ivibration
JF-Expert Member
- Oct 10, 2013
- 363
- 73
coup att
Wanajeshi 66 wauawa Sudan Kusini
17 Disemba, 2013 - Saa 13:09 GMT
Afisaa mkuu msimamizi wa hospitali ya kijeshi ya Juba, Brigedia Gen Dr Ajak Bullen,ameambia shirika la redio la Miraya mjini Juba kuwa wanajeshi 66 wameuawa katika mapigano ya siku mbili. Watafanyiwa mazishi ya pamoja.
Wakati huohuo afisaa mmoja wa serikali amesema kuwa watu 26 wameuawa katika mapigano ya siku mbili mjini Juba.
Zaidi ya watu miamoja wamejeruhiwa huku maafisa wakuu wakijaribu kudhibiti mji huo kufuatia kile ambacho serikali ilisema ni jaribio la mapinduzi mbalo liliweza kutibuliwa.
Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Kusini Barnaba Marial Benjamin amesema kuwa vikosi vya usalama vinawasaka wanajeshi watiifu kwa Riek Machar aliyekuwa makamu wa Rais wa Salva Kiir anayedaiwa kupanga njama hiyo ya mapinduzi.
Taarifa zinasema kuwa milio ya risasi ingali inasikika mjini Juba.
Source: BBC Swahili
99% ya wakazi wa huko ni cristian. sasa hivi dakika yoyote sudan ya kusini itasambaratika. watu wanauana baraza lote la mawaziri ni wakiristo . bunge na jeshi lote. ni wakati muafaka kuomba yasije yakatokea kama yanavyotokea Somalia
99% ya wakazi wa huko ni cristian. sasa hivi dakika yoyote sudan ya kusini itasambaratika.mauji ya kuviziana kama ya somalia
ni wakati muafaka kuomba isijekutokea kama somalia
mada yako imekaa kibaguzi!
Ni vema kwa mwanadamu yeyote mwenye hofu ya mungu kuombea amani popote pale duniani!
Kumekua na vita sehemu nyingi. Syria ni zaidi ya miaka 2 na africa ya kati, somali, drc, chad na sehemu nyingi tu!
Ni vema kumuomba mungu pamoja na kua ktk siku za mwisho moja ya dalili zake ni vita! Kwahiyo huu ni utungu tu ule mwisho bado!
wanadamu asili yetu ni kupenda sana mia nini malengo yetu madaraka bila kufikiri nini tunataka kuwafanyia wananchi. Sudan kusini walifurahia kujitenga bila kuwa na mipango dhabiti ya kujitawala.
jamaa anadhani sudan wanapigania kusimamishwa serikali ya kidini kama lra wa uganda wanaopigania amri kumi za mungu zitawale.