Nimekupa usaliti wa Maalim Seif ni wa kuzuia vuvugu la kujinasua na Tanganyika na waliosimamia vuguvugu hilo Jumbe,Dourado na Dr. Swanzi, kwa pamoja Maalim kwa kauli yake akawaita wahaini mbele ya kadamunasi ya wazanzibari na mbele ya Nyerere, unataka ushahidi gani? Ushahidi wa Kinyamwezi mimi sina!
Usisuse tunajifunza mengi hapa JF.
Tatizo sio kauli za maalim tatizo kumwita msaliti wa vugu vugu na msaliti wa Zanzibar. Wewe umeegemea Maalim kumwita Dourado na Jumbe kuwa wahaini na kwa hivyo kuridhika kuwa Maalim ni msaliti yaani hoja zako hazitoshi. Ilikuwa ni muhimu tupate ushahidi zaidi kwa sababu SIRI ZA AJENDA YA DURADO NA JUMBE YA SERIKALI TATU HUIJUI .KUMBUKA HUYO MAALIM NA WENZAKE WALIKUWA PAMOJA NA HAO AKINA DORADO NA JUMBE KWENYE HII MOVE. Lakini kwa nini walitofautiana kwa mantiki ya hicho unachokiamini eti ni ubinafsi wa Maalim? na wala sio maslahi ya Zanzibar?
Nimekuomba utupatie ushahidi concrete huo uliotowa unapwaya.
Kama huna mwengine basi tufunge mjadala.