CRDB Salary Advance

CRDB Salary Advance

Baado...naona wanaivutia upepo....! Hawaelewi vyuma vimekazaaa!

Wanatumia mufilis yupi?!
Kuna wakala wa kudai maden yao ndo wanamtumia. Hahaah, jamaa bwn me nliwambia heaabu zangu ziko ovyo but jamaa amekomaa anasema TUONANE TUJUE TUNAFANYAJE
 
Crdb Salary advance......ni mkopo kwa wafanyakazi wanaopitishia mishahara crdb na pia wamejiunga na simbanking.

Kiwango cha chini cha mkopo ni Tzs 50,000 na kiwango cha juu ni tzs 1,000,000.

Ili kuomba mkopo ingia simbanking...kisha chagua namba 6. Inachukua dakika tatu kupokea mkopo wako. Fedha inaingizwa kwenye account yako ya mshahara.

Mkopo utalipwa kutoka kwenye mshahara wako unaofuata.

Riba ya mkopo ni asilimia 5. Mfano kwa mkopo tzs 100,000 riba yake ni tzs 5,000 tu.

Riba inatozwa upfront.

Jaribu namna mpya ya kusukuma mwezi!
Pesa ntakayochukuA ,italipwa kwa muda gan?
 
Mkuu ukiwa unachukua salary advance ya TZS 500,000 ili ukatwe mwisho mwezi na ukafanya hivyo kila mwezi kwa miezi 12 utailipa benki jumla ya TZS 300,000 (TZS 25,000 X 12) hiyo ni sawa na 60% (yaani TZS 300,000/500,000)

Mkuu hizi hesabu zako za wapi????
Mbona hiyo riba ya 25,000 ndio pekee umezidisha mara miez 12 na ukaacha kuzidisha hizo 500,000 ulizochukua kwa miez 12???
Atakayekatwa 300,000 kwa mwaka (25,000 × 12) atakuwa kapokea Milion sita (6,000,000) kwa mwaka (500,000 × 12).

So hiyo hesabu yako hapo juu ni ya uongo mkuu. Haupo sahihi. Stil itabaki 5%
 
Mbona Mimi nimejaribu kukopa naambiwa hawajaniunga????

Kuna aliyejaribu kukopa humu ndani na akafanikiwa????

Maana tusijetukawa tunatoa pongezi zisizo na uhalali
Mimi nimeshakopa Mara mbili sasa. Mara ya kwanza elfu 50, ambayo unaingiziwa moja kwa moja kwenye account kiasi cha elfu 47500, na mwezi huu nimeshavuta zangu 95000 ambapo watakata laki moja. Huduma nzuri sana hii. Haina haja ya kwenda kupiga magoti kwa mtu ili akukope kwa matangazo juu. CRDB for ever.
 
Hapana wewe si mtaalamu wa pesa; hapa ni kwamba kila mwezi utakuwa kwenye Overdraft ya laki tano maana unachukua na kurudisha na kuchukua tena hivyo mkopo utakuwa 500,000 "throughtout the year" ambao utalipia TZS 300,000 kwa kipindi chote cha miezi kumi na mbili. Pia ieleweke mkopo huu wa dharua huchukulia ndani ya mwezi mmoja na mishahara hutoka kwenye tarehe ya ishirini (20) hivyo kwa wastani utakuwa unakaa na hii pesa kwa nusu mwezi hivyo basi, faidi unayilipa kwa mwaka ni TZS 300,000/500,000 /0.5 = 120%.

Hiyo hesabu wataelewa waliosoma "Finance"
Kweli somo la hesabu halijawahi muacha mtu salama
 
Sio Kimei huyo. Hapo kuna vijana waliotoka UDSM wamebrain storm na kuja na hiyo idea then wakampelekea Kimei, Kimei akasign..
Nataman nikujibu hiv....! Hiv nyerere anapopewa sifa zooote za kuijenga nchii hii ....ni kweli kwamba idea zote zilikuwa zake?!

Wapo watu wengi sana wanaochangia jambo kutokea au kufanyika....lakin sifa zinakwenda kwa kiongozi.

Sijui hao unaosema wametoka ud....huko ud walikuwa wanasomea nini?!? Banking au?! Usikute ni watu tu wamepewa kutekeleza idea ambayo tayar ilikuwapo....mie kwa maoni yangu....anayefanya final decision ndo anapewa big up...the rest just take the back sit....! Thats how it works!
 
Yaani system ya riba ni kwere, Masikini utabaki na umasikini wako, na tajiri anaendelea kukukamua ulicho nacho! Yani ukikopa milioni, utarudisha 50k!! Wakati hiyo 50k ungeweza kuishi nayo kwa siku hata 10 ama 15 hadi 20 ukingojea mshahara wako hehehe
 
Jamaa wanasumbua, bahat nzur nlihama majuz apa. Wameshampa details zangu Mufilisi wao, ananitafta. Nafukuzana nao kwel kwel, siku wakinipata sjui tu.
Sa tunafanyaje mkuu, we hawajakuona...??
Hivi Chief hao TARA wanakopa vipi? Masharti yao.. Hao Branch mhh
 
Yaani system ya riba ni kwere, Masikini utabaki na umasikini wako, na tajiri anaendelea kukukamua ulicho nacho! Yani ukikopa milioni, utarudisha 50k!! Wakati hiyo 50k ungeweza kuishi nayo kwa siku hata 10 ama 15 hadi 20 ukingojea mshahara wako hehehe
Unaambiwa matajiri wote wanamadeni. Si shida sana kukopa 1milion nikarudisha kwa ongezeko la elfu 50 tu.
 
Yaani system ya riba ni kwere, Masikini utabaki na umasikini wako, na tajiri anaendelea kukukamua ulicho nacho! Yani ukikopa milioni, utarudisha 50k!! Wakati hiyo 50k ungeweza kuishi nayo kwa siku hata 10 ama 15 hadi 20 ukingojea mshahara wako hehehe
Hali iko hivi...

Unakwenda kukopa pale ambapo ndani umebaki na buku tu, na hakuna matumain ya kupata hela hivi karibuni. Let's say, tar 15 alafu umabakiwa na buku 5 baada ya kulipia mambo fulani muhimu kimaisha.

Atakayebaki maskini daima ni yule ambaye alikopa ili akaweke heshima bar...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom