CUF ilikuwa na mgogoro kabla ya UKAWA

CUF ilikuwa na mgogoro kabla ya UKAWA

Ni mwendawazimu tu asiyekubali kuwa kujitoa kwa Lipumba na kurudi ofisini kwa nguvu ndiyo chanzo cha huu mgogoro.

Acheni unafiki.
Mkuu unafikiri hawajui? Wanajua sana ila wanajitoa ufahamu tu. Si unajua tena siasa za Afrika. Halafu kuwekwa rekodi sawa: Lipumba alirudishwa na serikali kwa kutumia nguvu ya fedha. Huyu mzee ameshazoea fedha za bure. Zile alizohongwa wakati wa uchaguzi zimemnogea na ametamani utajiri zaidi. Wanasheria wote wanaomtetea husema wazi kabisa fedha zao zote wanalipwa na serikali.
 
CCM wote ni kazi sana kujificha huwa kuna kipindi inabid waibuke mafichoni refer Slaa, Lipumba na wengine tunawasoma Jf
 
Uzi umeandaliwa kwa kiwango cha chini sana, mgogoro uliopo ni kati ya CUF na CCM kwa miaka mingi...,kuendesha siasa za upinzani Afrika siyo rahisi kama unavyofikiria tena unapopambana na chama dola.Humo upinzani wamejaa mamluki na huchukua muda kuwagundua. Fanya utafiti mkuu.
 
Seif na Lipumba wakikaa siku moja tu yanaisha haya

Tatizo huyo Lipumba wa kukaa na Seif alishajipotezea uhalali huo. Ningekuelewa ukilisema hilo endapo hawa watu wa CUF bara wangekua na kiongozi mwingine tofauti na Lipumba na akaanzisha hiyo movement.
Tatizo ni kwamba Lipumba alishajiuzulu mwenyewe bila kulazimishwa amerudi na ajenda mbili. Moja ni kulazimisha uhalali wake na ya pili ni huo mpasuko unaouongelea hivyo tusionganishe hivi vitu viwili.

Lipumba hana uhalali wa kuwa katika kiti alichokalia. Hiyo ni fact......mengine ndo yaleyale ya siasa za Tz tumeyazoea CCM,CUF,CDM,NCCR,TLP.....Wote ni siasa za kinafiq tu
 
CCM pamoja ubovu wake wote itatawala kwa muda mrefu sana nchi hii. Moja ya sababu ni kukosa upinzani ulio makini na ulio na mshikamano.
Watu kama ninyi mnaendelea kuishi tu kwa sababu CCM iko madarakani...jinsi inavyoyatwaa hayo madaraka kwenu si hoja bali hoja kwenu ni mtawezaje kuendelea kuneemeka bila CCM. Hebu nikuulize swali moja tu Bwa'Nchuchu, je CCM inaweza kudumu bila serikali kama vyama vingine angalau vilivyoweza kudumu? Je mkutano wa CCM ungeweza kuvamiwa kama tunavyoshuhudia kwa vyama upinzani?

Umeyaona yaliyowakuta Bashe, Msukuma, Nape (kwa kuwataja wachache waliojaribu kukosoa uongozi ndani ya CCM? Umemsikia tena Katibu Mkuu wa CCM tangu alipotoa maoni yake kuhusu uongozi wa juu ndani ya chama na serikali? Mnadharau upinzani lakini hamjui jitihada zao zinavyopigwa vita na vyombo vilivyotakiwa kuvilinda. Bila serikali CCM haiwezi kudumu hata kwa saa ishirini na nne...itasambaratika.
 
Unamjua Magdalena Sakaya?
Habibu Mnyaa?
Kambaya?

mbona hao wote wanamtambua Lipumba?

