Cuf inakufa kifo chema

Cuf inakufa kifo chema

watu wengine bana ww kusoma hujui, hata picha huoni? hivi nani asiyejua ccm B, imepoteza muolekuo, huku bara inawabunge wangapi? si bora hata chadema imesambaa karibu kona zote. ukienda kaskazini ipo mwanza kuna wabunge wao, nenda nyanda za juuu mbeya na iringa, kaskazini ndo usisemee. eeh tuambie cuf wanajivunia wapi?
Siasa za kwenye Vigango ndizo zinaenda kuimaliza CHADEMA
2015. Udini,udini,udini
 
Ingekuwa post hii inaiponda CHADEMA bila shaka ungeona matusi ya
nguoni yakiporomoshwa. Bahati CUF ina viongozi na wanachama waungwana
musitegemee matusi kutoka kwa wafurukutwa, wakereketwa, mashabiki na
wanachama wa CUF ni watu wastarabu sana, hii ni dalili kuwa nchi ikichukuliwa
na CUF itaendeshwa kistaarabu, Ole wettu kama CDM watachukua nchi itakuwa
ni Full matusi kuanzia maofisini mpaka majukwaani.

Aaa wapi,nijuavyo jukwaa kina sheria na mojawapo kutotoa matusi......ukweli unauma
 


Mkuu Mungi

Ni kweli operation za CUF hapa jijini Arusha zimejikita kwenye dimbwi la udini bahati mbaya wakuu wa hii mipango hawajui wapi watumie udini ili wafanikiwe na wapi wasitumie udini ili wafanikiwe.Mikoa ya kanda ya kaskazini unapotumia propaganda za kidini bila kujua ni dini gani ina wafuasi wengi hakika ni kujichimbia kaburi wakati bado unapenda kuishi.

Arusha City Cafe ni kamgahawa kadogo kasikokuwa na sifa ya hilo jina,ni sehemu iliyokuwa ikitumiwa na Dr Batilda kipindi cha kampeni za mwaka 2010 bahati mbaya kampeni ziliendeshwa kwa misingi ya dini na ukabila.CUF pengine kwa kutokujua mazingira ya Arusha wamehamishia propaganda zao dhaifu Arusha City Cafe wanazi wake sasa wanafaidi futari ya bure kipindi hiki cha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.Ifahamike wazi kijiwe hiki kilikuwa kijiwe cha CCM na si cha CDM.Hongera Juma mnene kazi nzuri makali ya gharama za futari hazikuhusu.Hongera Seif una uhakika wa wateja na kipato.

Mkuu Ngongo
Ni kweli kabisa kwamba Arusha City Cafe hakana hadhi ya kuwa na lile jina, na pia ilikuwa kijiwe cha CCM wakati wa kampeni. Lakini sasa kwa kuwa vyama hivi viwili CCM na CUF ni ndugu, wameona ndugu zetu CUF nao waitumie kile kijiwe kuiangamiza CUF kama kilivyotumika kuiangamiza CCM hapa Arusha.
CUF itakufa kifo kitakatifu kwakutumia udini kama mtaji.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom