CUF Habari
JF-Expert Member
- Dec 12, 2019
- 239
- 234
(CUF – Chama Cha Wananchi)
Office of The Secretary General
P.O. Box 10979 Dar Es Salaam, Tanzania
Office of The Secretary General
P.O. Box 10979 Dar Es Salaam, Tanzania
TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI.
CUF-Chama Cha Wananchi kimebaini mpango wa Muendelezo wa Viongozi wa CCM kuwa rubuni na kuwahamisha Madiwani wake Saba (7) wa Jiji la Tanga kijiunga na Chama hicho .
MADIWANI HAO NA KATA ZAO NI
NASSORO MOHAMMED wa Kata ya Tongoni
MOHAMMED ANIU wa Kata ya Tangasisi
MSWAHIRI NJAMA wa Kata ya Chongoleani
HABIBU MPA wa Kata ya Ngamiani Kati
SAIDI ALEI wa Kata ya Masiwani
AKIDA OMARI AKIDA wa Kata ya Ngamiani Kaskazini
SELEMANI LDDY MBAROUK wa Kata ya Majengo.
Waheshimiwa Wananchi na Wanachama wetu , Madiwani tajwa hapo juu wanatarajia kujiunga na CCM kesho kwenye Mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM utaofanyika Tanga Kwa hivyo hampaswi kushtuka bali tukio hilo linapaswa kuwaongezea Chachu na Morali ya kuiondoa CCM kwenye Uchaguzi Mkuu kama mlivyofanya Mwaka 2015.
Upinzani Kwa Jiji la Tanga si Kwa hao wanaotarajiwa kujiunga na CCM bali upinzani upo nyoyoni mwa Wanatanga Kwa kuzingatia historia ya Jiji la Tanga.
Mwisho CUF-Chama Cha Wananchi kinawataka CCM waache kujisumbua Kwa kununua Madiwani wa CUF kwani hilo si suluhisho la chuki ya Wananchi dhidi ya CCM.
CCM inapaswa kujikita katika kuboresha huduma za Jamii , kuzalisha Ajira na kuongeza pato la Mtanzaji na Taifa Kwa ujumla ndio njia pekee itayofanya Wananchi si wa Tanga tu bali maeneo mengi kufikiria kujiunga nao.
ABDUL KAMBAYA
MKURUGENZI WA HABARI
CUF-CHAMA CHA WANANCHI
MKURUGENZI WA HABARI
CUF-CHAMA CHA WANANCHI