Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Najua mtasema mbona hata CCM katibu mkuu ndiye mwenyekiti wa sekretarieti. Lakini ile inapaswa kuwa kamati ya utekelezaji wa maamuzi na kama CUF wanavyoiita kamati ya utendaji. Ina maana yupo anayeamua (labda kamati kuu au baraza) na kamati inasimamia utendaji. Lakini hili la sasa la kuwashughulikia waasi naona katibu mkuu kawa mwenyekiti kamili.
Kisha mna makatibu wasaidizi wawili, mmoja anasikika sana Tanganyika na Zanzibar na mwingine amekaa kimya tu akimwacha huyu wa huku abwabwaje. Hata minutes za vikao anazimwaga JF bila wasiwasi. Sasa huyu ndiye katibu mwa mwenyekiti maalim? Kuna nchi duniani zina rais wa heshima asiye na meno kama ilivyo kule Israel, ujerumani na India. Ndio nafasi ya Lipumba CUF?
Kisha mna makatibu wasaidizi wawili, mmoja anasikika sana Tanganyika na Zanzibar na mwingine amekaa kimya tu akimwacha huyu wa huku abwabwaje. Hata minutes za vikao anazimwaga JF bila wasiwasi. Sasa huyu ndiye katibu mwa mwenyekiti maalim? Kuna nchi duniani zina rais wa heshima asiye na meno kama ilivyo kule Israel, ujerumani na India. Ndio nafasi ya Lipumba CUF?