CUF ilikuwa na mgogoro kabla ya UKAWA

CUF ilikuwa na mgogoro kabla ya UKAWA

Hakuna chama chochote cha siasa kikubwa ambacho hakina migogoro ya ndani. Hata CCM wana migogoro ya ndani na ushahidi ni kufukuzwa kwa hivi karibuni kwa baadhi ya Wakongwe ndani ya chama hicho akiwemo Mwenyekiti wa UWT ambaye pia amepoteza Ubunge wake na kauli za hivi karibuni kama hizi za Kinana na Bashe.





Huyu Lipumba alishajiuzulu ndani ya chama na akawaita waandishi wa habari kujiuzulu kwake na pia kupeleka barua CUF kuhusu kujiuzulu kwake. Baada ya kujiuzulu akataka kurudi ndani ya chama kinyemela na akakataliwa na CUF wakatumia taratibu husika kama zinavyoruhusiwa na katiba yao kumfukuza huyu Lipumba.

Huu mgogoro wa CCM bara wanaokuza ni Serikali kwa nia tu ya kuisambaratisha CUF/UKAWA. Msajili wa vyama hana haki ya kuingilia mambo ya ndani ya CUF lakini cha kushangaza huyo msajili kaamua kufanya hivyo na kudai yeye anamtambua Propesa Lipumba ambaye alijiuzulu na pia kufukuzwa ndani ya CUF.

CCM KAMWE haiwezi kabisa kukubali kuingiliwa katika mambo yao ya ndani kwa mfano hao waliofukuzwa CCM warudi kinyemela na waruhusiwe kuongeza mfarakano uliopo ndani ya CCM ikiwemo ule wa Wabunge wa CCM kutokuwa na imani na Majaliwa.

Propesa Lipumba ndiye mwenye matatizo hilo halikwepeki hata chembe alijiuzulu na pia kufukuzwa ndani ya chama hivyo si mwanachama halali wa CUF lakini anatumika na hii Serikali dhalimu kuisambaratisha CUF na UKAWA.



Uhuni unaofanywa wa kumtumia Lipumba kufanya fujo ndani ya CUF tena kwa kutumia watu wanaofahamika KAMWE hauwezi kukubalika. Hili likiachwa liendelee linaweza kusababisha maafa makubwa sana kama tuliyoyaona katika uvamizi uliotokea Jumamosi.



Kuna kitu hakizungumzwi sana

ukweli ni kuwa CUF walikuwa na mgogoro wa chini chini wa siku nyingi
kuhusu CUF Zanzibar na CUF bara

UKAWA imetumka tu kuongeza mgogoro hasa kwa CUF bara
kuona CUF Zanzibar wanapora madaraka yoote
Lipumba kaona tu a loop hole la kuwa relevant na kupiga pesa
now kutoka CCM

Solution ni CUF Zanzibar wakubali tu kuwa kuna mgogoro
na wawe ready kuutatua..kuliko kudai tu ni Lipumba ndo mwenye matatizo

Lipumba anapataje support za hadi wabunge?au mtu kama Mnyaa?

tatizo la CUF linazidi kukua now lakini busara ikitumka linaweza kuisha
 
Nina mashaka sana na akili za sefu.Si aliitwa buguruni na lipumba wakazungumze?sawa hamtambui lipumba je na ofisi ya buguruni nayo haitambui kama ni ya cuf,Buguruni kuna kiti na meza yake pale kwa nini sefu kaamua kutokanyaga?
Huyu sefu anapenda sana kuwafanya wafuasi wake mafala.Ndio maana kila akiamka anawaambia kesho napewa urais na wao wanakubali wanaenda kuuza supu za mapweza maisha yanaendelea tu
 
Sidhani kama Chadema watakuelewa...

Kama ambavyo CCM hawataki CUF ya Lipumba na CUF ya Sefu waungane, ndio hivyo Chadema hawataki Lipumba na Sefu washirikiane....
Nakubaliana na wewe, tatizo la cuf hivi sasa ni kukubali kufanya siasa kwa manufaa ya vyama vingine. ccm inanufaika na cuf-bara na chadema cuf-zanzibar. ni ngumu kwao kwa sasa kukaa meza moja
 
JAJI MUTUNGI,

Ameibuka leo hii na kudai kuwa amesikitishwa sana na vurugu walizofanyiwa viongozi wa CUF pale Vina Hotel.
Mutungi anasema ati ameumizwa sana ni kitendo hicho na eti amepanga kutukutanisha sisi na Lipumba. Shame!

...
Mutungi huyu huyu anayesema hatambui maamuzi ya Mkutano Mkuu wa CUF Taifa ambao ulithibitisha kujiuzulu kwa Lipumba kwa maamuzi ya asilimia 70 ya Wajumbe wote, huku akijua kuwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria ya vyama vya siasa na kuingilia masuala ya ndani ya vyama.

Ni Mutungi huyu huyu ambaye alimtangaza Lipumba kuwa Mwenyekiti wa CUF huku akijua kuwa maamuzi ya nani ni kiongozi wa chama cha siasa hufanywa na vikao vya juu vya chama.

Ni Mutungi huyuhuyu anayesema hatambui maamuzi ya Baraza Kuu halali la CUF ambalo lilishamfukuza Lipumba uanachama, likawasimamisha kina Sakaya uanachama n.k. huku hivi sasa akimshawishi Lipumba ajianzishie Baraza Kuu lake (FEKI) huku akitambua maamuzi ya Baraza hilo la Lipumba.

Ni Mutungi huyuhuyu ambaye anamshawishi Msajili wa RITA aitambue Bodi ya Wadhamini Feki iliyoundwa na Lipumba kwa kushauriwa.

Ni Mutungi huyuhuyu aliyeshiriki kutorosha fedha za CUF, Shs. Milioni 400 na kuziweka kwenye akaunti isiyotambuliwa na chama kisha kusimamia uhamishwaji wake kuelekea kwenye akaunti ya mtu binafsi na kisha fedha hizo kutolewa kwenye mabegi hadi nyumbani kwa Lipumba ambako ziligawanwa kama karanga.
________________________

Mutungi ameshapoteza hadhi ya kuwa jaji, hana hata hadhi ya kuwa hakimu. Nchi hii inao majaji wanaojiheshimu sana, Mutungi si mmoja wao. Aibu zake za kukubali kutumiwa na dola bila chembe ya soni, zitamtafuna hadi kaburini.

Yeye Mutungi ndiye chanzo cha yote haya, Mazombi, Maninja, Majambazi, Mungiki, Wavamizi, Wabeba bastola, mapanga.... Watekaji n.k.

Mutungi hana pa kujificha tena na kama anahitaji mazungumzo hebu awakutanishe SOPHIA SIMBA na MAGUFULI. Shame!

Julius S Mtatiro.
 
Hiii nchi ya ajabu kwelikweli, mkitofautiana mawazo unageuka msaliti! Hizi ni fikra potofu na bila kukubali changamoto hatutaendelea. lazima ifike mahali tukubaliane kutokukubaliana ili tofauti ziwekwe kando na matatizo ya msingi yatatuliwe, unless tutaendelea kuwa wapinzani milele
Ni ajabu sana, eti ukitofautiana na CCM unabatizwa kuwa shujaa/kamanda. Lakini ukitofautiana na UPINZANI mara moja unavalishwa joho la usaliti. Prof. Lipumba, Dr. Slaa na Lowasa wote wanastahiki tuwaweke katika kapu moja kwa kuvikimbia vyama vyao wakati wa vita vya uchaguzi.
 
Unamjua Magdalena Sakaya?
Habibu Mnyaa?
Kambaya?

mbona hao wote wanamtambua Lipumba?

Kila shetwan hakosi mbuyu wake. Hao walikuwa mashetwan tangu waingie CUF. Walipoupata upenyo huu ndo wamejionesha makucha yao. Lakini, mwisho ndo ushafika
 
Back
Top Bottom