CUF kuiteka Zanzibar kwa maandamano

CUF kuiteka Zanzibar kwa maandamano

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
26,715
Reaction score
59,251
Vijana wa Chama cha Wananchi kupitia jumuiya yao (JUVI-CUF) wameweka msimamo kuwa ‘iwe iwavyo’ watafanya maandamano kesho visiwani humo kwa kuwa ni haki yao kufanya hivyo licha ya Jeshi la Polisi kupinga.

Maandamano hayo yameelezwa kuwa ni sehemu kumbukumbu ya Wazanzibari waliouawa mwaka 2000 kutokana na vurugu za kisiasa zilizotokea chini ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Maandamano hayo yametangazwa ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kutangaza tarehe 20 Machi mwaka huu kuwa siku ya kurudia uchaguzi visiwani humo.

Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi mkuu visiwani humo uliofanyika tarehe 25 Oktoba mwaka jana kwa madai ya kuwepo kwa kasoro mbalimbali jambo ambalo lilipingwa na CUF, taasisi za kiraia na baadhi ya makada wa CCM.

JUVI-CUF wamepanga kufanya maandamano makubwa visiwani humo kwa lengo la kupinga dhulma hiyo licha ya Jeshi la Polisi kuyagomea.

Wameeleza kuwa maandamano hayo watayafanya ili kuieleza dunia kwamba, Zanzibar haki inaminywa na kwamba, maandamano hayo yatakakuwa ujumbe mahsusi kwa wapenda demokrasia duniani.

Vijana hao wamesema kuwa, hawawezi kuona haki yao inapokwa na serikali kwa maslahi ya CCM na kwamba, maandamano hayo yatafanyike visiwani humo kama ilivyopangwa.

Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa JUVI-CUF, Abeid Ali amesema kuwa, wananchi wa visiwa hivyo hawatokoma kudai haki yao mpaka pale itakaposimama.

Mkurugenzi huyo ameeleza kwamba, wana imani kuwa si risasi wala mizinga ambayo inaweza kusimamisha haki visiwani humo na kwamba, watapigania haki hata kama wengine watauawa.

Kiongozi huyo amekumbushia mauaji yaliyofanya na Serikali ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa baada ya Uchaguzi Mkuu 2000 na kwamba, wananchi hawajaingia woga wala kurudi nyuma kudai haki yao.

“Sisi ni raia wakizanzibari, tuna uhuru wa kuandamana kwani CCM waliachiwa kuandamana na ulinzi wakapewa, na sisi tuna haki ya kufanya maandamano,” amesema Ali.

Amesema kuwa, maandamano hayo yatafanyika kuanzia Mtendeni kwenda Mnazimmoja na kumalizikia kwenye viwanja vya Maisara.

Chanzo: Mwanahalisionline
 
Uhuru wa Kuandamana bila kibali? hawa nao wapigwe tu. Nchi bila taratibu si nchi tena, itabaki kuwa genge la wahuni
 
hayo maandamano hayana tija yoyote zaidi ya kuleta vurugu...kama wana hamu ya kuandamana waandamanie majumbani mwao...
 
Uhuru wa Kuandamana bila kibali? hawa nao wapigwe tu. Nchi bila taratibu si nchi tena, itabaki kuwa genge la wahuni
nchi bila utaratibu haifai, kupinga maandamano ni utaratibu, kuandamana ni utaratibu,kibali ni utaratibu na mengi tu ni utaratibu!!!!
 
nchi bila utaratibu haifai, kupinga maandamano ni utaratibu, kuandamana ni utaratibu,kibali ni utaratibu na mengi tu ni utaratibu!!!!

