officialBossmtoto
JF-Expert Member
- Jul 1, 2019
- 370
- 1,227
Habari ya humu wanajamvi. Kwanza kama kuna muhanga yeyote wa hili gonjwa ama anamgonjwa ama amepoteza ndugu yake kwa huu ugonjwa naomba niseme pole zangu za dhati.
Pili niseme kuupata sio tiketi ya kufa, ila umakini unahitajika ili kupata nafuu na hatimae kua na afya tele tena.
Dhumuni la uzi huu ni kuchakata namna huu ugonjwa utakavotubadili kama ukipita (wako wanaoamini kwamba huu ndo ule mda unaotajwa kwenye vitabu vya imani kwamba ni nyakati za mwisho)
Swala kubwa ni swala la kuagana katika safari ya mwisho (mazishi). Ukitazama wenzetu wengi wa mataifa ya ulaya, asia na marekani wamekua wakiaga mwili kitofauti na hata mazishi yao hua ya tofauti. Mara chache sana utakuta mkusanyiko wa watu. Kawaida huzungukwa na familia ya karibu na ndugu wachache
Licha ya kwamba mazishi yao pia hugharimu sana fedha nyingi hasa ukizingatia mara nyingi eneo la kuzika lazima ulilipie ila ingekua ghali zaidi kama wangefanya kama hapa kwetu
Nirudi nyumbani Africa ambapo kwenye msiba wa mtu utaona watu ambao hata hujui wanahusikaje hapo. Mjukuu wa mwalimu aliemfundisha shule ya msingi na yeye atakuepo msibani, shangazi wa rafiki wa nesi aliemshikia mkoba mke wake wakati anaenda kujifungua naye atakuepo.
Yaani msiba unakua kama mkutano wa kampeni
Unakuta marehem alifariki kwa kukosa matibabu ambayo yangegharimu laki nne tuu, ila msiba wake budget inawekwa milioni sita. Ukizingatia aliefariki ndo kichwa cha familia hivo familia ndo inaingia kwenye umaskini hivo ila hilo hawalioni
Kama tutapita Corona naona watu wachache sana kwenye mazishi
Ila kama wote tutakwenda kwa hili tatizo la kushindwa kupumua basi tena tutakutana kwenye hukumu panapo majaaliwa
Pili niseme kuupata sio tiketi ya kufa, ila umakini unahitajika ili kupata nafuu na hatimae kua na afya tele tena.
Dhumuni la uzi huu ni kuchakata namna huu ugonjwa utakavotubadili kama ukipita (wako wanaoamini kwamba huu ndo ule mda unaotajwa kwenye vitabu vya imani kwamba ni nyakati za mwisho)
Swala kubwa ni swala la kuagana katika safari ya mwisho (mazishi). Ukitazama wenzetu wengi wa mataifa ya ulaya, asia na marekani wamekua wakiaga mwili kitofauti na hata mazishi yao hua ya tofauti. Mara chache sana utakuta mkusanyiko wa watu. Kawaida huzungukwa na familia ya karibu na ndugu wachache
Licha ya kwamba mazishi yao pia hugharimu sana fedha nyingi hasa ukizingatia mara nyingi eneo la kuzika lazima ulilipie ila ingekua ghali zaidi kama wangefanya kama hapa kwetu
Nirudi nyumbani Africa ambapo kwenye msiba wa mtu utaona watu ambao hata hujui wanahusikaje hapo. Mjukuu wa mwalimu aliemfundisha shule ya msingi na yeye atakuepo msibani, shangazi wa rafiki wa nesi aliemshikia mkoba mke wake wakati anaenda kujifungua naye atakuepo.
Yaani msiba unakua kama mkutano wa kampeni
Unakuta marehem alifariki kwa kukosa matibabu ambayo yangegharimu laki nne tuu, ila msiba wake budget inawekwa milioni sita. Ukizingatia aliefariki ndo kichwa cha familia hivo familia ndo inaingia kwenye umaskini hivo ila hilo hawalioni
Kama tutapita Corona naona watu wachache sana kwenye mazishi
Ila kama wote tutakwenda kwa hili tatizo la kushindwa kupumua basi tena tutakutana kwenye hukumu panapo majaaliwa