Congo na Tanzania tunatofautiana style ya matumizi ta kuongozi wa imra ya walio madarakani

Feb 7, 2015
85
37
Kwa mujibu wa Katiba ya DRC(Zaiire) leo ndio siku ya mwisho ya uongozi wa fascist Joseph Kabila. Kutokana na majukumu sijafahamu kinachoendelea Kinshasa kama jamaa kang'atuka au la.

Madikteta waliobaki ni pamoja na Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda, Pierre Nkurunziza wa Burundi, Omar Al Bashir-Sudan, Denis Sassu Nguesao-Congo-Brazzaville, Robert Mugabe wa Zimbabwe, na Rais wa Guinea ya Ikweta jina ().....yule wa Gambia anashughulikiwa na ECOWAS.

Paul Kagame anatakiwa kung'atuka kama anaheshimu demokrasia ya kweli........huu usanii wa kubadili katiba baada ya muda kuisha ni ufuska kisiasa.

Tanzania tuna saratani ya udikteta wa kimfumo........yaani unapokuwa ccm unakuwa sehemu ya saratani hiyo.

Tuendelee kuiombea Afrika, ila tuiombee zaidi Tanzania yetu. Ujambazi wa kisiasa uaofanyika hapa nchini ni mbaya kulilo udikteta ulioandikwa vitabuni.

Unaweza kujiuliza Ben Saanane amemezwa na chatu gani? Kama wamemchukua maharamia je serikali ya dhamana ya kusimamia usalama wa raia kwa kodi yetu inatumia kodi yetu kumtafuta Faru kuliko watanzania wenzetu waliopotea na ndugu hawalali tukimtafuata......ndio maana nasema bora ya nchi nyingine......huu upuuzi haujawahi kufanyika katika nchi yoyote katika sayari dunia.

[HASHTAG]#Justice4Lema[/HASHTAG]
[HASHTAG]#WeNeedBenSaananeAlive[/HASHTAG]

M4C Pamoja Daima
 
Back
Top Bottom