Sasa kama wanaomba kibali na wananyimwa pasipo sababu wafanye nini,wakati huo huo CCM wakiomba kibali wanapewa pasi na shida!!!
Kabla kibali hakijatolewa ni lazima mamlaka husika ijilidhishe na dhumuni la maandamao. si kila maandamano yana tija.
 
hayo maandamano hayana tija yoyote zaidi ya kuleta vurugu...kama wana hamu ya kuandamana waandamanie majumbani mwao...
Uhuru wa Kuandamana bila kibali? hawa nao wapigwe tu. Nchi bila taratibu si nchi tena, itabaki kuwa genge la wahuni

Yah right .............. wenye haki ya kuandamana ni UVCCM tu ............. tena pamoja na mabango yao ya kibaguzi!!
 
VIJANA wa Chama cha Wananchi kupitia jumuiya yao (JUVI-CUF) wameweka msimamo kuwa ‘iwe iwavyo’ watafanya maandamano kesho visiwani humo kwa kuwa ni haki yao kufanya hivyo licha ya Jeshi la Polisi kupinga. Anaandika Faki Sosi … (endelea).
Maandamano hayo yameelezwa kuwa ni sehemu kumbukumbu ya Wazanzibari waliouawa mwaka 2000 kutokana na vurugu za kisiasa zilizotokea chini ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Maandamano hayo yametangazwa ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kutangaza tarehe 20 Machi mwaka huu kuwa siku ya kurudia uchaguzi visiwani humo.
Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi mkuu visiwani humo uliofanyika tarehe 25 Oktoba mwaka jana kwa madai ya kuwepo kwa kasoro mbalimbali jambo ambalo lilipingwa na CUF, taasisi za kiraia na baadhi ya makada wa CCM.
JUVI-CUF wamepanga kufanya maandamano makubwa visiwani humo kwa lengo la kupinga dhulma hiyo licha ya Jeshi la Polisi kuyagomea.
Wameeleza kuwa maandamano hayo watayafanya ili kuieleza dunia kwamba, Zanzibar haki inaminywa na kwamba, maandamano hayo yatakakuwa ujumbe mahsusi kwa wapenda demokrasia duniani.
Vijana hao wamesema kuwa, hawawezi kuona haki yao inapokwa na serikali kwa maslahi ya CCM na kwamba, maandamano hayo yatafanyike visiwani humo kama ilivyopangwa.
Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa JUVI-CUF, Abeid Ali amesema kuwa, wananchi wa visiwa hivyo hawatokoma kudai haki yao mpaka pale itakaposimama.
Mkurugenzi huyo ameeleza kwamba, wana imani kuwa si risasi wala mizinga ambayo inaweza kusimamisha haki visiwani humo na kwamba, watapigania haki hata kama wengine watauawa.
Kiongozi huyo amekumbushia mauaji yaliyofanya na Serikali ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa baada ya Uchaguzi Mkuu 2000 na kwamba, wananchi hawajaingia woga wala kurudi nyuma kudai haki yao.
“Sisi ni raia wakizanzibari, tuna uhuru wa kuandamana kwani CCM waliachiwa kuandamana na ulinzi wakapewa, na sisi tuna haki ya kufanya maandamano,” amesema Ali.
Amesema kuwa, maandamano hayo yatafanyika kuanzia Mtendeni kwenda Mnazimmoja na kumalizikia kwenye viwanja vya Maisara.
Source Mwanahalisi forum
 
muandamane bila kibali kutoka polic? Mnakatazwa na police walinda aman mnalazimisha? Mkipigwa mtasema ccm ndo wameamurisha au, jaribun kuheshim sheria jaman na mkiandamana bila kibali mtapigwa tu kwa sababu hamna jinc pengne mmemis virungu vya polic
 
Kwani wakiandamana na kuimba weee na kuzungumza ya kwao hadi waishiwe ya kusema, nyie mnaowazuia au kutokubali mna hasra gani? Waacheni waandamane!
 
