Crdb wanakata hela kwenye mshahara wako?

Crdb wanakata hela kwenye mshahara wako?

Mpangamji

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2010
Posts
540
Reaction score
141
Nimejaribu kufuatilia mshahara wangu kila mwezi unapoingia CRDB nakatwa Tshs 4,000 ambayo imeandikwa EFT hii inakwata kwa ajili gani, maana kwa uelewa wangu ni kuwa monthly charges nalipa na pia mwajiri wangu anakatwa hela anazoziita bank charges kwa ajili ya mshahara wangu. nimeongea na jamaa yangu mmoja wa agent ya serikali yeye ameangalia akaona anakatwa Tshs 3,000 ambayo imeandikwa commission to .....(jina la agent).

Tunaweza kuwa tunachangia hela bila ridhaa zetu. Mwenye ufahamu zaidi afafanue. au kama hujui basi angalia statement yako baada ya mshahara kama unatumia bank ya CRDB.

Nawasilisha
 
Nimecheki.Kwangu hakuna hiyo kitu! Weka bstatement yako hapa tuone, tukushauri.
 
ngoja nichek bongo hapafai hapa

ni kweli wanakata na mshahara ukichelwa ukaingia mwezi mpya kama salio lako ni less than TSH 4,000 basi inaonesha negative. so unadaiwa na benki.....wizi mtupu!!
 
Kuweka Pesa benki si akiba ni kuitajirisha Benki. ukiwaomba Bank Statement wanakuambia elfu 20. ATM kadi inalipiwa kila mwezi hata kama hukutoa Pesa. Bora tukazichimbie ardhini huko hazikatwi!
 
Jamani imekuaje hiyo? Mimi nimejaribu kuangalia ktk benki statementi yangu, toka jan 2013 mpaka sasa sioni kitu! Labda nyie 'mnaokatwa' mngeenda benki kuuliza na mtuletee majibu mujarabu..
 
Hiyo ni Salary Processing Fee, ndio hivo serekali tapeli inakaba hadi penati na kutafuta ela kwa nguvu kutoka kwa sisi wazawa wavujajasho ilhali rasilimali ambazo zingekua sources za uhakika za income wanawapa wazungu na wachina. Cha msingi waajiriwa mkate shauri kugomea huu uizi wa mchanamchana, enzi za mwalimu mbona mambo haya hayakuepo? makato kila kona na bado hatuoni ahueni yoyote ktk huduma za kijamii. #hopeless .
 
Hiyo ni Salary Processing Fee, ndio hivo serekali tapeli inakaba hadi penati na kutafuta ela kwa nguvu kutoka kwa sisi wazawa wavujajasho ilhali rasilimali ambazo zingekua sources za uhakika za income wanawapa wazungu na wachina. Cha msingi waajiriwa mkate shauri kugomea huu uizi wa mchanamchana, enzi za mwalimu mbona mambo haya hayakuepo? makato kila kona na bado hatuoni ahueni yoyote ktk huduma za kijamii. #hopeless .

Sasa wadau kama hiyo inaitwa salary processing fee, kazi ya monthly fee na charges anazolipia mwajiri ni za nini?
 
Sasa wadau kama hiyo inaitwa salary processing fee, kazi ya monthly fee na charges anazolipia mwajiri ni za nini?
Kwa mujibu wa taarifa nilizokusanya ni kua salary processing fee inaeza kulipwa na mwajiri au mwajiriwa.
 
hamna bank isiyo charge mwaka jana benki zote ziliwahi kupublish charges zao sema ilikuwa kwenye guardian hivyo wachache walisoma crdb na nmb charges ndo zilikuwa chini ukiringanisha na mabenki mengine soo usidanganyike
 
Back
Top Bottom