Elusive
JF-Expert Member
- Nov 26, 2008
- 223
- 4
Hizi fikira za udini katika mambo ya siasa zimetokea wapi? Mbona hivi sasa
yanakuzwa kama vile yana play part katika uongozi? Tanzania na masuala
ya dini ya mtu ni jambo ambalo halijatatiza nchi hii tangu kuasisiwa. Watu tangu
na enzi za zamani wanaishi pamoja wenye dini tofauti bila ya mikwaruzo tangu kuanzia
nyumba za kupanga mpaka kwenye uhuru wa kuabudu.
Ni akili finyu mtu kuamini mambo ya udini ndani ya vyama kwani kila chama
cha siasa kina watu wenye imani mbali mbali na wanaendesha vyama vyao
kistaarabu, chokochoko za watu wachache wanaojifanya wana elimu kushinda
wenzao na kuponda dini za watu ndizo zitakazotupeleka pabaya.
Kuchanganya usomi, udini na uongozi ni kupungukiwa na akili kiasi fulani.
KUWENI NA UPENDO KWA WATU WENYE DINI TOFAUTI ILI MUISHI NA
KUABUDU KWA AMANI.
yanakuzwa kama vile yana play part katika uongozi? Tanzania na masuala
ya dini ya mtu ni jambo ambalo halijatatiza nchi hii tangu kuasisiwa. Watu tangu
na enzi za zamani wanaishi pamoja wenye dini tofauti bila ya mikwaruzo tangu kuanzia
nyumba za kupanga mpaka kwenye uhuru wa kuabudu.
Ni akili finyu mtu kuamini mambo ya udini ndani ya vyama kwani kila chama
cha siasa kina watu wenye imani mbali mbali na wanaendesha vyama vyao
kistaarabu, chokochoko za watu wachache wanaojifanya wana elimu kushinda
wenzao na kuponda dini za watu ndizo zitakazotupeleka pabaya.
Kuchanganya usomi, udini na uongozi ni kupungukiwa na akili kiasi fulani.
KUWENI NA UPENDO KWA WATU WENYE DINI TOFAUTI ILI MUISHI NA
KUABUDU KWA AMANI.