CRDB Tawi la Chanika mmeniibia

mkuu uwe unahesabu kwanza kabla hujaondoka counter, teller wenyewe huwa wanakosea ndio maana wanataka ujiridhishe, ukiwaamini na ukaondoka kumbe pesa imepelea hiyo inakuwa uzembe wako mwenyewe
 
Mkuu hivi kwa yale mazingira ya bank unaweza kukaa Counter ukahesabu hizo elfu tano tano mpaka zifike mfano milioni 4. Huku kuna kuna msululu wa watu umekaa nyuma wanakusubiri ?
atumie mashine vinginevyo ahesabu hata kama atatumia masaa mawili. unaharakia wapi kwani
 
Halafu Nmb kwanini hamtaki kufungua tawi Chanika ?mnatusumbua sana aisee huku kuna wakazi (sio yule wa hip hop)wengi sana ila huduma tunafata gomz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu uwe unahesabu kwanza kabla hujaondoka counter, teller wenyewe huwa wanakosea ndio maana wanataka ujiridhishe, ukiwaamini na ukaondoka kumbe pesa imepelea hiyo inakuwa uzembe wako mwenyewe
Cha muhimu wawe waaminifu maana nasikia ndo mchezo wao

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Anahesabu tena vizuri sana na skrini anakugeuzia, kupigwa ni pale mrembo anazitoa hizo noti kwenye mashine ili azipange akukabidhi.

Zimehesabiwa mbele yako hivyo hutakuwa na muda tena wala wasiwasi kuhakiki, naye anatumia vema mwanya huo kuchezesha noti mbili tatu ili maisha yasonge.

Mjini shule bwashee.
 
Hao hizo ndio tabia zao mkuu, siku nyingine hesabu mpunga wako hapo , mm pia imeshanitokea walinipiga 10,000 CRDB tabata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni njaaa sana Hawa wadada

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mada humu watu walizungumzia jinsi hao wahudum wanavyoiba. Wanazidondosha pale chini anapokua amekaa.
 
Mimi sio mvivu kabisa wa kuhesabu pesa hata unipe silver za mia tano tano kiasi cha milioni mbili nitahesabu vizuri tu sinaga ubishoo kabisa kwenye kuhesabu pesa


Sent using IPhone X
 
Kuna mpuuz mmoja alinipa mil4 alaf buku buku imagine...
 
Mimi sio mvivu kabisa wa kuhesabu pesa hata unipe silver za mia tano tano kiasi cha milioni mbili nitahesabu vizuri tu sinaga ubishoo kabisa kwenye kuhesabu pesa


Sent using IPhone X

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…