Kinachosikitisha ni kuwa Magdalene Sakaya asingepata Ubunge kama siyo akina Mbowe na Chadema lakini leo ameshapata Ubunge anawaona wale waliompigia kampeni siyo kitu MTU ni Lipumba aliyewasaliti.Ila wakija kushtuka Lipumba kaisha lipwa wanabaki Wenyewe
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Watu kama ninyi mnaendelea kuishi tu kwa sababu CCM iko madarakani...jinsi inavyoyatwaa hayo madaraka kwenu si hoja bali hoja kwenu ni mtawezaje kuendelea kuneemeka bila CCM. Hebu nikuulize swali moja tu Bwa'Nchuchu, je CCM inaweza kudumu bila serikali kama vyama vingine angalau vilivyoweza kudumu? Je mkutano wa CCM ungeweza kuvamiwa kama tunavyoshuhudia kwa vyama upinzani?

Umeyaona yaliyowakuta Bashe, Msukuma, Nape (kwa kuwataja wachache waliojaribu kukosoa uongozi ndani ya CCM? Umemsikia tena Katibu Mkuu wa CCM tangu alipotoa maoni yake kuhusu uongozi wa juu ndani ya chama na serikali? Mnadharau upinzani lakini hamjui jitihada zao zinavyopigwa vita na vyombo vilivyotakiwa kuvilinda. Bila serikali CCM haiwezi kudumu hata kwa saa ishirini na nne...itasambaratika.

Ni ukweli wasiopenda kuusikia.Bila Serikali na Jeshi CCM haiwezi kudumu hata masaa mawili
 
Mbowe na vijana wake ndio wanataka yasiishe haya ili wabaki wao kama chama dume cha upinzani na waendelee kutafuna ruzuku kwa raha zao,hilo Maalimu halioni kwani siku zinavyozidi kwenda Maalim anakuwa sawa na joka la Kibisa,hebu angalie hivi sasa kuna ukawa kweli?NLD imekufa na Makaidi wake,NCCR sijui imebaki Vunjo na Mbatia wake sijui kapotelea wapi siku hizi,CUF ndio imekuwa nusu mkate ,Chadema ndio wanazidi kuongeza kuni kwani vita vya panzi furaha ya kunguru chadema

Mie nilikuwa MTU wa kwanza kupinga Umoja wa vyama vya Siasa hasa kuhusisha CUF Bara,CUF Zanzibar wanamsimamo.siyo Bara.CCM kuwapa Pesa akina Lipumba wameshindwa kuvumilia wamepokea ili mradi kuua Upinzani.
 
Ni mwendawazimu tu asiyekubali kuwa kujitoa kwa Lipumba na kurudi ofisini kwa nguvu ndiyo chanzo cha huu mgogoro.

Acheni unafiki.

Kawaida ya CCM wakishanunua MTU,watampa sifa zote za Duniani na Motoni na watamlinda kweli kweli.Leo ati waliopigwa na akina Ka mbaya wanatungiwa mashtaka na wahalifu wanapata duh!IPO Bongo tu hii.
 
Kuna Vitu huwez kukaa ukasamee, ebu twambie nini nia ya lipumba kukiacha chama katika ile mda wa kampeni pamoja na kupigiwa magoti sana. Hivo unaweza kudharau nguvu ya lowasa katika ushindi wa SAKAYA.
Hivo ni kweli huoni ni namna gani Lipumba anatumika, Harafu eti wakae meza moja, ili iwe nini.

Unayemjibu ni Kada wa CCM, unapoteza muda.
 
Exactly...

Unajua kuna mambo mengine si ya kuyaweka hadharani.

Hivi kwa mfano unadhani CCM huwa hawakosani? Wanakosana sana na kutofautiana lakini ni nadra sana kuona viongozi wao waandamizi wakikwazana hadharani.

Huwa wanayamaliza nyuma ya pazia huko.

Lakini hawa wapinzani....hahaaa....so disappointing.

Nyuma ya ugomvi wa CUF ipo Serikali na CCM, kibali kata.Haingii akilini waliopigwa ndiyo wafunguliwe mashtaka na wavamizi wako huru hii ipo Darisalama tu.
 
