cutelove
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 3,317
- 7,509
Namshauri Rais kwa kasi hii ya maambukizi, tena mbaya zaidi kwa mara ya kwanza huu ugonjwa utafika vijijini
Namuomba mh Rais atangaze hali ya hatari ili kila mtu akae chonjo na vyombo vya dola viingie kazini kusaidia kudhibiti maambukizi
WHO walionya Afrika maambukizi Afrika kufika vijijini, sasa naamini Tanzania yatafika vijijini ndani ndani
Pia serikali itangaze kuanzia sasa hakuna mikusanyiko kwenye mazishi na yeyote atakayefariki kwa ugonjwa wowote asizikwe bila kupimwa na wanafamilia wanapaswa wawe makini na mgonjwa wao ambae ataugua kwa ghafla kuanzia sasa, watumie kinga kuwashika au kuwahudumia wagonjwa majumbani
Elimu ya ugonjwa huu itolewe vijijini kwa kasi, Yale maspika makubwa yanayofungwa CCM mbele kwa mbele, muda ndio huu yapite kila siku mitaani na vijijini kutoa elimu
Masoko na minada isitishwe, muda ndio huu
Namuomba mh Rais atangaze hali ya hatari ili kila mtu akae chonjo na vyombo vya dola viingie kazini kusaidia kudhibiti maambukizi
WHO walionya Afrika maambukizi Afrika kufika vijijini, sasa naamini Tanzania yatafika vijijini ndani ndani
Pia serikali itangaze kuanzia sasa hakuna mikusanyiko kwenye mazishi na yeyote atakayefariki kwa ugonjwa wowote asizikwe bila kupimwa na wanafamilia wanapaswa wawe makini na mgonjwa wao ambae ataugua kwa ghafla kuanzia sasa, watumie kinga kuwashika au kuwahudumia wagonjwa majumbani
Elimu ya ugonjwa huu itolewe vijijini kwa kasi, Yale maspika makubwa yanayofungwa CCM mbele kwa mbele, muda ndio huu yapite kila siku mitaani na vijijini kutoa elimu
Masoko na minada isitishwe, muda ndio huu