COVID 19 in Tanzania analysis and next steps

Ujinga mtupu hapo umeandika. Wagonjwa wameongezeka kutoka idadi ya mtu mmoja hadi leo kufikia147 halafu unaandika upupu hapa kuwa eti tumejipanga vizur. Kweli wew jinga lao kama jina lako lilivyo. Tena hapo idadi hiyo inaweza ikawa imechakachuliwa.

Waziri wa Afya amesema utafiti unaonesha ugonjwa unaambukizwa hata kwa njia ya hewa, bado mnaruhusu mikusanyiko ktk Ibada eti mkaombee nchi ninyi kweli mnazo kichwani ? Yaani hata Kinjekitile Ngwale alikuwa na Akiri kuliko nyumbu ninyi.

Endeleeni kuambukixana huko ktk nyumba zenu za ibada mfe kixembe tuu ujinga ni mzigo. Mimi ni muumini mzuri sana lakini sidanganywi kizembe hivi. Maandiko yanasema Watu wangu wanaangamia kwa kukosa Maarifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunasubiri michango kwanza.

 
Kinachomaliza watu ni hofu kubwa,na matangazo makubwa.Tungekuwa hatujui kitu kila mtu angekufa kivyake hamna mwenye time
Waliokufa ni watano tu
Asilimia 90 wanapona
Wengi waliokufa walikuwa na magonjwa mengine.

Tupunguze panic

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Jingalao, lazima tukubali kuwa kuna mahali tulikosea.

Tulijua katika vita hii, askari wa mstari wa mbele ni wataalam wa afya. Kama huo ndiyo ukweli, kwa nini hatukuwaacha wataalam wa afya watupe maelekezo namna ya kuenenda badala ya wanasiasa kuwapa maelekezo wataalam wa afya namna ya kuenenda?

Kama tumegundua makosa tuliyofanya awali, japo tumechelewa, sasa tunatakiwa tuwaulize wataalam wa afya, tuenende namna gani katika hatua hii tuliyoifikia. Kama tutaendelea kuwapa nafasi wanasiasa wawape maelekezo wataalam wa afya, tutazidi kupotea.

Curve unayoisema, tungeweza kuiepuka kama tungekubali kujifunza kutokana na makosa ya wenzetu waliopata maambukizi kabla yetu. Kuna nchi hazitapita kwenye curve uliyoisema kabisa, kwa sababu walitumia makosa ya mataifa yaliyoathirika mwanzo, kujiwekea tahadhari ili nao wasiipite njia ya wale wa mwanzo. Sisi tulizembea, na tutalazimika kupita kwenye njia chungu.

Tuache siasa, tuwaache wataalam watuongoze. Mataifa yote wanasema wamekata chain ya maambukizi kwa lockdown. Sisi tunaamini tutakata chain kimiujiza!

Sasa ni wakati wa wataalam kusimama wima, na waiambie serikali namna tunavyoweza kuenenda ili kupunguza athari. Kwenye hili, ndugu zangu, bila kusikiliza wataalam na kutumia uzoefu wa wenzetu, tutaangamia.

Tafadhali Rais na watendaji wako wote wa Serikali, na viongozi wa dini, sikilizeni ushauri na maelekezo ya wataalam. Ombeni pia ushauri na uzoefu wa mataifa yaliyofanikiwa kudhibiti maambukizi na vifo.
 
Sifa ya kipekee itakayoenda Tanzania ni kufikia peak na ku control bila lockdown....
let see and wait.lockdown sio approval ya conrol worldwide...
 
Hawataki kucopy

Leo nimeona karantini moja watu wamefanya mkusanyiko wakiwa carantini yaani carantini haijali how to keep distance ( nchi za wenzetu karantin wanatakiwa kuachana 2mita) yaani sisi ni maigizo, si serikali wala umma.
 
Mleta mada na 90% ya wachangiaji wako mpo kupamba pamba uzembe unaofanyika

Mathalani unasema njia zetu za kujikinga ni scientifically. Hivi scientifically unaweza tofautisha mkusanyiko wa ibada na mkutano wa siasa?

Ifike mahala tuache uongo na unafiki
Tunakoelekea hatupajui na hatupaelewi
Chamsingi tusali
 
Afadhali mkuu umeliona hilo, nilifikiri nipo peke yangu. Kuna watu hawaoni hali halisi ili mradi visenti vichache wanavyolipwa kupiga propaganda ya kusifia mitandaoni. Ni Kama vile wamekaa sehemu moja na kukubaliana Cha kuandika na kutoa comments
 
Huu wakati wale wasiounga mkono juhudi wawe makini, unaweza ukashughulikiwa wakakujumlisha kwenye idadi ya wahanga wa corona 😳
 
Sifa ya kipekee itakayoenda Tanzania ni kufikia peak na ku control bila lockdown....
let see and wait.lockdown sio approval ya conrol worldwide...
Sawa lakini ni watuambie kwani Rais wa nchi tunamuona kama baba wa taifa hasa wale wanaomlilia kila kukicha.
Lakini mkuu wa nchi kakimbia ikulu iliyo ofisi yake.
Dar palimshinda kasema Feb 2020 atakuwa Dodoma nako hakai.
Mzee wetu wa msoga tulimsema kwa kuwa kwao ni karibu hakuna picknick ndiyo maana alikwenda ulaya.
Ni upuuzi kuwa na ikulu kila mkoa na wilaya kwa ajili ya Rais.
Karibuni tuliona anavinjari mawe ya chamwino vilevile kahawa ya geita na ekarist ya mlimani.

Juzi kwenye endorsement ya Biden, Obama alisema" mtu anayepaswa kuwa pale juu anapaswa kuongoza kwa maarifa, uzoefu, humility, sympathy, kindness, and so on"
What kind of leader do we have?

Catholic Bishop kwangu ni mfano wa kiongozi bora au mbaya, kwa kuwa anamamlaka ya kila kitu jimboni, anamaarifa ya kutosha na uzoefu wengi wanafanya vizuri endapo watakuwa na msingi WA kanisa yaani unyenyekevu WA yesu katika kutumika hasa kuongoza watu kimwili na kiroho badala ya kubaki kiroho au kimwili tu. Wapo wengi na daima wanafanya kazi vizuri kwa kuwa ni mababa hivyo utupenda wote waliowake anapobagua kwa ubinafsi ni kosa analoweza kutubu isipokuwa pale anapobagua kwa kufundisha fadhila ya uvumilivu na kuchukuliana kwa upendo, lkn daima maamuzi yake yasichelewe ili yeye asife au hasibabishe kifo cha kiroho au kimwili. Na daima katika nyumba zao wanakuwa na nafasi ya tafakuri ambayo uhuisha nafsi na maovu lkn kwa watawala muda huo ni mchache mwingi ni kusikiliza washauri na wapambe ambao hawakupi tafakuri japo mateso katk dhamiri sasa au baadaye.

Mtawala mwema huwa na mchache WA matendo, wasaidizi na kusikiliza watu na mwingi katika kuisikiliza dhamiri.

Nashkuru mh. Rais Jana ameamua kuisikiliza kweli dhamiri yake na kuomba maombezi ya taifa. Ni sawa lkn hatupaswi kubaki rohoni tu kwani Mungu hutenda kwa muda wake na haongwi kwa sala zetu.

Mipango ya kimwili inahitajika kupita hapa tulipo: tunakumbuka, mengi na pambe nyingi zilibubujia na neno UTEKELEZAJI WA AWAMU YA TANO sasa corona amekuja kubomoa na kutukumbusha usivyojali wahanga WA majanga. Tunaomba utuonyeshe namna ya kulinda uchumi uliojenga pia utuokoe ksma kikwete wakati wa ukame WA 2006-2008 kwa njaa.

Mipango ya corona na uchumi iwekwe mezani na serikali ndipo tutajiona tuko salama.

Moon jae in alipiga simu kwa wakuu WA nchi 20 na kuomba msaada kupambana na corona na simu sake ziliwekwa hadharani ili kutoa matumaini kwa wakorea kuwa anawapigania dhidi ya janga hili; na kwa hakika amepata viti 180 kati ya viti 300 kimsingi anekibeba chama.

Natamani Leo urudi magogoni na ufanye mikakati ya kutunusuru ukiwa karibu na unaowahitaji.

Tunajua ulitamani uvunje bunge mapema kwa hotuba ukiliacha liendelee, lkn matumaini hayapo tena. Endapo hautachukua hatua sasa ugonjwa huu utadumu kwa muda mrefu hivyo uchumi wetu utadoda.
 
Jibi moja kwako ni kuwa hakuna nchi itakayoacha kipita kwenye hiyo curve ...hiyo curve ni sehemu ya principle ya mlipuko.hata kipindupindu kilipitia hiyo curve
 
Jibi moja kwako ni kuwa hakuna nchi itakayoacha kipita kwenye hiyo curve ...hiyo curve ni sehemu ya principle ya mlipuko.hata kipindupindu kilipitia hiyo curve
Achana na curve, tupe mipango ya serikali yako. Mipango wezeshi kwa kuwa ushaur tulishatoa ni zamu yao kufanya uamuzi.
Kwan hata makanisa yalishauriwa na Leo kitima kakubali



 
Hebu muulize pascal mayallah mwezi mmoja uliopita alikuja na andiko la kuwaita watu "mashuja", afuu muulize kawaza nini Leo kaja na andiko la SWALI la haya unayoyapigia makofi na kuona watu wanahitaji kusifia ili Hali maambukiz yanaongezeka mara 3 Kila kukicha!!. Watanzania bwana yaani unaweza ukampamba mwenzako anafanya vizuri ili tu haja zako zitimie.
 

Mkuu mada kama hii tegemea kuungwa mkono na watu kama mgombea ubunge mtarajiwa 'manjaa.'

Wanaofika kwenye kilele cha curve hawafiki kwa maombi. Ni kwa kazi kubwa, maumivu na kujitoa sadaka.

Jaribu kujifananisha na hawa hawajakwenda kwenye maombi (hata mara moja) kwa ajili ya hii kitu, wako vizuri, hajafa mtu hata mmoja, wamepona wengi zaidi kuliko sisi, wana wagonjwa wachache kuliko sisi na wana kasi ndogo mno ya maambukizi (hata kuliko ya wanaopona).

Sasa wanaenda 45 days za total lockdown:





Mkuu tafiti zako unafanyia Lumumba?

Ukweli mchungu, hapa tumelikoroga ni lazima tu tubadilike na tuifuate njia sahihi ambayo iko wazi mno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…