Kuna kitu hakizungumzwi sana

ukweli ni kuwa CUF walikuwa na mgogoro wa chini chini wa siku nyingi
kuhusu CUF Zanzibar na CUF bara

UKAWA imetumka tu kuongeza mgogoro hasa kwa CUF bara
kuona CUF Zanzibar wanapora madaraka yoote
Lipumba kaona tu a loop hole la kuwa relevant na kupiga pesa
now kutoka CCM

Solution ni CUF Zanzibar wakubali tu kuwa kuna mgogoro
na wawe ready kuutatua..kuliko kudai tu ni Lipumba ndo mwenye matatizo

Lipumba anapataje support za hadi wabunge?au mtu kama Mnyaa?

tatizo la CUF linazidi kukua now lakini busara ikitumka linaweza kuisha

Kwa post yako hii, nadhani wewe si yule The Boss wa kujenga hoja zenye mantiki.

Yaani kati ya wabunge wote wa cuf bara, ni wawili tu ndio wanamuunga mkono pumba; nawe unaona hapo kweli pumba ana support kubwa. Hivi umewahi kujiuliza kwa nini pumba ana support ya serikali katika mambo ayafanyayo katika kukuza mgogoro huu?
 
Kuna kitu hakizungumzwi sana

ukweli ni kuwa CUF walikuwa na mgogoro wa chini chini wa siku nyingi
kuhusu CUF Zanzibar na CUF bara

UKAWA imetumka tu kuongeza mgogoro hasa kwa CUF bara
kuona CUF Zanzibar wanapora madaraka yoote
Lipumba kaona tu a loop hole la kuwa relevant na kupiga pesa
now kutoka CCM

Solution ni CUF Zanzibar wakubali tu kuwa kuna mgogoro
na wawe ready kuutatua..kuliko kudai tu ni Lipumba ndo mwenye matatizo

Lipumba anapataje support za hadi wabunge?au mtu kama Mnyaa?

tatizo la CUF linazidi kukua now lakini busara ikitumka linaweza kuisha
Sasa mbona hoja zako zina contradict, unasema mgogoro ni CUF Zanzibar na CUF bara. Kisha unasema Mnyaa anamuunga mkono Lipumba. Kwani Mnyaa ni CUF bara?
 
Kabisa...si viongozi si wafuasi!

Ukiwekeza matumaini yako kwao basi jua unaji set up kwa major disappointment.

Na ukitaka ujue wapo kimaslahi binafsi...angalia mafao yao wabunge pindi wamalizapo mihula yao.

Huwa wanachukua si chini ya milioni 200 na kamwe huwa husikii wakishikia bango matumizi ya kiasi hicho cha fedha za walipa kodi huku kuna watumishi wa umma waliohenyeka miaka 30 kulitumikia taifa na hawapati kiasi kama hicho pindi wanapostaafu.

CCM pamoja ubovu wake wote itatawala kwa muda mrefu sana nchi hii. Moja ya sababu ni kukosa upinzani ulio makini na ulio na mshikamano.

Kama Tanzania ningekuwa na fair play Wapinzani wanapewa haki sawa na CCM Leo CCM ingekuwa maiti.

Wakati CCM wakifanya Mikutano Wapinzani wanapewa onyo na polisi.Wakati Lipumba akifanya Mikutano Seif ananyimwa sababu Lipumba ni kiatu kilichowekwa na CCM.

CCM inatumia Kodi zetu na nguvu kubwa kuua Upinzani na Nina uhakika siku CCM ikishindwa Uchaguzi itafanyavurugu kubwa mno.CCM bila Jeshi hakuna ushindi.
 
The Boss,

..kwa maoni yangu kinachowaweka pamoja ccm ni vyombo vya dola.

..lingine ni utitiri wa vyeo ambavyo Raisi/ Mwenyekiti wa CCM anaweza kuvitumia kama kishawishi kwa mwanachama yeyote yule ambaye hajaridhika.

