahirishwa baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwaomba wasitishe kama walivyoambiwa na Jeshi la Polisi kutokana na ugeni wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Hillary Clinton.

Cliton ambaye aliwasili nchini juzi kwa ziara ya siku tatu, jana alitembelea mitambo ya kuzalisha Umeme ya Symbion iliyopo Ubungo Dar es Salaam ambapo ndipo maandamano ya CUF yalitakiwa kuanzia na kumalizikia Manzese Bakhresa.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro aliliambia gazeti hili jana kuwa waliahirisha maandamano hayo kutokana na ombi la Waziri Pinda kupitia Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba ambalo alimtaka asitishe maandamano kutokana na ugeni uliopo.

Mtatiro alisema jana kwamba Profesa Lipumba alipokea barua kutoka kwa Pinda iliyoitaka CUF kusitisha maandamano hayo kwa sababu maeneo yalipotakiwa kuanzia ni moja ya sehemu ambazo mgeni huyo angetembelea.

Alisema Pinda aliwataka kusitisha maandamano hayo kwa sababu za kiusalama kwa kiongozi huyo wa Marekani."Busara za uongozi wa Waziri Mkuu zilitumika, wakatuambia kuwa maeneo ambayo tungefanyia maandamano hayo ndiko msafara wa kiongozi huyo ungepita kwa hiyo viongozi waandamizi wa CUF tulikaa pamoja na kukubaliana tuyaahirishe,"alisema na kuongeza kuwa;"Pinda alitushauri na kutueleza kuwa kama sisi tungekuwa ndiyo viongozi wa nchi halafu kuna ujio wa kiongozi mkubwa kama huyo anayekuja akakuta maandamano ingekuwaje?

Tulimuelewa na ndio maana tumeahirisha."Hata hivyo Mtatiro alilishutumu Jeshi la Polisi kutokuwa wawazi kwa kudai kuwa walikataa maandamano hayo kwa sababu za kiusalama bila kueleza kuwa Clinton atafanya ziara katika maeneo ambayo yatakuwapo maandamano.

"Baada ya ufafanuzi huo wa barua ya Waziri Pinda tulikaa kikao na viongozi waandamizi wa chama tukajadili na kuona ni vema tukaahirisha ili hata msafara wa Clinton ukipata tatizo tusilaumiwe," alisema Mtatiro.

Pia alisema baada ya kuondoka kwa kiongozi huyo wa Marekani, CUF itakaa kikao na viongozi waandamizi wa chama hicho ili kupanga siku ambayo watafanya maandamano. Juni 6 mwaka huu, CUF ilitangaza kufanya maandamano makubwa ambayo yangefanyika jana kuanzia Ubungo hadi Bakhresa Mazense kwa lengo la kupinga mauaji yanayofanywa na polisi dhidi ya raia nchini.
Lakini kulikuwa na mvutano mkubwa baina yao na polisi ambao waliwataka CUF kutofanya maandamano lakini walisisitiza kuendelea na msimamo wao wakidai kuwa Clinton si kiongozi wao, bali ni Mmarekani hivyo hawezi kuzuia maandamano hayo yanayodai haki za Watanzania.
Akitolea mfano Tamko la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu (UDHR) la mwaka 1945 linatoa haki ya kuandamana ikiwa watu au chama kinataka kuonyesha hisia zake kwa jamii na kwamba Tanzania ni mjumbe wa umoja huo na imeridhia.
"Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 ambayo tayari ina viraka zaidi ya 14 inatoa haki kwa raia wa Tanzania, vikundi au taasisi kutoa mawazo au hisia zao na hii iko kifungu ch 1 ibara ya 20,"alisema.

Aidha Mtatiro alisema kifungu cha 43(3) kinaeleza kuwa Ofisa wa Polisi hawezi kukataza maandamano chini ya kifungu cha 43 (2), isipokuwa iwapo atajiridhisha kuwa mkusanyiko huo utasababisha uvunjifu wa amani au utaathiri usalama wa nchi.
Alisema maandamano yatakayofanywa na CUF yatakuwa ya amani na kwamba hayatakuwa na silaha za moto isipokuwa watabeba mabango na kufikisha ujumbe walioukusudia kwa wananchi."Kwa mantiki hiyo kukataza maandamano bila polisi kusema yatavuruga vipi amani ni uzembe wa dhahiri na kamwe chama hakiwezi kusitisha maandamano kwa kutekeleza uzembe,"alisema.

Viongozi wa CUF walipaswa kuliona hilo mapema kabla ya kuombwa na Pinda. Imagine kama tukiwapa dola itakuwaje.... vululu vululu mpaka basi
 
Back
Top Bottom