Vijana wataandamana, Polisi watatumika kupambana na waandamanaji wasio na hata manati, maafa yanaweza kutokea na maisha ya watu yakapotea jee nini kitafuata?
Nionavyo mimi, kwa mara ya kwanza tutashuhudia viongozi wa Kitanzania nchi inayojiita ya amani na utulivu wakipelekwa kwenye mahakama ya kimataifa ya Uhalifu dhidi ya binadamu. Chondechonde ccm acheni kuwaponza wazee wenu hawa, hivi mnaona raha gani mkija sikia wananyea debe huko Ulaya kwa kuwalazimisha wafanye mkitakacho?
Nina uhakika mzee kama Shein hata hamu na haya mambo hana tena na alipenda baada ya kukataliwa kwa kura akajipumzisha na kula pension yake kwa raha mustarehe na Mama Mwema wake. Lakini nyie wabaguzi kwa vile kikiwaka hamtakamatwa nyie basi mnaona potelea mbali. SHAURI YENU!
 
Vijana wa Chama cha Wananchi kupitia jumuiya yao (JUVI-CUF) wameweka msimamo kuwa ‘iwe iwavyo’ watafanya maandamano kesho visiwani humo kwa kuwa ni haki yao kufanya hivyo licha ya Jeshi la Polisi kupinga.

Maandamano hayo yameelezwa kuwa ni sehemu kumbukumbu ya Wazanzibari waliouawa mwaka 2000 kutokana na vurugu za kisiasa zilizotokea chini ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Maandamano hayo yametangazwa ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kutangaza tarehe 20 Machi mwaka huu kuwa siku ya kurudia uchaguzi visiwani humo.

Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi mkuu visiwani humo uliofanyika tarehe 25 Oktoba mwaka jana kwa madai ya kuwepo kwa kasoro mbalimbali jambo ambalo lilipingwa na CUF, taasisi za kiraia na baadhi ya makada wa CCM.

JUVI-CUF wamepanga kufanya maandamano makubwa visiwani humo kwa lengo la kupinga dhulma hiyo licha ya Jeshi la Polisi kuyagomea.

Wameeleza kuwa maandamano hayo watayafanya ili kuieleza dunia kwamba, Zanzibar haki inaminywa na kwamba, maandamano hayo yatakakuwa ujumbe mahsusi kwa wapenda demokrasia duniani.

Vijana hao wamesema kuwa, hawawezi kuona haki yao inapokwa na serikali kwa maslahi ya CCM na kwamba, maandamano hayo yatafanyike visiwani humo kama ilivyopangwa.

Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa JUVI-CUF, Abeid Ali amesema kuwa, wananchi wa visiwa hivyo hawatokoma kudai haki yao mpaka pale itakaposimama.

Mkurugenzi huyo ameeleza kwamba, wana imani kuwa si risasi wala mizinga ambayo inaweza kusimamisha haki visiwani humo na kwamba, watapigania haki hata kama wengine watauawa.

Kiongozi huyo amekumbushia mauaji yaliyofanya na Serikali ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa baada ya Uchaguzi Mkuu 2000 na kwamba, wananchi hawajaingia woga wala kurudi nyuma kudai haki yao.

“Sisi ni raia wakizanzibari, tuna uhuru wa kuandamana kwani CCM waliachiwa kuandamana na ulinzi wakapewa, na sisi tuna haki ya kufanya maandamano,” amesema Ali.

Amesema kuwa, maandamano hayo yatafanyika kuanzia Mtendeni kwenda Mnazimmoja na kumalizikia kwenye viwanja vya Maisara.

Chanzo: Mwanahalisionline
singone mbele kudai hakiyenu ,na uhakika kuna watu wataenda watapelekwa mahaka ya kimatsifa
 
ndio maana leo naona landcruisers zao zinazunguka mjini zimewasha taa ka zimebeba maiti na askari wamebeba silaha zao, nikajiuliza kuna nini, kumbe ni hili duu, wananchi wametulia wanaendelea na shughuli zao
 
Back
Top Bottom