..Mwenyekiti wa CCM asiyekuwa na dola nyuma yake asingeweza kumdhibiti mwanachama aliyekuwa anaungwa mkono ndani ya chama kama Edward Lowassa.

..Pia umeona jinsi Mwenyekiti wa CCM alivyoweza kutumia madaraka yake ya Uraisi kumteua kada Dr.Nchimbi ( ambaye alileta ukorofi ktk chama)kuwa balozi.
 
Seif ndio tatizo la CUF toka seif aingie CUF wakati wa J.Mapalala Seif amekuwa akitumiwa na CCM kuhujum upinzani nchini wale wanao hoji kurudi kwa Lipumba baada ya kujiuzuru mbona hawahoji nini kiliafikiwa katika maongezi baina ya Seif Sharif na Kamati ya maridhiano baada ya uchaguzi kule Zanzibar Sharifu Hamadi anamtuhum Lipumba alie hoji makubaliano yasiri yaliofanywa na Sharifu Hamadi pamoja na Mbowe na Lowasa nakujipatia kitita cha pesa zilizowekwa kwenye ACOUNT yake binafsi kabla ya uchaguzi Sharifu anamuona Lipumba kama kikwazo kwake hasa kitendo cha kambi ya Lipumba kubadili account ya chama kabla wakati Sharif na mtatiro walipokuwa wakinufaika hapakuwa na mgogoro wowote kitendo cha msajiri kuzuia ruzuku kwa Seif kimezua mgogoro katika CUF
Hili gogoro linachochewa zaidi na Mbowe kwa maslahi ya Chadema kisiasa kwa upande wa Bara na upande wa Lipumba unapewa Baraka na CCM kwa kummaliza Sharifu kwa upande wa Zanzibar hasa kwa uchaguzi wa 2020 CCM Zanzibar haina mtu sahihi wakushindana na Seif hivyo kuwepo kwa mgogoro huu ni mtaji MKUBWA kwa CCM
Ila ikumbukwe Uimara wa Lipumba ndio ulio mfanya Sharifu kuwa sehem ya serikali ya umoja wa kitaifa mwaka 2010 ila usaliti wa seif kwa Lipumba ndio chimbuko la mgogoro huu miongoni mwa mipango ya chama ilikuwa pale CUF Zanzibar itakapo kuwa sehem ya serikali itaweza kupata pesa nyingi kutoka serikali ya Zanzibar pesa ambayo ilitakiwa itumike kujenga chama bara na Zanzibar lakini matokeo yake Sharifu alihodhi pesa za chama nakuzifanya kuwa pesa za CUF Zanzibar pekee huku yeye akiwa mnufaika zaidi katika pesa hizo, huku CUF ya bara ikiambulia pesa kiduchu katika uendeshaji wake
Naamini kama Hamadi ataendelea kufanya ubabe dhidi ya Lipumba naamin Mwisho wake kisiasa utakuwa umefika ila naamini kuna uwezekano mkubwa Sharifu kuhamia Chadema na kuachana na CUF na hili litakuwa kosa kubwa kisiasa kwa mzee Sharifu Hamadi
 
Lipumba na Seif hawawezi kuyamaliza matatizo yao kwa njia ya usuluhishi. Lipumba hana incentive ya kumsikiliza Seif, kwasababu bwana wake CCM ana mkwanja mrefu na anampa mpaka ulinzi. Na Lipumba sasahivi anaonekana motive yake ni relevance na pesa tu. Hivi vyote anavipata kwa wingi mno kutoka CCM, na hawezi kuvipata kwa huo wingi akiwa CUF. Seif is doomed, kwasababu anakabiliwa na dola. Chadema sielewi wanafaidikaje na mgogoro wa CUF. Na sijui hata wanaingiaje kwenye huu mgogoro.
 
Back
Top Bottom